Hinweis: Um die korrekte Darstellung der Seite zu erhalten, müssen Sie beim Drucken die Hintergrundgrafiken erlauben.
Slider Bild - CC BY-NC-ND 4.0
1/1

Kisu kichaka

Sammlung Braun
r 2018 / 18293
Taasisi inayotoa
Museen Stade
Eneo la Mkusanyiko
Sammlung Braun
Nambari ya uvumbuzi
r 2018 / 18293
Kichwa
Kisu kichaka
Maelezo
"53. Kisu cha kutumia porini = mundu / Amani 24. mwezi wa 12. 1905 / TB. 46,63 / [Maelezo ya vitu vilivyotumika kwenye mchoro ] mbao Hyphaene coriacea, chuma / [mchoro]"
chanzo: Museen Stade, r 2018 / 18566, Inventarheft - Inventorybooklet - Kitabu chenye orodha ya vitu
mwandishi: Karl Braun

"Jumapili d. 24. Mwezi wa kuminambili 1905. [imepigwa mstari, u. 60] [S. 61] [...] jioni imekwenda [...] [?] yenye thamani ya kimila. Karibu zote nimetafutiwa na Max.Kasha ya ugoro kutoka pembe & ubao imenunuliwa hapa kutoka Mswahili (1 Rup.) Picha cha kufanana Abb. kwa Baumann. Usambara. 1891. u. 231. / kisuaheli: tabakero imetengenezwa na Wanjamwezi [mchoro wenye maelezo ya vilivyotumika] mbao pembe mbao /vitana, 3 kama vile nilivyovichora TB. 44, u.68.Kitana kimoja kama picha hapo & kimoja nimechongewa na Mnyamwezi hivi karibuni jina lake [?] kina umbile kifuatacho [mchoro] / kisuaheli: chanuo / kimetengenezwa kutoka mbao mweupe laini bila kupigwa msasa [u.62], wakati vingine vinatokana[sic] na fundi hutu huyu mmoja (fundi) anayekuwa fundi maalum kwa kutengeneza vitana. Hivi vina rangi ya manjano na ni laini. [mchoro] / vijiko vidogo na vikubwa zaidi vilivyochongwa vyenye mabambo ya kuchoma vina umbile vya mduara vingine havina kina vingine vyenye kina zaidi mapambo ya kuchora viko tofauti tofauti [michoro ya vijiko saba a-g, mingine yenye umakini upande wa mapambo yenye maelezo] kisuaheli: kijiko / mwiko / wu bu [?] / kijiko chenye kina kirefu: [mchoro h] [mchoro wa fidla wenye maelezo ya mali ghafi] fidla ya mbao shaba kibuyu boga mbao kisuaheli: nzumari [masahihisho zumari] [u. 63] Kifaa cha kukunia. Nusu nazi [masahihisho] hukuniwa kwenye chuma kama msumeno [masahihisho], wakati mkunaji hukalia kifaa.pande za mbao za kukaliwa huchongwa kutoka mbao mmoja & huweza kukunjwa. [michoro miwili,mmoja huonesha kitu kidogo mmoja] kisuaheli: mbuzi (maana halisi = mnyama mbuzi) / kisu cha porini kisuaheli huitwa"munde" . vingi vinatoka Ujerumani, ila hici ni vyembamba zaidi. [mchoro] Max amepokea picha mbili zilizotariziwa kwenye hariri yenye rangi ya giza kwa ajili ya kuninginizwa ukutani[u.64].Nilikuwa nimezinunua [?] pamoja na vitambaa vingine kwa Muhindi Tanga. Halafu kitambaa chepesi sana labda kutoka nyasi za nanasi kimetariziwa na vipepo kwa hariri nzito kitambaa cha mezani,kazi ya Wahindi. –"
chanzo: Museum der Kulturen Basel, VI 56197, Tagebuch - Diary - Shajara
mwandishi: Karl Braun
Vipimo
Urefu: 54,5cm
Nyenzo
Mbao,
Chuma
Kiungo cha dondoo
https://www.amani-stade.gbv.de/item/sw_ms_92c7544f-9e79-4891-8484-514bd7241c8d
nakala kwenye ubao wa kunakili
Kikundi cha kitu / kitu cha mtu binafsi
Kitu cha mtu binafsi
Uainishaji
Zana/vifaa (ujenzi wa meli)  
Uzalishaji
Wakati
mpaka 1905-12-24
Mahali
  • Tansania
Ethnolojia
  • Swahili  
Kununua / Uuzaji
Wakati
1905-12-24
Maelezo
"Jumapili 24. Mwezi wa kuminambili 1905. [imepigwa mstari, u. 60] [u. 61] [...] jioni imekwenda [...] [?] yenye thamani ya kimila. Karibu zote nimetafutiwa na Max. Kasha ya ugoro kutoka pembe & ubao imenunuliwa hapa kutoka Mswahili (1 Rup.) Picha cha kufanana. kwa Baumann. Usambara. 1891. u. 231. / kisuaheli: tabakero imetengenezwa na Wanjamwezi [mchoro wenye maelezo ya vilivyotumika] mbao pembe mbao / vitana, 3 kama vile nilivyovichora shajara 44, u .68. Kitana kimoja kama picha hapo & kimoja nimechongewa na Mnyamwezi hivi karibuni jina lake [?] kina umbile kifuatacho [mchoro] / kisuaheli: chanuo / kimetengenezwa kutoka mbao mweupe laini bila kupigwa msasa [u. 62], wakati vingine vinatokana [sic] na fundi hutu huyu mmoja (fundi) anayekuwa fundi maalum kwa kutengeneza vitana. Hivi vina rangi ya manjano na ni laini. [mchoro] / vijiko vidogo na vikubwa zaidi vilivyochongwa vyenye mabambo ya kuchoma vina umbile vya mduara vingine havina kina vingine vyenye kina zaidi mapambo ya kuchora viko tofauti tofauti [michoro ya vijiko saba a-g, mingine yenye umakini upande wa mapambo yenye maelezo] kisuaheli: kijiko / mwiko / wu bu [?] / kijiko chenye kina kirefu: [mchoro h] [mchoro wa fidla wenye maelezo ya mali ghafi] fidla ya mbao shaba kibuyu boga mbao kisuaheli: nzumari [masahihisho zumari] [u. 63] Kifaa cha kukunia. Nusu nazi [masahihisho] hukuniwa kwenye chuma kama msumeno [masahihisho], wakati mkunaji hukalia kifaa.pande za mbao za kukaliwa huchongwa kutoka mbao mmoja & huweza kukunjwa. [michoro miwili, mmoja huonesha kitu kidogo mmoja] kisuaheli: mbuzi (maana halisi = mnyama mbuzi) / kisu cha porini kisuaheli huitwa "munde". Vingi vinatoka Ujerumani, ila hici ni vyembamba zaidi. [mchoro] Max amepokea picha mbili zilizotariziwa kwenye hariri yenye rangi ya giza kwa ajili ya kuninginizwa ukutani [u. 64]. Nilikuwa nimezinunua [?] pamoja na vitambaa vingine kwa Muhindi Tanga. Halafu kitambaa chepesi sana labda kutoka nyasi za nanasi kimetariziwa na vipepo kwa hariri nzito kitambaa cha mezani,kazi ya Wahindi. –" [Utafsiri]

chanzo: Museum der Kulturen Basel, VI 56197, 46 (63)
mwandishi: Karl Braun
Mtu
  • Mtu, haijulikani (Mchuuzi)
  • Braun, Karl (* 1870 † 1935) (Mnunuzi)
    GND Explorer
Mahali
  • Amani
Malipo
Wakati
kutoka 1905-12-24
Maelezo
"53. Kisu cha kutumia porini = mundu / Amani 24. mwezi wa 12. 1905 / TB. 46,63 / [Maelezo ya vitu vilivyotumika kwenye mchoro ] mbao Hyphaene coriacea, chuma / [mchoro]" [Utafsiri]

chanzo: Museen Stade, r 2018 / 18566
mwandishi: Karl Braun
Mtu
Nambari za hesabu za zamani
  • 53
Urithi
Wakati
1934-07-17
Maelezo
Mnamo mwaka 1934, aliyekuwa mkurugenzi wa Taasisi ya Biolojia ya Kilimo na Misitu (Biologische Reichsanstalt für Land- und Forstwirtschaft) Karl Braun (1870–1935) alitoa kile kinachoitwa “Kolonialsammlung Braun” (Makusanyo ya Mkoloni Braun) kwa Jiji la Hanseatic la Stade, au tuseme aliyekuwa mwakilishi wake, meya wa wakati huo Hans Arthur Meyer (1884–1961). Tazama faili „Uhamisho wa makusanyo ya kikoloni kutoka kwa diwani mkuu wa serikali Profesa Dk. Karl Braun huko katika Jiji la Stade” („Überlassung einer Kolonialsammlung vom Oberregierungsrat Professor Dr. Karl Braun in Stade an die Stadt Stade") katika Jimbo la Saxony ya Chini Hifadhi ya Nyalaka ya Stade (Niedersächsischen Landesarchiv Standort Stade).

chanzo: Niedersächsisches Landesarchiv Standort Stade, Dep. 10 Nr. 03025
Mtu
  • Braun, Karl (* 1870 † 1935) (Mfadhili)
    GND Explorer
  • Hansestadt Stade (Mpokeaji)
  • Hans Arthur Meyer (1884 - 1961) (Mpokeaji)
Mahali
  • Stade
Mkopo
Wakati
1997-02-17
Maelezo
Mnamo mwaka 1997, aliyekuwa mtunza kumbukumbu wa jiji kwa wakati huo Jürgen Bohmbach anahitimisha makubaliano ya makabidhiano kwa mkopo wa kudumu katika Jumba la Makumbusho (Museumsverein Stade e.V.) chini ya aliyekuwa mkurugenzi wa wakati huo Gerd Mettjes kwa kutia saini. Baadaye, makusanyiko kutoka kwa Karl Braun yalihamishiwa kwenye Jumba la Makumbusho (Museumsverein Stade e.V.) kwa ajili ya utunzaji.

chanzo: Museen Stade, Vereinbarung Leihgabe "Brauns'sche Kolonialsammlung"
Mtu
Mahali
  • Stade
Scientific use:
Wakati
2023-06-09
Maelezo
I: sawa, tunaenda kwenye picha nyingine, tuna picha nyingine hapa imesajiliwa kwa namba 2018_18293_001, hebu angalia unaweza ukatambua ni kitu gani hiki R: hiki ni kisu, lakini hiki kisu kilikuwa ni cha mzee haswa, yani ukiambia 'kaniletee giatu ni jangu' yani unaambiwa kalete kile kisu changu, ni hiki I: ilikuwa inaitwaje R: 'tuni' I: ni kabila gani hiyo R: hicho ni kisambaa, kipare 'kahandwi', sasa haka ni kahandwi maalum, na kisu hiki hiki kinaweza kikawa cha kushevia watu kwenye kumaliza msiba, lakini visu hivi sasa vinmeandaliwa vinakuwa na wazee maalum wazee wa mila, sio kwamba utavikuta kwa mtu yoyote, lakini vilienda vikafikia sasa walipoingia vijana vikatengenezwa kwa wingi, wakati mwingine wazee waganga wa kienyeji wanachanjia chale navyo hivi, ni vikali mno sana, vinanolewa kwenye mawe maalum yale unayoniambia ni meusi I: kwa hiyo walikuwa wanatumia wazee R: wazee I: wa kuanzia umri gani R: miaka 60, 70 mpaka 90 unamkuta anacho amekaa nacho, akashindwa kukitumia lakini anacho, na anaweza akaacha usia nkifa amani kisu changu apewe karedio, sasa hapo haibadiliki, wewe labda uchukue useme na mimi nampa fulani basi, lakini hivi hivi hata huko kitawekwa mpaka uje I: kilikuwa kimeunganishwa na mila moja kwa moja R: ee I: na umesema kwa kila mtu sasa hivi anaweza kuwa nacho R: ndio I: unadhani ni kwa sababu gani imekuwa rahisi kila mtu kuwa nacho tofauti na miaka hiyo R: maadili yale ya mila yameporomoka hakuna kujali ile mila sasa, kwa sababu sasa hivi ukimwambia mtu kisu kitengenezwe usikipeleke kwenye cherehe ukinoe tu kwenye jiwe anakuambia we utaniua, amaezoea ‘chwaaaa’ akigeuza huku kimekuwa kikali anaondoka anaenda zake, zamani hamna cherehe, kuna mawe ya kunoa na kuna mawe ya kugongea........ I: hayo mawe maalum ya kunolea yalikuwa yanaitwaje R: 'ibwe' I: maana yake R: ni jiwe, yani ukiambiwa 'kaniendie ibwe maalum, unaagizwa na sehemu ya kulipata, hayapatikani patikani hovyo I: sawa sawa, na unaweza ukatuambia kitu hiki kilikuwa kinatengenezwa na akina nani hasa R: kilikuwa kinatengenezwa na wazee wazamani mababu wakarithishana hivyo hivyo, vikaenda vikafikia na watu wengine wanarithishwa kama hivi tunavyoongea mkasema kama mimi ninaweza kutengeneza hicho na mimi nikawarithisha I: na unaweza ukatuambia kisu hicho kilitengenezwa kwa kutumia nyenzo gani hasa R: ni vyuma ambavyo vinatengenezwa kwa kuchoma kwenye moto, yani hiyo miamba inayoenda kubomolewa ndio inawekwa kwenye huo tunaita 'mvuo', wanasema 'uvugwithwa' yana unavugizwa mpaka kinakuwa chekundu halafu anaweka kwenye jiwe wanapiga mpaka kinatokea hiki I: kwa hiyo ni chuma na kitu gani kingine ambacho kinaenda sambamba kwenye kutenganeza hiki R: labda mpini ndio kitu kingine kinaingia, maana huku kimetengenezwa kikawekwa chambamba ndio mpini wake na kujaribu kuboreshwa na vitu vingine, mwingine anavalisha ngozi ya........kuna mnyama kwa kipare anaitwa 'sunipaa', wale digidigi, vitu kama hivyo ndio ilikuwa ngozi zake zinachukuliwa kuvalishwa kwenye visu maalum kama hivi I: kwa nini mnyama huyo R: wanasema mnyama yule ana aina fulani ya baraka, ndio kama vile watu wanavyosema ukimpata kakakuona umepata kitu fulani au kuna baraka, au wakati mwingine wanasema kakakuona ukimuona mazingira ambayo sio ni balaa, sasa hivi vinyama unaweza ukakaa hapo nje hakuna pori hapo ukakaona kamesimama hapo, sasa wazee wakikaa wakutolea tafsiri kwamba ile ni balaa nenda katambikie, au ni neema wanategemea kimetokea muda gani I: sawa sawa, kwa hiyo ilikuwa inaashiria baraka, na huo mpini ulikuwa ni mti gani hasa ulikuwa ukitumika kutengenezea hiyo R: kuna mti unaitwa 'mzuu' kwa kipare wanaita 'mthuluu', hiyo ndio miti niliyokuwa ninaiona inatumika kwenye mipini ya visu maalumu na fimbo ya hao wazee, akitengenezewa fimbo yake ya kutembelea huku sijawahi kuuona I: kwa nini walikuwa wanatumia mti huo tu R: wanasema ni mti mgumu halafu ni mti wenye baraka I: kwa hiyo ni mgumu lakini unabaraka, na ndio maana wakatumia hata ngozi ya hivyo vinyama kwa sababu na vyenyewe vina baraka R: ndio vinaendana na kuleta baraka, unajua watu wa zamani wanatofauti, mimi marehemu babu yangu, nyoka mweusi anaingia ndani 'nyoka huyo, nyoka huyo' anasema hapana msimuue muacheni huyo nyoka, anaingia anakuja anatembea hapo baba anachukua chupa ya samli anammwagia yule nyoka, nyoka akatoka, anasema msimuue, kwa nini, anasema ameleta baraka, lakini ni mweusi, lakini kama ni wa kijani anasema ueni, wakijani akiingia anasema ni balaa ueni, kwa mfano hawa digidigi ninaosema anafukuzwa anakuja anaingia kwenye zizi, mara mbili mara tatu mimi nilishuhudia kwa marehemu babu yangu, anafukuzwa anaingia kwenye zizi la mbuzi, wawindaji wakija anawambia 'tafadhalini jamani angalia beberu hii na hii inayomfaa chukueni mmoja yule muacheni,' mzee mnyama wetu, yeye anawambia 'chukueni huyu yule muacheni amejisalimisha na ameleta baraka kwenye zizi langu la mbuzi, atakaa hapo na mbuzi mkifungua wanatoka wote wanaenda porini, sasa sisi hatuli yule mnyama kwa sababu hizo, anasema amekuja kwetu kujisaliisha haifai kumla. I: tuni kama hiyo, kwa sasa unaweza ukainunua shilingi ngapi R: hii sasa hivi labda shilingi elfu 5, haikuwa na vitu vingi sana vya usumbufu, ni vichache vichache kama nilivyokueleza

chanzo: Amani-Stade Project / Amani Field Research, Interview No. 5
mwandishi: I: Mohamed Seif, R: Anonymous
Mtu
  • National Institute for Medical Research (NIMR) (Mteja)
  • unknown actor (wissenschaftlicheR BearbeiterIn)
Mahali
  • Amani
Mwandishi: Karl Braun, Nukuu/Angalizo: Museen Stade, r 2018 / 18566jifunze zaidi
Mwandishi: Karl Braun, Tarehe ya kutengenezwa: 1905-12-24, Nukuu/Angalizo: Museum der Kulturen Basel, VI 56197, 46 (63)jifunze zaidi

Rejeo la ndani la kitu

Sanduku la ugoro

Sanduku la ugoro

r 2018 / 18431
Rejeo la ndani la kitu
Kuhusiana na
Chanuo la mbao

Chanuo la mbao

r 2018 / 18493 a
Rejeo la ndani la kitu
Kuhusiana na
Chanuo la mbao

Chanuo la mbao

r 2018 / 18493 b
Rejeo la ndani la kitu
Kuhusiana na
Chanuo la mbao

Chanuo la mbao

r 2018 / 18493 c
Rejeo la ndani la kitu
Kuhusiana na
Chanuo la mbao

Chanuo la mbao

r 2018 / 18493 d
Rejeo la ndani la kitu
Kuhusiana na
Kijiko cha mbao

Kijiko cha mbao

r 2018 / 18311
Rejeo la ndani la kitu
Kuhusiana na
Kijiko cha mbao

Kijiko cha mbao

r 2018 / 18220
Rejeo la ndani la kitu
Kuhusiana na
Kijiko cha kuchochea cha mbao

Kijiko cha kuchochea cha mbao

r 2018 / 18506 b
Rejeo la ndani la kitu
Kuhusiana na
Filimbi ya mbao

Filimbi ya mbao

r 2018 / 18504
Rejeo la ndani la kitu
Kuhusiana na
Kipasulio cha nazi, Mbuzi

Kipasulio cha nazi, Mbuzi

r 2018 / 18424
Rejeo la ndani la kitu
Kuhusiana na
Asili ya data ya kitu
Museen Stade
Leseni
Creative Commons Namensnennung, nicht kommerziell, keine Bearbeitung 4.0jifunze zaidi
Imepitishwa katika lango imewashwa
2025-12-04T15:38:39+01:00

Rekodi zetu za takwimu zinafanyiwa maboresho kila mara. Tafadhali wasiliana nasi ikiwa una maswali au maoni au ikiwa unahitaji taarifa zaidi au nyingine zinazohusu mali hii. Taarifa juu ya ulinzi wa takwimu.
Rudi kwenye utafutaji