Hinweis: Um die korrekte Darstellung der Seite zu erhalten, müssen Sie beim Drucken die Hintergrundgrafiken erlauben.
Slider Bild - CC BY-NC-ND 4.0
1/1

Mkono wa kusokotea nyuzi

Sammlung Braun
r 2018 / 18301
Taasisi inayotoa
Museen Stade
Eneo la Mkusanyiko
Sammlung Braun
Nambari ya uvumbuzi
r 2018 / 18301
Kichwa
Mkono wa kusokotea nyuzi
Vipimo
Urefu: 50cm, Kipenyo: 10cm
Nyenzo
Mbao
Kiungo cha dondoo
https://www.amani-stade.gbv.de/item/sw_ms_96096322-7d92-43e2-8480-0341db2950f7
nakala kwenye ubao wa kunakili
Kikundi cha kitu / kitu cha mtu binafsi
Kitu cha mtu binafsi
Uzalishaji
Wakati
mpaka ca. 1920
Mtu
  • Mtu, haijulikani (Mtengenezaji)
Mahali
  • Tansania
Acquisition:
Wakati
ca. 1904 - ca. 1920
Mtu
Mahali
  • Tansania
Urithi
Wakati
1934-07-17
Maelezo
Mnamo mwaka 1934, aliyekuwa mkurugenzi wa Taasisi ya Biolojia ya Kilimo na Misitu (Biologische Reichsanstalt für Land- und Forstwirtschaft) Karl Braun (1870–1935) alitoa kile kinachoitwa “Kolonialsammlung Braun” (Makusanyo ya Mkoloni Braun) kwa Jiji la Hanseatic la Stade, au tuseme aliyekuwa mwakilishi wake, meya wa wakati huo Hans Arthur Meyer (1884–1961). Tazama faili „Uhamisho wa makusanyo ya kikoloni kutoka kwa diwani mkuu wa serikali Profesa Dk. Karl Braun huko katika Jiji la Stade” („Überlassung einer Kolonialsammlung vom Oberregierungsrat Professor Dr. Karl Braun in Stade an die Stadt Stade") katika Jimbo la Saxony ya Chini Hifadhi ya Nyalaka ya Stade (Niedersächsischen Landesarchiv Standort Stade).

chanzo: Niedersächsisches Landesarchiv Standort Stade, Dep. 10 Nr. 03025
Mtu
  • Braun, Karl (* 1870 † 1935) (Mfadhili)
    GND Explorer
  • Hansestadt Stade (Mpokeaji)
  • Hans Arthur Meyer (1884 - 1961) (Mpokeaji)
Mahali
  • Stade
Mkopo
Wakati
1997-02-17
Maelezo
Mnamo mwaka 1997, aliyekuwa mtunza kumbukumbu wa jiji kwa wakati huo Jürgen Bohmbach anahitimisha makubaliano ya makabidhiano kwa mkopo wa kudumu katika Jumba la Makumbusho (Museumsverein Stade e.V.) chini ya aliyekuwa mkurugenzi wa wakati huo Gerd Mettjes kwa kutia saini. Baadaye, makusanyiko kutoka kwa Karl Braun yalihamishiwa kwenye Jumba la Makumbusho (Museumsverein Stade e.V.) kwa ajili ya utunzaji.

chanzo: Museen Stade, Vereinbarung Leihgabe "Brauns'sche Kolonialsammlung"
Mtu
Mahali
  • Stade
Scientific use:
Wakati
2023-06-14
Maelezo
I: mzee [Anonym] nina picha nyingine hapa imesajiliwa kwa namba 2018_18301_001, hebu angalia unaweza ukatambua hiki ni kitu gani R: hiki ni kitu cha kutolea moto I: kinaitwaje R: kwa kipare kinaitwa 'linyindi', hii kuna mti maalum na mti unaitwa 'mvumo', lakini kuna mti mwingine wa pili ambao ndio unatumika hivyo 'mkonde', iko hiyo miti, unapata uliyokauka ndio unachukua unafanya hivi unatengeneza kitu cha duara unapikicha mpaka unaoa moshi moto unatoka, lakini kuna mti unaitwa 'mzumba nkhozo wautei', huo mti ndio unaochukua…wenyewe umekaa kama kamba hivi, ni wingi sana hata huku tunauona, sasa unachukua yale yaliokauka ndio ukiyafikicha hivi unapata ule unga wake unatumbukiza hapa, ukifanya hivi unalipuka moto haraka sana I: kipare umesema inaitwa R: 'lunyindi' I: na kisambaa R: 'unyindi', yani una geuka geuka hapo hapo I: na ni makabila gani hasa walikuwa wakitumia lunyindi R: ni wasambaa, wapare, wambugu na makabila mengine wasafwa, wangoni kwa sababu kule walikuwa wapo wengi I: wasafwa wanapatikana mkoa gani R: wasafwa wanapatikana mkoa wa mara, tarime bara huko I: na wangoni R: wangoni ni songea I: kwa hiyo ilikuwa ni maalum kwa ajili ya kuwashia moto R: porini mkienda ndio kibiriti I: na mti mwingine ambao ulikuwa unaendana sambamba R: miti ninayoijua ni hiyo miwili, 'mvumo' na huo 'mkonde', I: na waliokuwa wanatumia lunyindi ni wa jinsia gani na umri gani hasa R: hii hasa zaidi ilikuwa inatumiwa na wazee wanaoenda kuwinda, na wazee wanaoenda shambani hawana haja ya kubeba moto wanabeba hii, au ametengeneza kabanda kake vinakaa huko, ndio ilikuwa inatumiwa na watu wa namna hiyo, lakini baada ya tuseme wazee kuzeeka sana wakatumia vijana sasa wanapoenda kuwinda wanabeba hii, au wanaenda kuchonga huko porini, yani unaweza kuchonga halafu ukafanya ukapata moto I: unachoma kwa mti ulio kauka au mbichi R: mti uliokauka, uliokauka tena umepewa jina 'khunge', yani umekauka ni wa muda mrefu sana, lakini kwa kipare wanasema 'ikulunge' I: na ni lazima uwe na mti mwingne ndio upikiche upate moto R: ee I: na kulikuwa kina umuhimu gani hasa kwa tamaduni hizo za watu uliowataja R: ni umuhimu wa kuepuka kununua vibiriti kutoka dukani wote: wanacheka I: kulikuwa kuna vibiriti kipindi hicho R: ee vibiriti vinaitwa vya 'nyota' I: ni miaka gani hiyo R: ni miaka ya 61,62 I: kwa sasa lunyindi inatengenezwa R: labda mtu anayependa kama hivi nyinyi mmependa labda mmekumbuka labda mkaona niwarithishe, maana wamesema ‘tuhifathi tuwarithishe’, tulirithishwa na mababu na sisi tuwarithishe, labda mimi niseme nina wajukuu na watoto niwafundishe lakini hawataki, kazi za namna hii hawataki hizi kazi I: wanapenda nini sana R: kununua vibiriti vya gesi... wote: wanacheka I: mzee [Anonym] lunyindi kama hiyo ikiletwa kwenye mazingira yetu ya sasa, unaweza ukainunua shilingi ngapi R: labda elfu 5, kwa sababu mali ghafi zake sio sana kama vile vingine nilivyowaelezea

chanzo: Amani-Stade Proejct / Amani Field Research 2023, Interview No. 19
mwandishi: I: Mohamed Seif, R. Anonymous
Mtu
  • National Institute for Medical Research (NIMR) (Mteja)
  • unknown actor (wissenschaftlicheR BearbeiterIn)
Mahali
  • Amani
Asili ya data ya kitu
Museen Stade
Leseni
Creative Commons Namensnennung, nicht kommerziell, keine Bearbeitung 4.0jifunze zaidi
Imepitishwa katika lango imewashwa
2025-12-04T15:01:14+01:00

Rekodi zetu za takwimu zinafanyiwa maboresho kila mara. Tafadhali wasiliana nasi ikiwa una maswali au maoni au ikiwa unahitaji taarifa zaidi au nyingine zinazohusu mali hii. Taarifa juu ya ulinzi wa takwimu.
Rudi kwenye utafutaji