Wakati
1908-08-23
Maelezo
"Jumapili 23. Mwezi wa nane 1908 [ime pigwa mstari] nimesafisha picha zangu – Leo nimepata sketi ya mwanamke inayoendana na suruali inayoelezwa u. 36 imetengenezwa na kitambaa cha kawaida cheupe [mchoro] shingoni mkononi na kwa chini kumewekwa kitambaa kilichokunjwakunjwa Kifuani juu chini, shingoni na mgongoni kwa juu [u. 57] kuna mapambo ya nyuzi za njano na nyeusi zilizowekwa na washonaji Waswahili kwa kutumia cherehani. [michoro makini miwili ya mapambo yakiwa na maelezo ] utepe kifuani urefu 31,5 cm, upana 5,5 cm / utepe shingoni upana 4,5 cm / mapambo ya mgongoni ni nyota ya kawaida mistari myeusi kwa nje mistari ya manjano kwa ndani. nimeilipia 1 rp. 5. Tena nikapata suruali ya mwanamke kama nilivyoionesha u 36 ila na rangi tofauti u. 36: Sikuwa na rangi stahiki rangi ya machungwa yangu ingepaswa kuwa pinki nyote nyeusi zimeshonwa kwa juu. Kitu chenyewe kimeunganishwa na mistari mingi. Nimelipa 1 rp. 25. Jioni nyumbani kwa Prof. Vosseler mkusanyiko: [u.58] Prof. Zimmermann & mke wake, Lommel, Prof Vosseler, Raab, Daktari rasmi Dr England na mimi." [Utafsiri]
1,25 Rupien
chanzo: Museum der Kulturen Basel, VI 56197, 52 (57)
mwandishi: Karl Braun
Mtu
Mahali