Hinweis: Um die korrekte Darstellung der Seite zu erhalten, müssen Sie beim Drucken die Hintergrundgrafiken erlauben.
Slider Bild - CC BY-NC-ND 4.0
1/1

Kengele kwenye kamba ya ngozi

Sammlung Braun
r 2018 / 18204
Taasisi inayotoa
Museen Stade
Eneo la Mkusanyiko
Sammlung Braun
Nambari ya uvumbuzi
r 2018 / 18204
Kichwa
Kengele kwenye kamba ya ngozi
Vipimo
Urefu: 19cm
Nyenzo
Ngozi,
Chuma,
Ngozi,
Chuma
Kiungo cha dondoo
https://www.amani-stade.gbv.de/item/sw_ms_537bf6d5-4e73-42ae-9be0-eaa79f6ea479
nakala kwenye ubao wa kunakili
Kikundi cha kitu / kitu cha mtu binafsi
Kitu cha mtu binafsi
Uainishaji
Vyombo vya muziki  
Uzalishaji
Wakati
mpaka 1906-04-10
Mtu
  • Person (Mtengenezaji)
Mahali
  • Tansania
Ethnolojia
  • Massai  
Kununua / Uuzaji
Wakati
1906-04-10
Maelezo
„Jumanne 10. Mwezi wa nne1906. [imepigwa mstari] kwa muda wa siku kadhaa nikapokea vitu vya kimila: mapambo ya masikioni ya Masai. Hutengenezwa kwa udongo na kupakwa udongo mwekundu. Udongo huo umechanganywa na ulanga vitu vyanuka vibaya mno . Udongo umewekewa shanga za buluu. Nywele hutumika kama manyamunyamu. 1 = Hella 25 [mchoro] kengele zinazovaliwa wakati wa kucheza ngoma [ngoma] zaidi ya 50 kwenye utepe wa manyoya. Zimetengenezwa kwa mkono kwa kupiga nyundo karatasi za vyuma zenye umbo wa mduara.kwa kengele 50 nikalipa 3 Rup. 75. [michoro makini miwili]" [Utafsiri]

chanzo: Museum der Kulturen Basel, VI 56197, 46 (115)
mwandishi: Karl Braun
Mtu
  • Mtu, haijulikani (Mchuuzi)
  • Braun, Karl (* 1870 † 1935) (Mnunuzi)
    GND Explorer
Mahali
  • Amani
Malipo
Wakati
1906-04-10
Maelezo
"70. Kengele yenye nyuzi za ngozi zinazotengenezwa zikiwa vipande 20 au zaidi huzungushwa mwilini wakati wa kucheza kila kengele hamsini = 3 Rp. 75 zote zimetengenezwa kwa mikono. / TB 46,155 [mchoro] mstari ulioinuka" [Utafsiri]"

chanzo: Museen Stade. r 2018 / 18566
mwandishi: Karl Braun
Mtu
Nambari za hesabu za zamani
  • 70
Urithi
Wakati
1934-07-17
Maelezo
Mnamo mwaka 1934, aliyekuwa mkurugenzi wa Taasisi ya Biolojia ya Kilimo na Misitu (Biologische Reichsanstalt für Land- und Forstwirtschaft) Karl Braun (1870–1935) alitoa kile kinachoitwa “Kolonialsammlung Braun” (Makusanyo ya Mkoloni Braun) kwa Jiji la Hanseatic la Stade, au tuseme aliyekuwa mwakilishi wake, meya wa wakati huo Hans Arthur Meyer (1884–1961). Tazama faili „Uhamisho wa makusanyo ya kikoloni kutoka kwa diwani mkuu wa serikali Profesa Dk. Karl Braun huko katika Jiji la Stade” („Überlassung einer Kolonialsammlung vom Oberregierungsrat Professor Dr. Karl Braun in Stade an die Stadt Stade") katika Jimbo la Saxony ya Chini Hifadhi ya Nyalaka ya Stade (Niedersächsischen Landesarchiv Standort Stade).

chanzo: Niedersächsisches Landesarchiv Standort Stade, Dep. 10 Nr. 03025
Mtu
  • Braun, Karl (* 1870 † 1935) (Mfadhili)
    GND Explorer
  • Hansestadt Stade (Mpokeaji)
  • Hans Arthur Meyer (1884 - 1961) (Mpokeaji)
Mahali
  • Stade
Mkopo
Wakati
1997-02-17
Maelezo
Mnamo mwaka 1997, aliyekuwa mtunza kumbukumbu wa jiji kwa wakati huo Jürgen Bohmbach anahitimisha makubaliano ya makabidhiano kwa mkopo wa kudumu katika Jumba la Makumbusho (Museumsverein Stade e.V.) chini ya aliyekuwa mkurugenzi wa wakati huo Gerd Mettjes kwa kutia saini. Baadaye, makusanyiko kutoka kwa Karl Braun yalihamishiwa kwenye Jumba la Makumbusho (Museumsverein Stade e.V.) kwa ajili ya utunzaji.

chanzo: Museen Stade, Vereinbarung Leihgabe "Brauns'sche Kolonialsammlung"
Mtu
  • Hansestadt Stade (Mkopeshaji)
  • Museum Schwedenspeicher (Mkopaji)
    GND Explorer
  • Bohmbach, Jürgen (* 1944) (Mkopeshaji)
    GND Explorer
  • Gerd Mettjes (Mkopaji)
Mahali
  • Stade
Scientific use:
Wakati
2023-09-15
Maelezo
I: Sawa nina picha nyingine hapa ambayo imesajiliwa kwa namba 2018_18204_1 mzee […] uliitambua hii vizuri hebu tuambie hiyo kwa kimasai inaitwaje? R1: Hii inaitwa ondwala engerei I: Kazi yake hasa ilikuwa ni nini mzee […]? R1: Hii kama nilivyokuambia mwanzo kwamba hii walikuwa wanafungiwa watoto wadogo ili itakapotembea sehemu kando ya watu, watu waweze kusikia yupo wapi maana watu walikuwa wanaishi porini yani huwezi ukakuta maboma ya kakaa kama hapa kwa pamoja unakuta boma moja hapa boma lingine unalikuta Lunguza na nyingine ukaikuta Kisima kwahiyo watu walikuwa wanaishi porini wakatumia hiki alafu kitu kingine kijana alikuwa akiua simba kuna fahari ya kijana wa kimasai katika jamii kuua simba sasa anacheza kwa kutumia hizi kengele anavalishwa hapa anafungwa hapa au hapa mguuni basi hapo sasa na huwezi ukamkuta ambaye hajavishwa labda hayuko kwenye sherehe ya kumuua simba hapana hii ilikuwa kazi yake ndiyo hiyo I: Na hao waliokuwa wanamuua simba walikuwa wana umri gani mzee […] hebu tuambie hapo? R1: Ni morani peke yao wale tuliyokuambia ni layoni hata aue simba hawezi akavalishwa hii na hata kama ni mzee akiua hata aue simba hawezi akavalishwa ni morani tu peke yao ndiyo wanavalishwa I: Na hawa watoto walikuwa ni watoto wa umri gani ambao walikuwa wanavalishwa hizo namba moja hebu tuambie? R1: Anapoanza kutembea miaka kuanzia mwaka mmoja na kuendelea mpaka aonekane amekuwa na akili timamu ya kujua anatakiwa arudi nyumbani ndiyo ananyang’anywa anapewa mdogo mwingine I: Kwahiyo walikuwa wanavalishwa watoto wa kike na wakiume? R1: Wote I: Na hivi sasa bado zinatumika hizi kengele? R1: Hapana I: Odwala engerei? R1: Eeeh ondwala engerei ni kengele ya mtoto I: Sasa hivi hazitumiki? R1: Sasa hivi hazipo hazitumiki R2: Lakini juzi juzi nilikuwa na moja sijui imepotelea wapi I: Ulimvalisha mtoto? R1: Eeeh kwa kweli sasa hivi hata ukimvalisha mtoto ni fahari sana kwasababu watu wengi sasa hivi hawavalishi na watamshangaa I: Mzee [anonymous] na wewe ulivaa hiyo miaka hiyo? R2: Eeeeh lazima sisi wote tulivaa kwasababu mimi kwenye kumbukumbu mimi nimeugua tu polio lakini nilikuwa natembea na nilivishwa pia hii I: Na waliokuwa wanatengeneza hizo kengele ni watu wa jinsia gani? R2: Kwa kweli ni wanaume I: Wa umri gani hasa? R2: Umri wowote tu wakuanzia miaka 18 na kuendelea nani ufundi tu anaweza kuwa na miaka midogo lakini akawa anaweza akatengeneza I: Na walikuwa wanatumia kitu gani kutengenezea hiyo? R1: Hii walikuwa wanatumia tu mabati, vyuma, eeeh yani ni vyuma haswa ndiyo walikuwa wanatumia katika kutengeneza I: Na humo ndani walikuwa wanaweka vitu gani ili ipige kelele? R1: Walikuwa wanaweka gololi ya chuma I: Na huo mkanda? R1: Mkanda niwa ngozi ya ng’ombe ndiyo ya kufungia I: Ndiyo ya kufungia? R1: Eeeh I: Sawasawa na hizo mlikuwa mnanunua au zilikuwa zinatengenezwa? R1: Zinanunuliwa hizi mpaka ununue I: Kama hiyo sasa hivi inaweza ikauzwa shilingi ngapi? R1: Hiyo mpaka elfu kumi sahivi au elfu kumi na kulingana na uhitaji wako anaweza akakuuzia hata zaidi ya elfu kumi sasa hivi ikitokea hapo itauzwa elfu ishirini maana watu watanunua kwa wingi

chanzo: Amani-Stade Project / Massai Field Research 2023 / Interview No. 04
mwandishi: I: Mohamed Seif, R1: Anonymous
Mtu
  • National Institute for Medical Research (NIMR) (Mteja)
  • unknown actor (wissenschaftlicheR BearbeiterIn)
Mahali
  • Lunguza
Scientific use:
Wakati
2023-10-03
Maelezo
I: Ni kweli niliishika mimi ni nzito sana sawa nina picha nyingine hapa ambayo imesajiliwa kwa namba 2018_18204_1 kuna mmoja wenu aliitambua hii ehe namba mbili hebu tuambie kwa jinsi ulivoiona ukaielewa? R2: Unajua watu wa zamani wanakula nyama porini I: Kwanza kabla hujaendelea hiyo kwa kimasai inaitwaje? R2: Hii hapa inaitwa olitwala na hii hapa ni mkanda ndiyo wanaweka milima mizima zamani wanaweka kwenye milima tuseme ndiyo wameiba ng’ombe sehemu fulani wanashika hizi kamba hivi ukishika hivi watakuja watu kumuokoa wanasikia ambae yupo Luzilwa anasikia ujue ameiba ng’ombe watu wote ndiyo wanaamka lakini wale wanaoenda kukamata ng’ombe kurudisha anaweka na kengele zao mguuni na wapo na pembe nyingine basi atakuwa anasikia kama kengele fulani hivi mbali kunavitu vingine vinalia vuu, vuuu, vuuu pembe yani walikuwa wanafuraha kubwa sana hata kwenda kuua samba huko porini wanaweka hapa wanakuja hiyo ni vitu vya kimila na desturi za zamani maana hivyo vitu vipo sana katika jamii yetu hii ya kimasai vipo sana I: Anafunga kwenye paja? R2: Eeeh kwenye paja I: Kwahiyo kazi yake kubwa ni kama ishara? R2: Ni kama ishara I: Kupeana tarifa? R2: Eeeeh I: Kwahiyo ilikuwa ni kwa ajili ya kwenda kuua simba na kufuatilia mifugo na kazi gani nyingine ilikuwa inatumika? R2: Hata kuiba ng’ombe I: Waliokuwa wanaenda kuiba ndiyo wanavaa hivyo? R2: Aaaa hao walioiba hawavai lakini tuseme mtu aliyekuja kutoka Ngorongoro kusema anakuja kuiba ng’ombe ya Longido kuja kuiba ng’ombe ya Longido kwahiyo watu waliofuata Longido ndiyo wanaitana kwa kutumia hii kengele lakini anapofuata ng’ombe akienda kumkuta ng’ombe anamkamata anaweka kengele zao mguuni watakuwa wazee wanavyokaa nyumbani atasema hawa ndiyo wameshika ng’ombe maana wanasikia kengele zao zile eeh wamerudisha ng’ombe kwenda kutafuta simba ndiyo wanawawekea kengele hawa wakina mama na wazee kwamba leo ndiyo wameua simba hawa ndiyo simu kama simu ambazo zilikuwa zinatumika kipindi hicho cha zamani I: Kwahiyo ambao hawajaua simba walikuwa hawatakiwi? R2: Watakuja tu kumuona lakini atakuja kimya kimya maana hana furaha maana hiyo niya furaha kabisa R1: Sasa hii ni ishara ya furaha yani ipo mara mbili maana unajua kwenye wizi kuna kengenle mara mbili kuna ile ya mdomoni puuu kuna mlio fulani pekee wa kupiga na pia hii iko hivo hivo lakini hii inaweza ikaingia mara mbili kwa mfano kwenye hiyo furaha tuseme kama ng’ombe wakimpata wakishaua yule simba na kurudi nyumbani vijana hawajajua wanaweza wakafurahi lakini kama watu wamejua hawa furahi yani hawataweka kwenye paja maana ni kimya kimya mpaka tu maana watu wameliwa na simba ameuliwa lakini simba amemkwaruza mtu awe ana damu au amekufa au amemjeruhi tu hii haivaliwi hii tunavalisha wale watoto wadogo pale akitaka kuanza kunyanyuka yani mtoto mdogo kitu ambacho sasa zile ambazo viatu vyenu mnavyonunulia watoto wakikataa kutembea sasa wewe unakuwa unamvalisha kinavyofanya tii, tii, tii inakuwa inamsaidia mtoto kuweza kunyanyuka na kuanza kutembea tembea kuna mabobo yao yalikuwa yanafungwa yawasaidie wale watoto kutembea kwa urahisi kama watakuwa wanasua sua katika kutembea kwahiyo kihalisia tunaona ni kama mkanda tu ule wa kufungia mdomo wa kengele I: Na ilikuwa hiyo kengele inatengenezwa kwa kutumia nini na nini namba moja hebu tuambie hapo? R1: Kengele hii ni ngozi lakini hizi huwa wamasai wananunua tu kutoka kwenye zile makereketwa au kwenye wale watu wa machuma chuma sasa wanaweka gololi ndani ndiyo zinatoa kelele I: Kwahiyo kwa watoto walikuwa wanavaa watoto wa kike na wakiume wote wanavaa katika jamii? R1: Mtoto mdogo ambaye anakataa kutembea anavalishwa ili imsaidie aamke aanze kutembea inakuwa ni hivyo I: Inaitwa olitwala ndiyo kengele hiyo? R2: Eeeeeh

chanzo: Amani-Stade Project / Massai Field Research 2023 / Interview No. 06
mwandishi: I: Mohamed Seif, R1, 2: Anonymous
Mtu
  • National Institute for Medical Research (NIMR) (Mteja)
  • unknown actor (wissenschaftlicheR BearbeiterIn)
Mahali
  • Longido District
Mwandishi: Karl Braun, Nukuu/Angalizo: Museen Stade, r 2018 / 18566 [70]jifunze zaidi
Mwandishi: Karl Braun, Tarehe ya kutengenezwa: 1906-04-10, Nukuu/Angalizo: Museum der Kulturen Basel, VI 56197, 46 (115)jifunze zaidi

Rejeo la ndani la kitu

Kengele kwenye kamba ya ngozi

Kengele kwenye kamba ya ngozi

r 2018 / 18261 a
Rejeo la ndani la kitu
Kitu kinacholingana
Vipande viwili vya vito vya masikio

Vipande viwili vya vito vya masikio

r 2018 / 18238
Rejeo la ndani la kitu
Kuhusiana na
Asili ya data ya kitu
Museen Stade
Leseni
Creative Commons Namensnennung, nicht kommerziell, keine Bearbeitung 4.0jifunze zaidi
Imepitishwa katika lango imewashwa
2025-12-04T15:17:15+01:00

Rekodi zetu za takwimu zinafanyiwa maboresho kila mara. Tafadhali wasiliana nasi ikiwa una maswali au maoni au ikiwa unahitaji taarifa zaidi au nyingine zinazohusu mali hii. Taarifa juu ya ulinzi wa takwimu.
Rudi kwenye utafutaji