Hinweis: Um die korrekte Darstellung der Seite zu erhalten, müssen Sie beim Drucken die Hintergrundgrafiken erlauben.
Slider Bild - CC BY-NC-ND 4.0
1/1

Vazi la kichwa lenye manyoya na shanga

Sammlung Braun
r 2018 / 18527
Taasisi inayotoa
Museen Stade
Eneo la Mkusanyiko
Sammlung Braun
Nambari ya uvumbuzi
r 2018 / 18527
Kichwa
Vazi la kichwa lenye manyoya na shanga
Vipimo
Urefu: 55cm, Upana: 30cm
Nyenzo
Manyoya,
Kioo shanga
Kiungo cha dondoo
https://www.amani-stade.gbv.de/item/sw_ms_734dce92-f7b3-4496-87e9-18303bbf42b7
nakala kwenye ubao wa kunakili
Kikundi cha kitu / kitu cha mtu binafsi
Kitu cha mtu binafsi
Uainishaji
vito vya kikabila  
Uzalishaji
Wakati
mpaka 1906-05-26
Mtu
  • Person (Mtengenezaji)
Mahali
  • Tansania
Kununua / Uuzaji
Wakati
1906-05-26
Maelezo
"„Jumamosi 26. Mwezi wa tano 1906 [imepigwa mstari] [njiani na Dr [7] Lenz kutoka kwenye meli ya mvuke bandarini Dar es Salaam hadi ""Meiller-Shamba"" tukaendelea hadi ""Waldschlöschen"" [8], kupitia makazi ya wazawa, wakati wa kurudi kupitia sokoni kuelekea meli ya mvuke] [...] Nimekwenda melini na kweli kulikuwa an ujumbe ""urudi haraka mavuno ya karanga yamemalizika."" nifanyaje kabla ya tarehe 7. Mwezi wa sita hakuna meli ya mvuke. Nikaenda makao makuu ya utawala nikaagizwa nisafiri Mikindani nikaangalie mengi yawezekanavyo. Nikifurahiahatimaye kuwa na mwelekeo nikatembea kurudi. – Barbarani nikakutana na mwanamume aliyekuwa anauza vitu kadhaa [u. 15].: Meli kubwa iliyochongwa na kifuu (?) imetengenezwa na fundi bei yake ilikuwa Rupie 2 halafu mitumbwi miwili midogo imetengenezwa kutoka nusu ya tunda ya baobab kushoto na kulia na viambatanisho vinavyoelea majini dann [mchoro wa ] boti hizo za wazawa huitwa ""Ngarawa"" [orofdha. na. Karl Braun 74]. Pia vinyago viwili kwa ajili ya Pepo Goma, kila moja kimewekewa kauri (kila moja = 1 Rupie) [mchoro] [Orofdha. na. Karl Braun 75], pambo kubwa la kichwa lenye manyoya na shanga za kioo = 6 Rup. [mchoro] [orofdha. na. Karl Braun 76] & bangili tatu kwamatumizi yale yale = 5 Rup [Orofdha. na. Karl Braun 77]. Nimetapeliwa na hivi vitu kwa maneno ya mkazi wa hapa aliyekuwepo melini akisema vitu hivyo vyanunuliwa kwa Rupie 1 ila sikuamini jioni melini"" [Utafsiri] [7] daktari au mwenye phd [8] kasri ndogo msituni"

chanzo: Museum der Kulturen Basel, VI 56197, 47 (15)
mwandishi: Karl Braun
Mtu
  • Mtu, haijulikani (Mchuuzi)
  • Braun, Karl (* 1870 † 1935) (Mnunuzi)
    GND Explorer
Mahali
  • Dar es Salaam
Malipo
Wakati
kutoka 1906-05-26
Maelezo
"76. Mapambo ya kichwani yenye manyoya ya mbuni kwa ajili ya kucheza ngoma. Ukanda wa kichwa wenye mapambo ya shanga / Daresalam 26. mwezi wa tano 1906 = 6 Rp (ghali mno!) / TB 47,15. [mchoro]" [Utafsiri]

chanzo: Museen Stade, r 2018 / 18566
mwandishi: Karl Braun
Mtu
Nambari za hesabu za zamani
  • 76
Urithi
Wakati
1934-07-17
Maelezo
Mnamo mwaka 1934, aliyekuwa mkurugenzi wa Taasisi ya Biolojia ya Kilimo na Misitu (Biologische Reichsanstalt für Land- und Forstwirtschaft) Karl Braun (1870–1935) alitoa kile kinachoitwa “Kolonialsammlung Braun” (Makusanyo ya Mkoloni Braun) kwa Jiji la Hanseatic la Stade, au tuseme aliyekuwa mwakilishi wake, meya wa wakati huo Hans Arthur Meyer (1884–1961). Tazama faili „Uhamisho wa makusanyo ya kikoloni kutoka kwa diwani mkuu wa serikali Profesa Dk. Karl Braun huko katika Jiji la Stade” („Überlassung einer Kolonialsammlung vom Oberregierungsrat Professor Dr. Karl Braun in Stade an die Stadt Stade") katika Jimbo la Saxony ya Chini Hifadhi ya Nyalaka ya Stade (Niedersächsischen Landesarchiv Standort Stade).

chanzo: Niedersächsisches Landesarchiv Standort Stade, Dep. 10 Nr. 03025
Mtu
  • Braun, Karl (* 1870 † 1935) (Mfadhili)
    GND Explorer
  • Hansestadt Stade (Mpokeaji)
  • Hans Arthur Meyer (1884 - 1961) (Mpokeaji)
Mahali
  • Stade
Mkopo
Wakati
1997-02-17
Maelezo
Mnamo mwaka 1997, aliyekuwa mtunza kumbukumbu wa jiji kwa wakati huo Jürgen Bohmbach anahitimisha makubaliano ya makabidhiano kwa mkopo wa kudumu katika Jumba la Makumbusho (Museumsverein Stade e.V.) chini ya aliyekuwa mkurugenzi wa wakati huo Gerd Mettjes kwa kutia saini. Baadaye, makusanyiko kutoka kwa Karl Braun yalihamishiwa kwenye Jumba la Makumbusho (Museumsverein Stade e.V.) kwa ajili ya utunzaji.

chanzo: Museen Stade, Vereinbarung Leihgabe "Brauns'sche Kolonialsammlung"
Mtu
  • Hansestadt Stade (Mkopeshaji)
  • Museum Schwedenspeicher (Mkopaji)
    GND Explorer
  • Bohmbach, Jürgen (* 1944) (Mkopeshaji)
    GND Explorer
  • Gerd Mettjes (Mkopaji)
Mahali
  • Stade
Scientific use:
Wakati
2023-06-14
Maelezo
I: sawa, asante tumepata maelezo ya kibobo na stori nyingi ndani yake, tuna picha nyingine hapa imesajiliwa kwa namba 2018_18527_1, hebu angalia unaweza ukatambua ni kitu gani hiki R: hiki kulikuwa na ngoma zamani zinachezwa na mabinti kama hivi, kwa kipare tunasema 'mueka', anachezwa ngoma, kwa kisambaa wana namna zao wanasema 'dawau unyago', yani anapitishwa unyago, sasa watoto wa jumbeau aliyefanya vizuri sana alikuwa anavalishwa kitu kaa hiki I: inaitwaje hiyo R: hii ni kofia lakini ilikuwa inaitwa 'ivungah', hicho ni kipare, 'adokwa ivungah’, yani huyo ameshinda ndio anavalishwa ambavyo wameboresha sasa hivi wanasema amevalishwa taji, kisambaa wanasema tu kofia au 'azaikwa taji', sasa hivi vinakuwa vimelala humu, basi akiletwa kule anatembea namna hii wanapiga vigelegele, hivi vigelegele wanaita 'ngagha' kwa kipare, wazaramo wanasema 'nkheghe' akipigiwa hivyo kwanza ameshinda vitu vyote I: kwa hiyo ni makabila gani walikuwa wanatumia kofia kama hizo R: wapare, lakini pia hata wambugu, hata wasambaa walikuwa wakitumia kama hivi wakifanya hayo matambiko, sasa hivi vilikuwa vinatengenezwa halafu vinauzwa... I: vilikuwa vinauzwa zaidi mikoa gani R: ni huko lushoto ninakokuambia, kule same, gonja maore kuna masoko kule, kwa mfano kuna soko linaitwa ‘kwekanga’, halafu kuna soko linaitwa ‘baga’ na ‘kwemakame’, ndio masoko ambayo yalikuwa vinauzwa vitu hivyo, na pale mazinde kuna soko lilikuwa linaitwa ‘mshangai’, I: mzee [anonymous] hao mabinti waliokuwa wanavalishwa hiyo, walikuwa ni mabinti wa kuanzia umri gani R: kuanzia miaka 18, 20ambao ndio hao wanachezwa hizo ngoma I: na kuchezwa walikuwa wanachezwa baada ya kuwekwa ndani R: ee I: ndani walikuwa wanawekwa kwa muda gani R: wiki au mwezi, inategemeana na nafasi ya yule mwenye mtoto I: na taji au kofia kama hilo bado inatumika kwa sasa R: hapana I: kwa nini unadhani haitumiki R: zile mila na tamaduni na wale waliokuwa wanazithamini wengi wamekufa na wengi hawakurithi I: na ili kofia hiyo itumike kuna kitu kingine ambacho kilikuwa kinapaswa kuwa sambamba anayevaa kofia hilo labda anatakiwa awe na kitu kingine cha kuendana na hiyo kofia R: ndio I: ni vitu gani R: mavazi, kunaandaliwa gauni ambalo linashonwa moja refu mpaka huku, lakini mtindo wake lilikuwa linaitwa 'mshono wa mwamvuli' yani ukitimiza hivyo anaambiwa 'ula ni mgothi', lakini ndani ya hivyo vitu ninavyokutajia vikikosekana na vipambopambo vingine havimo 'ni mgothi yani ula atekoloshe', yani hakutimiza, na wasambaa wanasema 'simtuja, ukimuona mtu wa mana mya atala ngoma a mwanae, itimize, nainosiabigo waa, osiemteme vikoja', maushanga makubwa yana punje kubwa na makoja mengine kokwa zake ni nene kama vile matunda damu, basi yale ndio yalikuwa yanatumika kwenye mila zinazoendana na hii I: na waliokuwa wanatengeneza haya mataji kwa ajili ya mabinti walikuwa ni wa jinsia gani na kuanzia umri gani R: ni wanaume, ila kwenye hayo ninayokuambia makoja, hayo yanatengenezwa na wanawake, kwa sababu inafikia hatua ni ya kuenda kumpima shingo wanapima wanawake wenyewe, mengine ni ya kuvaa kiunoni anaenda kupima mwanamke, lakini wale wa zamani zinaweza zikawa hamsini hapa akipiga mguu hivi zenyewe zinalia... wote: wanacheka I: mzee [anonymous] hebu tuambie ni vitu gani vilikuwa vinatumika kutengenezea hiyo taji R: kunatumika manyoya ya kuku, manyoya ya ndege na hizi kamba kamba hizi kuna miti mingine ilikuwa inachunwa porini kuletwa kuja kuunganishwa... I: ni miti gani R: kuna mti unaitwa 'ifyofyokoo',au 'minyambo' ndio inachunwa na inasukwa sukwa, yani hiyo miti yenyewe ukiichuna ukiianika kwenye jua inakuwa na rangi yake, ukiianikia ndani inakuwa na rangi kama nyeusi na nyingine zilikuwa zinachukuliwa ule mkia wa ng'ombe yale manyoya yake yanasukwa I: kwa hiyo kuna hizo kamba, kuna manyoya na kitu gani kingine? R: na hizo nywele za mkia wa ng'ombe I: na hivi vyeupe vyeupe ni nini R: hizi ndio hizo kamba ninazokuambia, zinaanikwa zinatofautishwa zinaboreshw kwenye kuziandaa, huku ni manyoya ya kuku, ya ndege na nini ndio vitu hivi vilivyojaziwa jaziwa, lakini hizi ni kamba ambazo zimeandaliwa kwa mfumo wa aina yake... I: naona kama kuna vitu vya duara duara R: hivi vya duara duara hapa ndani ndio hivyo tunavyosema ‘vikoja’ I: na kofia kama hii kwa wale wanaofahamu umuhimi wake, ingeletwa katika mazingira sasa hivi ingeweza kuuzwa shilingi ngapi R: hizi zilikuwa zina bei, kwa sasa hivi ninaweza nikakuambia elfu kumi au hata ishirini, hizi zilikuwa zina mzunguko mrefu sana I: na ilikuwa binti asipovaa hivyo hajakamilika R: ndio maana nikakumbia (...anaongea kilugha...) basi ni vitu kama hivyo I: lile jukumu la kununua hivi nani R: ni baba na ndio anayemuambia mama aende aandae hivyo anampa hela, lakini baba ndio mwenye maandalizi yote ya kuandaa, inaweza ikauzwa ng'ombe ikaenda tafuta vitu hivi na vinginevyo I: na ilikuwa ni heshima akivaa R: ee ni heshima, huyo mtoto hata ukienda kuposa, ukifanikiwa ukikaa na wenzako wanasema 'tha uyu ne mgothe avae aingia ao avae hekoloke' yani; huyu mwanaume naye ni mzima maana amekubalika pale', yani hapo huwezi kuenda ovyo ovyo, lakini siku hizi binti akionekana 'oyaa, vipi wewe pita naye huyo mwanangu' wote: wanacheka

chanzo: Amani-Stade Project / Amani Field Research 2023, Interview No. 19
mwandishi: I: Mohamed Seif, R: Anonymous
Mtu
  • National Institute for Medical Research (NIMR) (Mteja)
  • unknown actor (wissenschaftlicheR BearbeiterIn)
Mahali
  • Amani
Scientific use:
Wakati
2023-10-04
Maelezo
I: Na tutaanza na picha yetu ya kwanza ambayo imesajiliwa kwa namba 2018_18527_1 ni nani aliitambua hii picha namba tatu uliitambua hii picha unaweza kutuambia ni kitu gani hicho hiki kinitwaje? R3: Hiki kinaitwa orimoronyi I: Orimoronyi maana yake ni nini? : R3: Hiyo walikuwa wanavaa zamani wamasai lakini hiyo orimoronyi walikuwa wanavaa morani mimi natambua kwa hivyo I: Walikuwa wanavaa morani? R3: Eeeeh tena ni morani wakali waliovaa siyo morani wakienyeji tu ni morani wakali ambao wapo kwenye jamii I: Una maana gani ukisema morani kali? R3: Kama anaenda kutafuta simba zamani lakini anaua peke yake huyo samba bila uwoga wowote lakini kama ng’ombe atarudi na ng’ombe wengi kuliko wengine huyo sasa ndiyo morani mkali I: Kwahiyo ni yule shujaa? R3: Eeeeh I: Ilikuwa inatumikaje hiyo? R3: Hii ni aina ya ndege ambayo wakienda kwenye vita anashinda yule shujaa analetewa anashonewa na anavalishwa kichwani sasa hapo ndiyo itaonekana kwamba huyu inaonyesha utofauti wa shujaa na wale wengine na ilikuwa ni aina ya ndege ambao walikuwa wanang’ata pia watu kwahiyo historia ni kwamba walipoenda vitani shujaa aliposhinda ndiyo wakamkuta yule ndege akaua alafu akasema huyu ni ndege wangu sasa historia ikaanzia hapohapo kwamba yoyote atakaye kuwa anavaa hivyo ni shujaa kwasababu kipindi ameenda kwenye vita amepambana na adui na kafanikiwa kushinda sasa anavokuwa anarudi anavishwa kofia hiyo ya kuwa shujaa I: Huyo ndege alikuwa anaitwaje? R3: Huyu ndege anaitwa olimotonyi I: Kwahiyo alikuwa anapiga watu huyo ndege? R3: Eeeeh I: Ni mkubwa? R3: Ni mkubwa sana I: Kama mbuni au ni zaidi ya mbuni? R3: Kama mbuni I: Kwahiyo hiyo ilikuwa ni kwa ajili ya kuvalishwa mashujaa tu ambao wameua Simba au yule ambaye ameleta ngombe wengi? R3: Eeeeh I: Wakati anavalishwa kuna sherehe yoyote inafanyika au? R3: Kama kuna sherehe yoyote anavaa I: Walikuwa wanafanya nini mpaka kumvalisha hiyo? R3: Alivokuwa anavalishwa walikuwa wanatangaziwa ilikuwa inajulikana kwamba ni yule morani wa motonyi kwamba yani itakuwa kama sifa kwake kuvalishwa kwasababu ndiye shujaa kwenye jamii I: Nataka kufahamu utaratibu uliokuwa unatumika kumvalisha hiyo kofia namba namba mbili hebu tuambie? R2: Kipindi cha nyuma watu walikua wanapitiana kwenda kutafuta ng’ombe alafu wanaiba wale ng’ombe wanaleta yule shujaa ambaye ameua watu wengi anakuja anavalishwa alafu kuna ubarikio anabarikiwa alafu anavalishwa alafu wanaletwa wale ng’ombe nyumbani na pia wanavoenda kuwapiga wale watu na kuchukua ile mifugo sasa wakiwaua wale watu sasa wale ndege wanashuka kwenye ile mizoga ya wale watu na wanakula akija yule morani anaua yule ndege mkubwa alafu akishamaliza kuua analeta nyumbani anawapa wa mama alafu wa mama wanashona alafu wanamvalisha kijana ambaye amekuwa shujaa kwa kuua watu wengi na kuiba ng’ombe wengi I: Nataka kujua sasa utaratibu wa kumvalisha hiyo kofia ni kitu gani kinafanyika mpaka kuvalishwa akileta tu anavalishwa au kuna kitu kinafanyika namba moja hebu tuambie hapo inakuwaje? R1: Hii kitu inaitwa olimotonyi kuna namna ya kuvalisha huyu kijana kwasababu yeye mwenyewe ameenda sehemu na ameenda kuua hiyo olimotonyi na amerudisha na amekuja kwenye boma itakuja kuwa sikukuu kubwa ya kuja kusifu huyu kijana ambaye ameleta sifa kwenye boma kwenye mji wa kimasai ameua simba na amekuja kuua hiyo olimotonyi na amerudisha ng’ombe yao wamasai wamesema kitu ambacho wanamfanyia huyu kijana ni kumshonea hiyo olimotonyi baada ya kuja analeta sikukuu kubwa kwa morani anaimba anakuja kwenye boma anavalisha huyu kijana olimotonyi ili sifa yake ionyeshe kwamba alienda kufanya kitu cha maana eeh I: Kwenye hiyo sikukuu na kuchinja labda? R1: Anachinja ng’ombe anachinja mbuzi zamani wanachinja ng’ombe kwasababu siyo masikini walikuwa na mifugo mingi sana siyo kama sasa hivi zamani walikuwa na ng’ombe wengi kwa hiyo walikuwa wanachinja ng’ombe I: Ng’ombe nyingi? R1: Eeeh anachinja dume nje anakuja kuleta nyama ya mama anakula na wa mama wanavaa nguo vizuri ambayo inaitwa orekelaa ambayo imetengenezwa kwa kutumia ngozi na anashonea na ushanga nawa mama wanavaa kitu kinaitwa mboroo ili amsubiri huyu kijana wake ambaye ameleta sifa kwenye mila yetu ya kimasai baadae wa mama wanakuja kuimba alafu wanamvalisha huyu kijana hiyo olimotonyi kwasababu amefanya la maana sana kwenye jamii kuiletea sifa boma I: Na kwasasa bado inafanyika hivyo kama ilivyokuwa inafanyika kipindi hicho namba moja hebu tuambie? R1: Haiwezekani kufanya baba kwasababu baba haendi sehemu ya ugomvi baba ni mtu ambaye anaenda kuzuia ugomvi kwa vijana lakini wa mama, wa baba, na vijana anakuja kuvalishwa kwasababu ya sifa aliyoileta lakini baba anakuja usiku huyu kijana ameleta sifa kwenye boma lakini haitaingia ugomvi I: Sasa hivi kijana akifanya tendo la ushujaa bado anavalishwa hii kofia namba moja hebu tuambie? R1: Kabisa anavalishwa sasa hivi morani kama ameenda kuua simba anaweka kitu kinaitwa mboroo anaweka hapa anaweka hapa anavaa nguo na anafunga mkanda hapa kitu kinaitwa engimeta anaweka mboroo sehemu za pande zote mbili kwasababu ameua nini simba wanaimba wanakuja wanafanya hivi wanaimba wanaimba wamama wanakuja kusimama kwenye boma kila mama anavaa mboroo anavalisha kijana hii kwasababu ni sifa kubwa sana katika jamii yetu hii ya kimasai I: Hiyo mboroo ndiyo nini? R1: Ushanga kama huu lakini anashona nyingi atavalisha mtu upande huu anavalisha pia upande huu anaweka hizi lomboi ili aonyeshe mtu mboroo ni kitu ya sifa sana kwa mtu ambaye amefanya kazi vizuri I: Kwahiyo anapovalishwa kijana huyo wa kimasai hii olimotonyi anavaa nini kitu kingine ni kofia tu anavalishwa au kuna kitu kingine anakuwa anavalishwa hiyo olimotonyi namba moja hebu tuambie? R1: Anavalishwa na mboroo ana mkanda ambao anaweka pia kitu kinaitwa endoroto unajua hiyo ni kidonge cha dawa analeta vitu ambavyo vipo porini anakuja kuweka maji kidogo anavalisha huyo kijana anaweka kila mahali ushawahi kuona pundamilia porini na morani anafanywa kama hivyo I: Anapakwa rangi rangi? R1: Anapakwa rangi, rangi na anavaa kitu kinaitwa odwala anafunga hapa anaimba, anaimba wanasimama wamama wawili au wanne wanasimama upande wa milango ya boma kila mama anashika endoroto huyo kijana akikimbia kuja hapa kusifu au kuimba wanamvalisha kwasababu ya sifa aliyoleta kwenye boma kuwa shujaa kwa kupambana na adui mpaka kumshinda adui hiyo ni sifa kubwa I: Kwahiyo hii ilikuwa ni kiashiria cha ushujaa kwenye jamii ya kimasai? R1: Eeeeh I: Kwahiyo waliokuwa wanatengeneza hizi ni kina nani? R1: Wa mama ndiyo wanashona lakini mtu anayeleta kutoka porini ni kijana I: Kijana analeta huyo ndege? R2&1: Eeeeh analeta anachinja hiyo olimotonyi analeta ngozi yake anakuja kuchanganya ngozi ya ng’ombe ambayo imekauka itashonwa hivi itawekwa kitu kama kofia na hiyo kofia ndiyo ataenda kuvalishwa I: Kwahiyo ni ngozi ya ng’ombe? R1: Eeeeh siunaona hizi huyu ameweka urembo lakini ni ngozi ya ng’ombe wameshona atavalishwa hivi atavaa kama kofia I: Anavalishwa kama kofia? R1: Eeeeh I: Na kwasasa hivi bado zinatengenezwa kama hizi? R1: Unaweza kutengeneza lakini sasa hivi mambo mengi sana yamekaa mbali na watu kwasababu unajua kila kitu sasa hivi imesema serikali haitoi kwahiyo watu wamekuwa waoga kwa vitu vyao wenyewe I: Kwahiyo waliokuwa wanawashonea hawa walikuwa ni kina mama kuanzia umri gani namba moja hebu tuambie? R1: Hata wazee kama sisi anaweza kushona anaweza akatafutwa mama mzee ambaye ni mtaalamu unajua kila kitu ni utaalamu hospitali wana mtaalamu ambaye anajua kutoa dawa kwenye boma kuna utaalamu ambao watu wanajua kushona vizuri kuna watu unajua wamekaa muda mrefu kama sisi wazee bila kushona kitu kama hicho wamasai watauliza ni nani ni mama nani anajua kushona olimotonyi wanasema wa mama wazee basi wanamwita njoo anashona kofia kama hii ili waje kumvalisha kijana na olimotonyi inateremka hivi ili afanye hivi akiwa anaimba eeeh I: Nani uzi gani ulikuwa ukitumika kushonea olimotonyi? R1: Zamani sisi anashonea na kitu kinaitwa endupati ambayo ni katani kuna katani mbili kuna katani ambayo ina madawa dawa kuna katani ambayo nimeona sehemu nyingi ya shule ipo kitu kinaitwa ndubai na ndiyo hii inashonea hata sasa hivi kitu kingine ameshona na endupati ni uzi ambao siyo uzi wa uswahilini niya ndubai ndiyo inatengeneza na mama anashona hiyo olimotonyi I: Namba tatu ulitaka kuongezea kitu R3: Hicho kitu kinaitwa enopini kwenye ngozi ya ng’ombe kuna kitu kidogo kama enopini inashonea kitu kama hii I: Ile nyama nyeupe ya kwenye ngozi ndiyo inatengenezwa alafu inashonea namba tatu hebu tuambie? R3: Eeeeeeh

chanzo: Amani-Stade Project / Massai Field Research 2023 / Interview No. 10
mwandishi: I: Mohamed Seif, R1-3: Anonymous
Mtu
  • National Institute for Medical Research (NIMR) (Mteja)
  • unknown actor (wissenschaftlicheR BearbeiterIn)
Mahali
  • Kimokouwa
Mwandishi: Karl Braun, Tarehe ya kutengenezwa: 1906-05-26, Nukuu/Angalizo: Museum der Kulturen Basel, VI 56197, 47 (14-16)jifunze zaidi
Mwandishi: Karl Braun, Nukuu/Angalizo: Museen Stade, r 2018 / 18566 (76)jifunze zaidi

Rejeo la ndani la kitu

Meli ndogo

Meli ndogo

r 2018 / 18324 b
Rejeo la ndani la kitu
Mazingira/Muktadha wa upataji/Upatikanaji
Meli ndogo

Meli ndogo

r 2018 / 18324 a
Rejeo la ndani la kitu
Mazingira/Muktadha wa upataji/Upatikanaji
Mask iliyofanywa kwa vipande vya wicker na shells za cowrie

Mask iliyofanywa kwa vipande vya wicker na shells za cowrie

r 2018 / 18491
Rejeo la ndani la kitu
Mazingira/Muktadha wa upataji/Upatikanaji
Tuft ya manyoya

Tuft ya manyoya

r 2018 / 18519
Rejeo la ndani la kitu
Kitu kinacholingana
Mask iliyotengenezwa kwa vipande vya kusuka na shells za cowrie

Mask iliyotengenezwa kwa vipande vya kusuka na shells za cowrie

r 2018 / 18522
Rejeo la ndani la kitu
Mazingira/Muktadha wa upataji/Upatikanaji
Sanduku la usafiri 2

Sanduku la usafiri 2

r 2018 / 18423
Rejeo la ndani la kitu
Kuhusiana na
Bangili ya shanga

Bangili ya shanga

r 2018 / 18207 c
Rejeo la ndani la kitu
Mazingira/Muktadha wa upataji/Upatikanaji
Bangili ya shanga

Bangili ya shanga

r 2018 / 18207 b
Rejeo la ndani la kitu
Mazingira/Muktadha wa upataji/Upatikanaji
Bangili ya shanga

Bangili ya shanga

r 2018 / 18207 a
Rejeo la ndani la kitu
Mazingira/Muktadha wa upataji/Upatikanaji
Kijitabu cha hesabu

Kijitabu cha hesabu

r 2018 / 18566
Rejeo la ndani la kitu
Kuhusiana na
Asili ya data ya kitu
Museen Stade
Leseni
Creative Commons Namensnennung, nicht kommerziell, keine Bearbeitung 4.0jifunze zaidi
Imepitishwa katika lango imewashwa
2025-12-04T15:34:03+01:00

Rekodi zetu za takwimu zinafanyiwa maboresho kila mara. Tafadhali wasiliana nasi ikiwa una maswali au maoni au ikiwa unahitaji taarifa zaidi au nyingine zinazohusu mali hii. Taarifa juu ya ulinzi wa takwimu.
Rudi kwenye utafutaji