Hinweis: Um die korrekte Darstellung der Seite zu erhalten, müssen Sie beim Drucken die Hintergrundgrafiken erlauben.
Slider Bild - CC BY-NC-ND 4.0
1/1

Sampuli ya karatasi, ususi

Sammlung Braun
r 2018 / 18396 b
Taasisi inayotoa
Museen Stade
Eneo la Mkusanyiko
Sammlung Braun
Nambari ya uvumbuzi
r 2018 / 18396 b
Kichwa
Sampuli ya karatasi, ususi
Vipimo
Upana: 13cm, Urefu: 24cm
Nyenzo
Plant fibre
Fasihi
Braun, Karl Ueber einige in Amani gezogene, Fasern und Flechtwerk liefernde Pflanzen, nach einem Vortrag, gehalten während der Unterrichtskurse in Amani am 11. Januar 1911, Der Pflanzer. Ratgeber für tropische Landwirtschaft, 1911, GVK
Braun, Karl Die Flechtereien der Eingeborenen in Deutsch-Ostafrika, Der Pflanzer. Zeitschrift für Land- und Forstwirtschaft, 1913, GVK
Braun, K. Mattenflechterei im ostafrikanischen Küstengebiet, 1931, GVK
Kiungo cha dondoo
https://www.amani-stade.gbv.de/item/sw_ms_521b3189-2834-4e61-9377-08b80c89a156
nakala kwenye ubao wa kunakili
Kikundi cha kitu / kitu cha mtu binafsi
Kitu cha mtu binafsi
Uzalishaji
Wakati
ca. 1912-03-25
Maelezo


chanzo: Museum der Kulturen Basel, VI 56197, 57 (174)
mwandishi: Karl Braun
Mtu
  • Mtu, haijulikani (Mtengenezaji)
Mahali
  • Kisiwa cha Chole
Acquisition:
Wakati
kutoka ca. 1912-03-25
Mtu
Mahali
  • Kisiwa cha Chole
Urithi
Wakati
1934-07-17
Maelezo
Mnamo mwaka 1934, aliyekuwa mkurugenzi wa Taasisi ya Biolojia ya Kilimo na Misitu (Biologische Reichsanstalt für Land- und Forstwirtschaft) Karl Braun (1870–1935) alitoa kile kinachoitwa “Kolonialsammlung Braun” (Makusanyo ya Mkoloni Braun) kwa Jiji la Hanseatic la Stade, au tuseme aliyekuwa mwakilishi wake, meya wa wakati huo Hans Arthur Meyer (1884–1961). Tazama faili „Uhamisho wa makusanyo ya kikoloni kutoka kwa diwani mkuu wa serikali Profesa Dk. Karl Braun huko katika Jiji la Stade” („Überlassung einer Kolonialsammlung vom Oberregierungsrat Professor Dr. Karl Braun in Stade an die Stadt Stade") katika Jimbo la Saxony ya Chini Hifadhi ya Nyalaka ya Stade (Niedersächsischen Landesarchiv Standort Stade).

chanzo: Niedersächsisches Landesarchiv Standort Stade, Dep. 10 Nr. 03025
Mtu
  • Braun, Karl (* 1870 † 1935) (Mfadhili)
    GND Explorer
  • Hansestadt Stade (Mpokeaji)
  • Hans Arthur Meyer (1884 - 1961) (Mpokeaji)
Mahali
  • Stade
Mkopo
Wakati
1997-02-17
Maelezo
Mnamo mwaka 1997, aliyekuwa mtunza kumbukumbu wa jiji kwa wakati huo Jürgen Bohmbach anahitimisha makubaliano ya makabidhiano kwa mkopo wa kudumu katika Jumba la Makumbusho (Museumsverein Stade e.V.) chini ya aliyekuwa mkurugenzi wa wakati huo Gerd Mettjes kwa kutia saini. Baadaye, makusanyiko kutoka kwa Karl Braun yalihamishiwa kwenye Jumba la Makumbusho (Museumsverein Stade e.V.) kwa ajili ya utunzaji.

chanzo: Museen Stade, Vereinbarung Leihgabe "Brauns'sche Kolonialsammlung"
Mtu
Mahali
  • Stade
Scientific use:
Wakati
2023-06-09
Maelezo
I: Hebu tuangalie hii imesajiliwa kwa namba 2018_18396_b, hebu angalia unaweza ukafahamu hicho ni kitu gani? R: Huu ni mkeka I: Huo ni? R: Mkeka I: Angalia vizuri R: Nilivohisi kama mkeka I: Kama mkeka R: Eeeeh pia niseme nimeshindwa kutambua I: Nakusikiliza R: Huu mimi nahisi ni mkeka lakini sasa hivi viungo ungo hivi vimeletwa na nini maana hivi huu ni mkeka huu amesuka na minyaa na rangi tofauti kaunganisha unganisha eeh I: Ukiunganishwa ndiyo unakuwa mkeka? R: Ni ukindu I: Haujaunganishwa ukiwa haujaunganishwa? R: Ni ukindu I: Hahahahahahah huu ni? R: Humu katikati kumbe hakujaungwa bado I: Hakujaungwa bado R: Basi sawa I: Kwahiyo huo ni nini mama? R: Ukindu R: Ukindu R: Eeeeh I: Ukindu ni jina la kabila gani ukindu? R: Ukindu kwa kisambaa tunaita misaa I: Misaa? R: Eeeeh I: Maana yake nini msaa? R: Msaa ni huu mti ambao una hivi vitu eeh I: Ni makabila gani wanatengeneza ukindu? R: Wasambaa, wabondei, wakwizu, watu wa bara wengi tu wanatengeneza wabena, wahehe, wanyakyusa, ni kazi zao hizo I: Kwahiyo mikoa ambayo inapatikana sana ukindu ni mikoa gani hasa? R: Mkoa wa tanga I: Mkoa wa Tanga R: Eeeeh I: Tanga sehemu gani hasa unapata ukindu? R: Sehemu za magunga hizo kule kwetu Lushoto ipo na humu Amani pia ipo lakini Zaidi sehemu za wagunda hapo ndiyo sana I: Na ukindu unatumikaje? R: Ukindu unatumika kwa mikeka, unatumika kwa vikapu, mikoba, vitu kama hivo ndiyo ukindu unatumika I: Na hadi sasa unatumika? R: Mpaka sasa unatumika I: Na ukindu unaweza ukawa na matumizi tofauti na kutengenezea mikeka? R: Tofauti yake I: Eeeeh R: Mikeka ni vikapu nafikiri vitu viwili I: Mkeka na vikapu R: Eeeeh na makofia haya I: Kofia? R: Eeeeeh I: Na nikina nani hasa wanatengeneza? R: Zaidi akina mama I: Akina mama R: Eeeeeh I: Wa umri gani? R: Wa umri wa miaka ishirini na tano, thelathini, arobaini, sitini na kuendelea watu wazima sana ni kazi zao I: Kwanini ni kina mama nani watu wakubwa? R: Sehemu kubwa wanatengeneza wakichoka na shamba mtu amekaa amepumzika ana kazi hii anatengeneza pia inambadilisha yani ule upweke yuko mwenyewe ana jisikia tu kufanya ile kazi anaona kama inamchangamsha eeh unachangamka hutapata uvivu wakulala lala hovyo kwahiyo inachangamsha mwili eeh I: Kwa mawazo yako inaweza ikafika wakati kwamba ukindu ukawa hauhitajiki kutumika tena kwa watu wa makabila uliyoyataja? R: Huu kupotea kabisa siyo rahisi japo sasa hivi imetokea vitu vya kisasa lakini huu kwasababu watu wanao vitengeneza watu tunasema ni wazee lakini wanavijana wanao waigiza wasichana kwahiyo hautapotea sana hautapotea kwa mikoa yote I: Watu wanaendelea kutengeneza? R: Kwasababu hivo vikapu ni endelevu na makofia vitu vyote hivo vinaendelea eeh I: Na ili ukindu utumike uanze kuutengeneza unatakiwa uwe na kitu gani kingine? R: Ukindu ili uutumie unapanga tatu uje uuanike kwenye jua ukauke uwe na pini au sindano ya kuchongea kuiweka sawa ndiyo unaanza kutumia sasa ukimaliza na uzi unaoshonea unaanza kuunganisha huo mkeka I: Sawasawa na ukindu una umuhimu gani kwako au kwa watu wa utamaduni uliowataja? R: Kutumika I: Una umuhimu gani? R: Huu una umuhimu kukalia, na kwenye shughuli I: Shughuli kama zipi? R: Shughuli za harusi, shughuli za misiba na wengine wanapamba kwenye vyumba vyao wanaweka ukutani ee ndiyo inayotumika zaidi I: Sawasawa R: Kwa njia nyingine kwa wasiokuwa na kubadilisha kuita mkeka kuna vitanda pia vilivokua vinatengenezwa kwa ukindu I: Kwa ukindu R: Eeee I: Vitanda hivo vinaitwaje? R: Vitanda vile vinaitwa vitanda vya kamba na kamba zake zile zilikuwa zinaitwa supatu kwa kisambaa eeeh I: Eheee R: Mnakwenda kutafuta supatu nitengeneze kitanda eeh ni vitanda vinavotumika sana mpaka sasa kwenye kulazia maiti vinatumika sana na hivyo vitanda vya aina hiyo I: Kwanini wanatumia kulazia maiti sana? R: Yani kama sasa ni utamaduni wanaona ni urahisi hata wakimuosha ni kwamba hawapati usumbufu maji kwenda kwenye mbao ni kama ni utamaduni wa hivyo vitanda yani hata visikosekane kwenye kijiji visikosekane itapatikana msiba lazima nani anacho lazima atafutwe eeh I: Kwahiyo ni sehemu ya utamaduni? R: Ndiyo I: Kwahiyo inamaanisha utaendelea kutumika kwasababu bado matumizi yake yapo R: Vitaendelea kwasababu matumizi bado hayatakoma eeh I: Na ukindu unatengenezwa kwa vifaa gani na vifaa gani? R: Hivi vifaa hapa ni ukindu tu unaoendelea mpaka patokee mkeka ni ukindu na kamba I: Ukindu na kamba? R: Kamba yenyewe yaweza kutumika ile ile ya ukindu au kamba ya mkonge I: Mkonge? R: Eeeeh kamba ya mkonge I: Sawasawa na nyenzo zinazotumika kutengeneza ukindu zimekuwa zikibadilika au miaka yote ni hizohizo? R: Aaah tuseme miaka yote haijawahi kubadilika I: Haijawahi kubadilika? R: Haibadiliki na kibao I: Kibao? R: Kibao wakati wakuunda unatumia kibao kuvingirisha hii kamba kushona mpaka ule mduara unaotegemea sasa umetosheka unatumia kisu kukata I: Ahhaa kukata? R: Eeeeh I: Na ukindu unathamani gani ukikadiria kwa mfano huo ukindu unaouona kwenye picha ukiletwa sokoni unaweza ukauzwa shilingi ngapi? R: Ukindu sasa hivi unathamani ukindu zamani kichanga kama kichanga hivi kinaweza kikauzwa mia tano lakini sasa hivi kichanga cha ukindu kinafikia shilingi elfu moja I: Elfu moja? R: Eehh I: Kwahiyo hicho ambacho kimeshasukwa hivo kinaweza kikauzwa shilingi ngapi? R: Duara moja I: Kimesukwa kimewekewa rangi kama hivo unavoona R: Ni shilingi elfu thelatini mpaka elfu arobaini eeh unatumika hata kutunza maharusi vinafikia hata arobaini elfu I: Sawasawa basi asante tumepata maelezo mazuri sana kwenye ukindu hahahhaha R: Hahahahhah umetosheka I: Eeeeh sasa tuchukue picha yetu ya mwisho siku ya leo R: Ndiyo

chanzo: Amani-Stade Project / Amani Field Research 2023, Interview No. 03
mwandishi: I: Mohamed Seif, R: Anonymous
Mtu
  • National Institute for Medical Research (NIMR) (Mteja)
  • unknown actor (wissenschaftlicheR BearbeiterIn)
Mahali
  • Amani
Scientific use:
Wakati
2023-06-10
Maelezo
I: Sawa hapa mkononi nina picha nyingine imesajiliwa kwa namba 2018_18396_b hebu angalia unaweza ukkatambua ni kitu gani hicho? R: Huu ni ukili I: Ukili? R: Eeeeh I: Hivi ukili au ukindu? R: Ukili I: Ukili na ukindu vinatofauti gani? R: Ukindu ni mbichi eeh ama umekaushwa ukindu huu umesukwa ni ukili I: Kwahiyo ukisukwa unakuwa ni ukili? R: Eeeeh maana hapo unaweza kuunganisha ukawa mkeka I: Nani makabila gani walikuwa wakitengeneza ukili? R: Wote wasambaa, kabila za bara wote tulikua tunatumia I: Mikoa gani hasa ulikuwa unaweza ukapata ukili? R: Ukili hata huku kwetu upo I: Tanga? R: Eeeeh I: Na mikoa mingine unayoifahamu? R: Aaaaa mingine siifahamu I: Ulikuwa unatumikaje? R: Huu I: Eeeh R: Huu unatumika kama hivi nilivokuambia kuwa kama ukisuka kama hivi unaunganisha hivi unapima kiasi cha kutoka mkeka ukitoka mkeka unatumika kama mkeka I: Ulikua ni kwa ajili ya mkeka tu au vitu vingine vilikuwa vinatimika kutengenezwa na ukili hebu tuelezee? R: Vinatengenezwa kuna mifuko, kuna makawa, kuna vipepeo, eeh I: Mifuko, makawa, vipepeo, vyote vilikua vinatengenezwa na ukili? R: Eeeeh I: Ahaaa na watu gani walikuwa wakitengeneza jinsia gani walikuwa wakitengeneza? R: Wakike I: Kwanini wakike? R: Wanajua vya kukalia chini, mwingine anapamba kwenye ukuta eeh I: Wa umri gani hao wakina mama walikuwa wakitengeneza? R: Wazee eeh I: Kwahiyo ilikuwa ni kazi ya wazee? R: Eeeeh I: Kwanini ilikuwa kazi ya wazee? R: Wazee wenyewe wanajua mahitaji ya ndani eeh I: Vijana hawajui? R: Aaa hawajui bao hahah I: Hhahahaha sawasawa unadhani inaweza ikafika kipindi ukili ukawa hauna thamani tena wakutumika na jamii ya wasambaa hapa kijijini kwenu? R: Saivi hawatumii kwasababu wanaita manini yale wanayoyatandika mabusati saivi dniyo wanatumia huu umekufa sasa I: Umekufa? R: Ukiona anasuka ni mmoja mmoja sasa I: Kwahiyo saivi umeletwa mabusati? R: Eeeh basi hayo ndiyo yanayotumika saivi badala ya mkeka I: Kwahiyo matumizi ya mkeka? R: Yamepitwa na wakati I: Kwahiyo itafika wakati itakuwa hamna kabisa? R: Eeeeh hamna kabisa I: Sawasawa na ili uweze kutumia ukili unatakiwa uwe na kitu gani kingine? R: Ni uzi I: Uzi? R: Eeeeh sindano, unatumia ya kushonea lakini ukisuka tu kama hii ni mkono tu I: Ni mkono? R: Eeeh ni mkono tu ukitaka kuunganisha sasa unatumia sindano na uzi eeh I: Kwahiyo ukishasuka wenyewe unatafuta sindano na uzi ndiyo unanza kuunganisha? R: Eeeeh inakuwa mkeka I: Ni uzi na sindano? R: Eeeeh kawa, vipepeo, mifuko ni uzi tu na sindano I: Kawa ni nini? R: Ni cha kufunikia chakula I: Aaaaa vile vya kufunikia chakula? R: Eeeeh I: Unacho hapa? R: Eeeeeh I: Hhahahah tutaomba kuona tukimaliza hapa R: Haya I: Sawa na waliokuwa wanatengeneza ni watu wa jinsia gani? R: Akina mama I: Akina mama? R: Eeeeh I: Kwanini? R: Kwasababu wanajua matumizi yake R: Eeeeeeh ukitoa chakula mgeni amekuja unafunika kwanza ili inzi asiguse I: Kwa ajili ya kufunikia chakula? R: Eeeh! I: Kwa Tanga ni maeneo gani ya Tanga vinatengenezwa sasa hivi? R: Tena Tanga ni wote I: Wote? R: Eeeeh I: Unaweza ukajua ni wilaya gani na wilaya gani? R: Ni hiyo hiyo ya Tanga ndiyo ninayoijua I: Kwahiyo sehemu zote za Tanga wanatengeneza? R: Eeeeh I: Sawasawa na vifaa vinavyotumika kutengenezea ukili hizo umesema ukindu, sindano, na uzi vimekuwa vikibadilika? R: Ni hivyo hivyo I: Miaka yote haijawahi kubadilika? R: Yote hivyohivyo havibadiliki I: Ni uzi wa namna gani ulikuwa ukitumika? R: Hata huo wa ukindu wenyewe unaweza ukapasua unashona huohuo wa ukindu unaweza ukapasua ukindu wako kidogo unatia kwenye sindano unashonea I: Ukiangalia jinsi ilivonakishiwa huo ukili huo ukiletwa kwenye masoko yetu ya sasa hivi unaweza ukauzwa shilingi ngapi? R: Saivi ni elfu ishirini na tano I: Kwasababu gani unaweza ukauzwa elfu ishirini na tano? R: Siwanauza bei za zamani ee wazee wa zamani hawana bei hata saivi akikushonea mkeka ujue ni ishirini na tano elfu tu I: Ishirini na tano? R: Eeeh

chanzo: Amani-Stade Proejct / Amani Field Research 2023, Interview No. 09
mwandishi: I: Mohamed Seif, R: Anonymous
Mtu
  • National Institute for Medical Research (NIMR) (Mteja)
  • unknown actor (wissenschaftlicheR BearbeiterIn)
Mahali
  • Amani
Mwandishi: Karl Braun, Tarehe ya kutengenezwa: 1912-03-25, Nukuu/Angalizo: Museum der Kulturen Basel, VI 56197, 57 (168-174)jifunze zaidi
Asili ya data ya kitu
Museen Stade
Leseni
Creative Commons Namensnennung, nicht kommerziell, keine Bearbeitung 4.0jifunze zaidi
Imepitishwa katika lango imewashwa
2025-12-04T15:40:04+01:00

Rekodi zetu za takwimu zinafanyiwa maboresho kila mara. Tafadhali wasiliana nasi ikiwa una maswali au maoni au ikiwa unahitaji taarifa zaidi au nyingine zinazohusu mali hii. Taarifa juu ya ulinzi wa takwimu.
Rudi kwenye utafutaji