Wakati
2023-06-09
Maelezo
I: Haya, hii ya mwisho ukishindwa hii basi tutakuwa tumeishia hapa, haya hii ni picha imesajiliwa kwa namba 2018_18316_001, hebu angalia unaweza ukafahamu hicho ni kitu gani?
R: Hiki ni kikapu kilichotengenezwa na matete
I: Kikapu kilichotengenezwa na matete?
R: Eeeeh
I: Kikabila inaitwaje kikishakuwa kimetengenezwa hivo?
R: Kitezu
I: Kitezu?
R: Eeeeh kitezu
I: Maana yake ni nini kitezu?
R: Kitezu hiki maana yake ni kikapu bali hiki kimeenda mfano wa mkoba eeh
I: Na kikapu hiko kimekuwa kikitengenezwa na watu wa utamaduni gani hasa?
R: Hiki haswa na wabena
I: Wabena
R: Wahehe watu wengi wa bara wabena na wahehe
I: Wabena na wahehe
R: Ndiyo
I: Na kilikuwa kikitumikaje?
R: Hiki kilikua kinatumika sana kuhifadhia unga ndani ya nyumba eeh kama tunavohifadhi kwenye ndoo sasa hivi hiki sanasana kilikuwa cha unga ndani
I: Cha kuhifadhia unga
R: Lakini sasa naona hiki kina uwazi uwazi
I: Kina matundu makubwa kidogo hiki
R: Kina matundu makubwa kidogo hata kwendea shamba kuvuna mboga, mahindi vinatumika hivi
I: Kwahiyo kina matumizi mengi?
R: Eeeh
I: Na watu gani walikuwa wakitumia sana?
R: Yani hiki watu wa bara kuanzia wabena, wahehe haya makabila gani haya wangoni
I: Wabena, wahehe na wangoni
R: Na hawa wafipa hivi vitu ndiyo vinatumika sana eeh kwa wasambaa hivi hapana siyo sana hamna labda anunue tu lakini siyo asili yetu hii
I; Sawasawa hapa kuna wabena kwani?
R: Eeeeh wengi tu
I: Itabidi tupate mbena mmoja
R: Hapa wapo bali zaidi ya hapa ni kwenye kuhifadhia unga na kwendea kenye mboga maana tuliletewa hata sisi tuliolewa na wabena tuliletewa zawadi eeh
I: Na ndiyo mlikua mnatumia kufanyia hivo?
R: Eeeeh tulikuwa tunatumia wanakuletea kikubwa cha kuhifadhia ndani na kidogo cha kuchotea unga ndani kuja jikoni eeh
I: Na wewe ulishawahi kutumia?
R: Eeeeh nimeshawahi kutumia
I: Wewe ulitumia kwa muda gani?
R: Ah vinadumu hivi eeh hata vingine vidogo wametuletea tunawekea sadaka kanisani eeh
I: Kwa matumizi ya sasa?
R: Eeeeh
I: Lakini kipindi hicho ilikua ni kuhifadhia unga na kwenda kuvunia?
R: Eeeeh kwenda kuvunia yani hiki kikubwa chakuvunia na hiki kingine cha matumizi ya ndani hivi vidogo tuliletewa hata sisi na wamama wakibala walituletea viko kanisani hapo tulikua twawekea sadaka kwahiyo sasa hivi sasa tumeacha tu kwa ajili kuna mifumo ya kisasa wametengeneza vya mbao eeh lakini hivi vitu zaidi ni vya kibala
I: Vya kibala?
R: Eeeeh
I: Kati ya wanaume na wanawake akina nani wanatumia zaidi?
R: Ni wanawake
I: Wanawake?
R: Eeeeh
I: Umesema kinaitwaje?
R: Kitezu
I: Kitezu:
R: Eeeeh ni mkoba wa kikapu yani kwa mbena atajua jina lake sasa zaidi eeh
I: Sawasawa na kwa mawazo yako inaweza ikafika wakati kikawa hakihitajiki tena?
R: Hivi havitapotea
I: Kwasababu gani?
R: Kwa kupotea vinaweza vikapotea kwa hii mikoa ambayo sisi tunaletewa lakini kwa kule bara havitapotea sana kwasababu hivi vifaa wanavyo wenyewe hii minyaa wanayo, na matete haya wanayo na ufundi wanao eeh
I: Na ili kutumia hicho kitezu unatakiwa uwe na kitu gani kingine?
R: Tena hapa ni kutumia tu hii peke yake maana hapa unavitembeza tu vyenyewe na kidole hiki eeh bali kwa ila kutengeneza lazima pawe na kisu na huku juu kutakuwa na sindano ya kukazia lakini huku ni kamba zenyewe ndiyo zinazozunguka mpaka zikafanya hivi
I: Sawasawa na waliokuwa wanatumia zaidi ni wanawake au hata wanaume pia?
R: Hata wanaume kama kipo ndani mwanaume ila kwa utengenezaji ni wanawake
I: Watengenezaji ni wanawake?
R: Eeeeh
I: Na wanawake wa kuanzia umri gani wanatengeneza zaidi?
R: Miaka kumi na tano, kumi na sita na kuendelea mpaka miaka hamsini sitini mpaka sabini kama mimi
I: Kwanini wanawake?
R: Kwasababu kinatumika sana ni kazi za jikoni eeh
I: Kazi za jikoni?
R: Ndiyo
I: Sawasawa na umesema vinatumia matete, kitu gani kingine kimetumika kutengenezea hicho kitezu?
R: Hapa kukazia huku juu imetumika sindano hizi kubwa za kushonea magunia
I: Sindano
R: Na uzi
I: Uzi?
R: Eeeeh
I: Sawasawa labda vitezu vya sasa hivi ambavyo mnaletewa ambavyo vinatumika hadi makanisani utofauti na material yaliyotumika kutengenezea au nyenzo?
R: Havina tofauti bali vya zamani ni imara Zaidi
I: Kwanini vya zamani ni imara Zaidi?
R: Wale watengenezaji zamani akitengeneza kitu sianatengeneza ngumu lakini sasa hivi anatengeneza kitu kiishe upesi ni biashara ili aendelee kutengeneza kwahiyo wako kibiashara zaidi
I: Sawasawa hasa ukiangalia kitezu hicho cha miaka hiyo ya elfu moja mia tisa miaka mia iliyopita kikiletwa katika masoko yetu ya sasa kinaweza kikauzwa shilingi ngapi?
R: Hiki sasa hivi kinaweza kikauzwa elfu kumi mpaka kumi na tano eeh
I: Aha
R: Kumi mpaka kumi na tano
I: Kumi mpaka kumi na tano?
R: Eeeeeh
I: Sawa mimi nishukuru kwa ushiriki wako wa siku ya leo umetusaidia taarifa nyingi sana kwahiyo tushukuru sana kukubali ushiriki wako asante sana
R: Asanteni na nyinyi
I: Haya asante
chanzo: Amani-Stade Project / Amani Field Research 2023, Interview No. 03
mwandishi: I: Mohamed Seif, R: Anonymous
Mtu
-
National Institute for Medical Research (NIMR)
(Mteja)
-
unknown actor
(wissenschaftlicheR BearbeiterIn)
Mahali