Hinweis: Um die korrekte Darstellung der Seite zu erhalten, müssen Sie beim Drucken die Hintergrundgrafiken erlauben.
Slider Bild - CC BY-NC-ND 4.0
1/1

Vipande viwili vya vito vya masikio

Sammlung Braun
r 2018 / 18238
Taasisi inayotoa
Museen Stade
Eneo la Mkusanyiko
Sammlung Braun
Nambari ya uvumbuzi
r 2018 / 18238
Kichwa
Vipande viwili vya vito vya masikio
Nyenzo
Kauri,
Kioo shanga,
Udongo,
Tallow,
Nywele
Kiungo cha dondoo
https://www.amani-stade.gbv.de/item/sw_ms_2f7e325c-97a1-441f-a4e1-5ce48a209c30
nakala kwenye ubao wa kunakili
Kikundi cha kitu / kitu cha mtu binafsi
Kitu cha mtu binafsi
Uainishaji
Vito vya mwili na nguo (nguo za wanaume)  
Vito vya mwili na mavazi (Nguo za wanawake)  
Uzalishaji
Wakati
mpaka ca. 1906-04-10
Mahali
  • Tansania
Ethnolojia
  • Massai  
Kununua / Uuzaji
Wakati
1906-04-10
Maelezo
„Jumanne 10. Mwezi wa nne 1906. [imepigwa mstari] kwa muda wa siku kadhaa nikapokea vitu vya kimila: mapambo ya masikioni ya Masai. Hutengenezwa kwa udongo na kupakwa udongo mwekundu. Udongo huo umechanganywa na ulanga vitu vyanuka vibaya mno . Udongo umewekewa shanga za buluu. Nywele hutumika kama manyamunyamu. 1 = Hella 25 [mchoro] kengele zinazovaliwa wakati wa kucheza ngoma [ngoma] zaidi ya 50 kwenye utepe wa manyoya. Zimetengenezwa kwa mkono kwa kupiga nyundo karatasi za vyuma zenye umbo wa mduara.kwa kengele 50 nikalipa 3 Rup. 75. [michoro makini miwili]" [Utafsiri]

50 Heller / Stk

chanzo: Museum der Kulturen Basel, VI 56197, 46 (115)
mwandishi: Karl Braun
Mtu
Mahali
  • Amani
Malipo
Wakati
kutoka ca. 1906-04-10
Maelezo
"69. Mapambo ya masikio ya Masai, udongo mwekundu & mafuta ya ngombe. yamewekewa shanga za kioo kadha za buluu & nyeupe. Nywele zimewekwa kama manyamunyamu / 1 = 25 Hela / Amani 10. mwezi wa nne 1906 / TB. 46,115 [mchoro]"

chanzo: Museen Stade, r 2018 / 18566
mwandishi: Karl Braun
Mtu
Nambari za hesabu za zamani
  • 069
Urithi
Wakati
1934-07-17
Maelezo
Mnamo mwaka 1934, aliyekuwa mkurugenzi wa Taasisi ya Biolojia ya Kilimo na Misitu (Biologische Reichsanstalt für Land- und Forstwirtschaft) Karl Braun (1870–1935) alitoa kile kinachoitwa “Kolonialsammlung Braun” (Makusanyo ya Mkoloni Braun) kwa Jiji la Hanseatic la Stade, au tuseme aliyekuwa mwakilishi wake, meya wa wakati huo Hans Arthur Meyer (1884–1961). Tazama faili „Uhamisho wa makusanyo ya kikoloni kutoka kwa diwani mkuu wa serikali Profesa Dk. Karl Braun huko katika Jiji la Stade” („Überlassung einer Kolonialsammlung vom Oberregierungsrat Professor Dr. Karl Braun in Stade an die Stadt Stade") katika Jimbo la Saxony ya Chini Hifadhi ya Nyalaka ya Stade (Niedersächsischen Landesarchiv Standort Stade).

chanzo: Niedersächsisches Landesarchiv Standort Stade, Dep. 10 Nr. 03025
Mtu
  • Braun, Karl (* 1870 † 1935) (Mfadhili)
    GND Explorer
  • Hansestadt Stade (Mpokeaji)
  • Hans Arthur Meyer (1884 - 1961) (Mpokeaji)
Mahali
  • Stade
Mkopo
Wakati
1997-02-17
Maelezo
Mnamo mwaka 1997, aliyekuwa mtunza kumbukumbu wa jiji kwa wakati huo Jürgen Bohmbach anahitimisha makubaliano ya makabidhiano kwa mkopo wa kudumu katika Jumba la Makumbusho (Museumsverein Stade e.V.) chini ya aliyekuwa mkurugenzi wa wakati huo Gerd Mettjes kwa kutia saini. Baadaye, makusanyiko kutoka kwa Karl Braun yalihamishiwa kwenye Jumba la Makumbusho (Museumsverein Stade e.V.) kwa ajili ya utunzaji.

chanzo: Museen Stade, Vereinbarung Leihgabe "Brauns'sche Kolonialsammlung"
Mtu
Mahali
  • Stade
Scientific use:
Wakati
2023-10-03
Maelezo
I: Sawasawa asante ngoja tujadili picha moja ya mwisho ili tukaendelee na majukumu mengine nina picha nyingine hapa ambayo imesajiliwa kwa namba 2018_18238_1 hebu nikumbusheni jina la hiki kitu? R1: Sasa hiki kitu ni kama desturi moja ya kimasai wakati mtoto anaanza kukua kutoka kwenye utotoni na kuelekea kwenye kijana kwenda kutahiriwa anaweza sasa akavalishwa hiki kikaninginizwa tu hapa shingoni anavaa siku ya kwanza ya pili siku nyingine inatolewa wanapewa watoto wengine siyo kitu ya kudumu nacho baada tu ya kuvalishwa lakini inavaliwa kwa kipindi hicho. I: Siku akiwa anaenda wapi? R1: Siku ile akiwa anaenda kutahiriwa yani kuna aina ya mifugo baadhi ambayo zinasindikiza kama mbuzi ambo wanaitwa lailibono sasa mkishatoka wanaita orikitukubene ndiyo siku hiyo unatoka sasa unavalishwa hii baada ya mbuzi kuchinjwa ikisha chinjwa hii miti inatolewa sasa yani kwa tafsiri nyinyi mnasema ni udongo lakini hatujakuta hizo tumekuta njia yake ya kuendeleza ni kama tunda la miti ulani. I: Mti huo unaitwaje? R1: Olikimogiki sasa ndiyo inapekechwa sasa ikishapekechwa inawekwa ile uzi hadi inakamilika. I: Uzi gani ulikuwa unatumika kuweka? R1: Yani ni igonoti ngozi iliyokwanguliwa ngozi ya kondoo. I: Ngozi ya kondoo? R1: Eeeeh ikishaanza kuwekwa anavaa baada sasa ya kwenda kutahiriwa yani siku hiyo unaimbiwa ukiwa nayo unalala usiku na siku hiyo unaimbiwa bila kuvaa nguo moja ila tu hiki kipo shingoni. I: Huna nguo yoyote? R1: Huna nguo hata moja unapingwa na baridi mpaka asubuhi saa kumi na mbili unaelekea pale uangaliwe ujasiri wako kama utaweza kukubali ile kisu upingwe tu bila kunungunika na bila sindano hasa ndiyo siku hiyo unatolewa yote hayo yalikuwa yanafanyika kupima ujasiri wako ulionao. I: Kwahiyo ilikuwa ni kwa ajili ya vijana wa kiume tu? R1: Eeeh yoyote wa kiume hata wasichana ila wasichana hawatoi nguo kwanza hawaruhusiwi na hawaimbiwi kabisa. I: Anayeimbiwa niwa kiume tu? R1: Eeeh wa kiume tu yani unateswa tu ili kupata hasira ili kama una hasira kabisa yani unadamka asubuhi uwe unangangana na ile kisu eeh ya yule jamaa anayetahiri na haitakiwi sindano aa unabaki hivyohivyo saa kumi na mbili au sa moja moja ndiyo sasa uonekana kwamba unaweza huogopi kisu. I: Kwahiyo akisha tahiriwa hiyo anavuliwa? R1: Eeeeh anatolewa. I: Siku hiyo hiyo? R1: Eeeh anatoa hii anapewa malaiyoni. I: Namba mbili ilikuwa ina umuhimu gani? R2: Unajua zamani vijana kama hajatahiriwa anakaa sana kwa vijana ndiyo wanafanya vitu vingine vya ajabu ajabu anaua ua vitu hovyo hovyo kwahiyo hiyo ni kitu kilichokuja kufaa hii akiamka asubuhi kuna maji fulani anaoshwa na hii maji fulani akioshwa na maji fulani ndiyo anatoa hii. I: Maji gani hayo? R2: Haya ni maji ambayo haichemshwi yanakuwa ya baridi lakini kuna chuma fulani anapoweka haya maji. I: Chuma hiyo inaitwaje? R2: Inaitwa endolu wengine wanaita ondido anapoweka anavooshwa na haya maji baridi na atatoa hizi vitu au wakisema vitu vya watoto sirudii tena kufanya maana chochote ulichofanya wakati wa utotoni ndiyo anasema anaomba msamaha leo anaviacha wakati bado hajatahiriwa sasa hivi anakuja kuingia kwenye uwanaume fanya kazi yoyote hiyo yote maana unakuta akipita paka vitu vingine haviliwi ndiyo atakuwa ameoshwa siku hiyo hutakiwi ukiwa mwanaume kila kitu ule ule lakini usile kitu ambacho hakiliwi katika jamii yetu ya kimasai maana ni dhambi kwako maana hiyo katika sisi wamasai kwa mila yetu tunasema tunajaribu kuacha vitu vilivyofanywa na vijana. I: Khaa historia ndefu hahhha kwahiyo ilikuwa ni kama kumuosha kumtakasa na yale yote aliyofanya? R2: Kabisa. I: Akitoka hapo anakuwa mweupe? R2: Kabisa kabisa mweupe. I: Sawasawa na wanaowaosha ni watu gani? R1: Sasa hiyo kuosha ni sio mtu mkubwa ambaye ametahiriwa ile maji ambayo inawekwa ile kitu kama shoka aina ya ulimi wa shoka na chuma ambacho kina mpini kidogo wa kijiti sasa ile maji ni kwamba ni kama sindano fulani lakini haina sindano ni kama ile pedoli ya baskeli ichongwe kabisa iwe ni kama chuma yenye ukali kabisa sasa ile inachukuliwa yale maji yanatundikwa kwenye baridi. I: Kwenye mti au kwenye nini? R1: Juu ya nyumba na yanalindwa na mtu, mtu anawekwa wakulinda yale maji yani yanawekwa kuanzia sa mbili ya usiku yanapingwa na baridi mpaka saa kumi na mbili ya asubuhi na hayachemshwi yani kitu chake kinachofanyia kuweka yale maji kwenye friji ni ile chuma baada sasa ya kutoka kwenda nje ya boma kutahiriwa unaenda nje ya boma kidogo yale maji unamiminiwa kuanzia kichwani na haitakiwi kusema yani kusikia kwamba niya baridi yani wewe tu uone kama maji ya moto kwahiyo hutakiwi kunungunika wala kufanyaje alafu ile safuria unaipiga teke moja yani ukishamaliza kumiminiwa na yule kijana mguu mmoja unaambiwa unapiga na mguu huu tu. I: Mguu gani? R1: Mguu wa kushoto ndiyo unaotumika katika kupiga sufuria huwezi ukapiga na mguu wa kulia. I: Maana yake nini kupiga na mguu wa kushoto? R1: Yani hivyo vitu ni kama uhalifu fulani wa vitu ambavyo havina maana ulivyovifanya ukiwa utotoni kama kuua kitu ambacho hakifai kuua umekitesa na kukiua bure ni kheri uue kitu ambacho kinaliwa lakini kama umeua kitu ambacho hakiliwi au kama punda hauli nyama na umeua paka hauli nyama, pundamilia hauli nyama, na umeua sasa ndiyo unajaribu kuyasafisha hayo yote umetoka kwenye hilo group la kufanya ujinga unaelekea sasa kwenye group la waerevu unapiga sasa teke safuria na mguu wa kushoto unakimbilia sasa kwa yule dakitari anaeenda kukutahiri sasa ndiyo taratibu za hivyo vitu katima mila na desturi katika jamii yetu ya kimasai. I: Sawasawa na hizo walikuwa wanatengeneza wakina nani? R1: Hii ni mama anatengeneza na maji ni mama anayelinda mpaka asubuhi yale maji ya kulala nje kutoka saa mbili usiku anayalinda pale yalipowekwa mpaka saa kumi na mbili asubuhi ndiyo anamkabidhi anayehusika hatakiwa kuondoka na kuyaacha yenyewe maana hayatakiwi kuguswa kabisa. I: Mama ndiyo analinda mpaka aje sasa mzee mmoja wa kuchukua na kwenda kumkabidhi layoni wa kummiminia yule mtu. I: Mpaka sasa bado vinatumika hivi? R1: Hiyo inatumika kabisa. I: Sawasawa. R1: Kwasasa hivi unajua wanawatoa watu kwa group kwahiyo sahivi bado miaka mitatu ndiyo waanze tena maana unajua magroup ya rika yakitolewa inaweza ikawekwa kuanzia miaka sita mpaka saba yani watu wamekatwa hakuna kutahiriwa tena hadi miaka mingine ya kutahiri itakapofika. I: Mpaka miaka sita ikifika tena? R1: Ndiyo mpaka miaka saba ikifika tena watu wameshaanza kukua wameshatanuka akili kidogo hilo group na lenyewe sasa ndiyo wananza sahivi wanatoa tena garanteen ya miaka mitatu kutahiriwa au ,miaka minne kutahiriwa hilo group lingine tena ikishafika miaka minne yani watu wa mila wanajua kwamba sasa hivi tunako elekea tushatahiri watu miaka minne mfululizo wanaenda kuingilia watoto wadogo ambao hawafai kutahiriwa ilibidi tufunge kabisa moja kwa moja mpaka miaka mingine ili watu wakue vizuri nawakomae kiakili ndiyo waweze kutahiriwa tena. I: Sawa labda tumalize na namba tatu hebu tupe historia kidogo ya olimokogiki naam karibu sana namba tatu? R3: Unajua hawa wameshaeleza vizuri kwasababu wanawatengeneza wakati wa kutahiriwa kwahiyo hawa wameshaeleza. I: Sawasawa namba nne ni hivyohivyo au kuna cha kuongeza. R4: Wameelezea vizuri kwasababu wamepitia hali moja ambayo inaitwa olimokogiki ambayo wanavaa kipindi wakati huyu kijana anatahiriwa wa kimasai kwasababu inakuwaga mara mbili wakati sasa anaenda kutahiriwa kuna dume linachinjwa hapo tayari imeshabarikiwa naya pili ambayo ndiyo olimokogiki ndiyo inatumika ambayo ni dume la kondoo ndiyo sasa inafanyika hapo ili uweze kwenda kutahiriwa kwahiyo hapo wameelezea vizuri kwasababu unatumia hiyo mpaka ile siku unatahiriwa mwisho unakaa nayo siku mbili inakuwa kazi yake imeshaisha kabisa kwa wakati huo eeh. I: Kwahiyo hilo dume la kondoo linachinjwa kabla ya kutahiriwa au baada ya kutahiriwa namba nne hebu tuambie? R4: Kabla hujatahiriwa yani siku hiyo kama ni jana ndiyo dume la ng’ombe limeshabarikiwa sasa hii siku ya pili ndiyo linachinjwa hili dume la kondoo ambalo linatumika siku moja hiyo siku unaenda siku ya tatu unaingia kwenye kutahiriwa ndiyo mila na desturi za jamii ya kimasai zilivyo. I: Sawasawa asante sana namba nne umeongea kidogo taarifa ndiyo maana ya kufanya kwenye kundi kama hivi mwingine akisahau mwingine anakumbushia sawasawa basi mimi nichukue fursa hii kuwashukuru tumejadili picha nyingi kidogo na muda umekimbia najua kuna nyingine zimebaki lakini tutaendelea kwasababu tuna makundi mengine yanayofuata naamini tunaweza tukapata taarifa hizo kwahiyo mimi niwashukuru kwa muda wenu asanteni sana na kwa maelezo mazuri mimi nimetokea kuipenda hii kazi maana najua mila na desturi za watu sahivi kwahiyo nashukuruni sana kwa muda wenu. R: WOTE: Sawa. I: Asanteni sana. R: WOTE: Haya.

chanzo: Amani-Stade Project / Massai Field Research 2023 / Interview No. 06
mwandishi: I: Mohamed Seif, R1-4: Anonymous
Mtu
  • National Institute for Medical Research (NIMR) (Mteja)
  • unknown actor (wissenschaftlicheR BearbeiterIn)
Mahali
  • Orbomba
Mwandishi: Karl Braun, Tarehe ya kutengenezwa: 1909-03-31, Nukuu/Angalizo: Museum der Kulturen Basel, VI 56197, 53 (42)jifunze zaidi
Mwandishi: Karl Braun, Nukuu/Angalizo: Museen Stade, r 2018 / 18566jifunze zaidi
Mwandishi: Karl Braun, Nukuu/Angalizo: Museen Stade, r 2018 / 18566jifunze zaidi
Mwandishi: Karl Braun, Tarehe ya kutengenezwa: 1906-04-10, Nukuu/Angalizo: Museum der Kulturen Basel, VI 56197, 46 (115)jifunze zaidi

Rejeo la ndani la kitu

Vito vya masikio

Vito vya masikio

r 2018 / 18435 c
Rejeo la ndani la kitu
Kitu kinacholingana
Kengele kwenye kamba ya ngozi

Kengele kwenye kamba ya ngozi

r 2018 / 18204
Rejeo la ndani la kitu
Kuhusiana na
Kengele kwenye kamba ya ngozi

Kengele kwenye kamba ya ngozi

r 2018 / 18261 a
Rejeo la ndani la kitu
Kuhusiana na
Asili ya data ya kitu
Museen Stade
Leseni
Creative Commons Namensnennung, nicht kommerziell, keine Bearbeitung 4.0jifunze zaidi
Imepitishwa katika lango imewashwa
2025-12-04T15:00:08+01:00

Rekodi zetu za takwimu zinafanyiwa maboresho kila mara. Tafadhali wasiliana nasi ikiwa una maswali au maoni au ikiwa unahitaji taarifa zaidi au nyingine zinazohusu mali hii. Taarifa juu ya ulinzi wa takwimu.
Rudi kwenye utafutaji