Wakati
2023-06-09
Maelezo
I: Hapa ninapicha nyingine ambayo imesajiliwa namba 2018_18300_1 hebu angalia unaweza ukatambua ni kitu gani hicho?
R: Ni mfuko uliotengenezwa na aina ya Ngozi
I: Ni mfuko ulio tengenezwa na ngozi unaweza ukafahamu jina la mfuko huu?
R: Mh hapana
I: Hapana
R: Eeeeh
I: Unaweza ukahusisha na tamaduni za watu gani mfuko huu?
R: Labda wanaoweza kutengeneza vitu kama hivi niseme labda wamasai
I: Wamasai?
R: Eeeeeeh
I: Mikoa gani wanapatikana Zaidi watu hawa?
R: Mikoa wanayopatikana wamasai mikoa ya Kilimanjaro, mikoa ya Tanga,
I: Unaweza ukafahamu matumizi ya mfuko huu?
R: Matumizi ya mfuko huu ni kuwekea vitu mbalimbali eeh
I: Kama vitu gani vinaweza vikahifadhiwa huku?
R: Kama ni mwanamke ni mkoba wa kusafiria unaweka vifaa vyako vya aina zote unavyotaka kusafiri navyo
I: Sawasawa nani jinsia gani wanaweza wakatumia mfuko wa aina hiyo kwenye jamii ya kimasai?
R: Hapa ninaweza sema jinsia ya kike eeh na wenye umri kuanzia miaka kumi na nane na kuendelea
I: Unadhani inaweza ikafikia kipindi kifaa hicho kikawa hakina thamani na kutumika tena katika jamii ya kimasai?
R: Sidhani kwasababu hiki kifaa hakiwezi kikatoka thamani kwasababu ni kifaa ambacho kina umuhimu kwao siyo kwao tu hata kwa wengine kwahiyo huwezi kama sisi wanawake huwezi ukatoka bila mkoba maana yake hapo nitaweka vitambulisho vyako utaweka sijui kalamu zako vitu vya aina mbalimbali tuseme hela zako utaweka hapo kwahiyo hiki sioni kama hakina thamani kina thamani wakati wote
I: Thamani wakati wote kwa mantiki hiyo kinaendelea kutumika hivi karibuni umewahi kuona mikoba kama hiyo inaendelea kuzalishwa?
R: Kwa kweli sijawahi kuona sijawahi kuona kwasababu muda mrefu niko huku na hizi wan apenda kuzalisha watu wa mikoa ile ya Kilimanjaro kwa upande wa wamasai
I: Nawanaotengeneza ni wamasai wa kike au kiume Zaidi Zaidi?
R: Kwa kweli sijawahi kuwaona ila nimewahi kuona wakiwa wanauza
I: Wanauza?
R: Eeeeh sasa sijajua wanaotengeneza ni mwanamke au mwanaume
I: Sawasawa umetaja nyenzo iliyotumika kutengeneza hao kwamba ni ngozi ni nyenzo gani nyingine unaona imetumika hapo?
R: Mimi siwezi kujua
I: Tukipe thamani tukikadirie thamani ya huo mkoba umeletwa umeenda sasa hivi ukaukuta ukaupemda unaweza ukaununua shilingi ngapi?
R: Hapa hata elfu kumi nanunua
I: Kwanini?
R: Kwasababu ngozi ni kitu ambacho kinadumu kwa muda mrefu alafu hakiishi thamani yake
I: Kwahiyo hata ikikaa miaka mia ijayo kitaendelea kuwa na thamani ile ile?
R: Eeeeeh ukiwa mtunzaji
I: Kama ni mtunzaji?
R: Eeeeeh
chanzo: Amani-Stade Project / Amani Field Research 2023, Interview No. 03
mwandishi: I: Mohamed Seif, R: Anonymous
Mtu
-
National Institute for Medical Research (NIMR)
(Mteja)
-
unknown actor
(wissenschaftlicheR BearbeiterIn)
Mahali