Wakati
2023-10-03
Maelezo
I: Sawasawa asante nina picha nyingine hapa ambayo imesajiliwa kwa namba 2018_18232_1 kuna mtu aliitambua hii inaitwaje kimasai hii?
R2: Engalemu maana hiyo sahivi hii iko ndani ya mila mpaka sahivi mzee akitoka kuchinja dume lale au chochote tu ni kisu ambacho kipo vizuri anahalalisha hakifanyii kitu chochote ni kuchinjia dume la ng’ombe maana hiyo inaitwa engaremu
I: Kwahiyo ni kwa ajili ya kuchinja tu dume la ng’ombe au kuna matumizi mengine kinatumika namba mbili hebu tuambie?
R2: Eeeeh
I: Na anayekaa nacho hicho kisu ni nani?
R2: Mzee
I: Wakuanzia umri gani?
R2: Mzee ndiyo anaweka sehemu yake au unamkuta mke wako uliye muamini sema haendi kutumia kwenye matumizi mengine anapewa anaweka kama hii maana haiwezi kuguswa na mtu mwingine
I: Haiguswi na mtu mwingine?
R2: Eeeeeh
I: Na wanaotengeneza hiyo ni kina nani?
R2: Wazee
R1: Hichi ni kisu najua kinatumika kwa vitu vingi sana moja mzee anaweza akatumia kwa ajili ya kuchinjia mbili kuna kipindi unakuta sasa hivi kama tuseme huyu baba ameshafikia umri wake sasa hivi na sisi ni rika nyingine tukishaelekea kwenye upande wa rika kuna dume ambalo tunachinjaga kulingana na watoto uliopata kumaanisha umekuwa mzee sasa ni kama dume la shukurani kwa jamii wote maana mtu kama huna watoto huwezi ukachinja hilo dume yani ni ile tu kwamba ni shukurani kutoka kwa watu na pia kuonekana na wewe umeshaingia kwenye lile group la watu wa rika kwahiyo ni shukurani unatoa kwa jamii nzima kwa kuchinja dume hilo la ng’ombe
I: Ni rika gani hiyo ambayo ukiingia lazima uchinje dume la ng’ombe namba moja tuelezea hapa?
R1: Yani inategemea na kundi kutolewa kwahiyo unaweza ukakaa tu ukiwa mtoto mdogo umekuwa kijana umetahiriwa bado huna mwanamke unavokuja umeoa umepata watoto wako sasa ukishaanza kuwa na watoto maana bila watoto huwezi kuchinja ile dume la ng’ombe ila kwa vile umepata watoto umepata mvulana, msichana sasa unaanza kuchinja yani inaonekana kabisa kihalisia lile dume nila shukrani na ukishamaliza ile sasa hapo umeshamaliza mambo ya vijana umekuwa mzee unaelekea kwenye kundi la wazee ushaachana na vijana na shukurani umeshatoa na vitu ulivyopata chini ya ardhi hivyo ndivyo ilivyokuwa inafanyika katika jamii yetu ya kimasai
I: Na bado kinatumika mpaka hivi sasa?
R1: Eeeeh kisu bado kinatumika sanasana kinakuwa ni kisu kwa ajili ya mzee na kama mzee ana nyumba yake ataenda kuweka kwake na kama ana mwanamke anamwamini anaweza akampa na anaweza akalaani hata isiguswe kabisa ndani ya boma mpaka yeye aruhusu iguswe au aje kuigusa mwenyewe hizi zote ni tamaduni, mila na desturi katika jamii yetu hii ya kimasai na lazima zizingatiwe
R3: Matumizi ni kuchinja ng’ombe ile ya rika ni baada ya kuwa mzee kwasababu siumekuwa mtoto ukawa morani, sasa unaonyesha sasa umekuwa mzee na una watoto wako huweki tena sehemu kwahiyo mtu kama amekuwa mzee ndiyo anachinja
I: Ndiyo anachinja?
R3: Eeeeh inaonyesha sasa kazi imeisha
I: Na hii Engalemu ilikuwa inatengenezwa kwa kutumia nini na nini namba tatu hebu tuambie hapo?
R3: Inatengenezwa kwa kutumia vijiti unaweka vijiti alafu unaweka hii chuma
R2: Unjaua hii hizo ni chuma za kizamani wanaojua hata mfupa ina haribu kabisa hiyo inatengeneza kutafuta hizo kitu inayoitwa tupa kutengeneza kabisa na kutengeneza vizuri na kutafuta hivi vijiti na kuweka vizuri
I: Hii njiti iliyokuwa inatumika ni njiti ya namna gani?
R2: Hiyo ni aina ya miti ya olitepesi mizizi yake ya ndani
I: Kwanini mzizi?
R2: Ndiyo ngumu haiwezi kupasuka unaweka olitepesi au osilale hii yote ni miti ambayo haipasuki
I: Kwahiyo ilikuwa ina umuhimu mkubwa sana kwenye jamii?
R2: Eeeh kwenye mila na desturi
I: Kwahiyo ni mzee au mke anayemwamini ndiyo anampa kuhifadhi hicho namba mbili hebu tueleze?
R2: Eeeeh kuhifadhi lakini siyo kutumia
I: Ni kwa ajili ya matumizi ya kuchinja tu?
R2: Kabisa hiyo tu katika boma lako lazima iwe nayo hii kisu
I: Kwahiyo kila boma lazima iwe nayo?
R2: Eeeh kisu ya mzee
chanzo: Amani-Stade Project / Massai Field Research 2023 / Interview No. 06
mwandishi: I: Mohamed Seif, R1, R2, R3: Anonymous
Mtu
-
National Institute for Medical Research (NIMR)
(Mteja)
-
unknown actor
(wissenschaftlicheR BearbeiterIn)
Mahali