Hinweis: Um die korrekte Darstellung der Seite zu erhalten, müssen Sie beim Drucken die Hintergrundgrafiken erlauben.
Slider Bild - CC BY-NC-ND 4.0
Slider Bild - CC BY-NC-ND 4.0
1/2

Mkufu

Sammlung Braun
r 2018 / 18426 c
Taasisi inayotoa
Museen Stade
Eneo la Mkusanyiko
Sammlung Braun
Nambari ya uvumbuzi
r 2018 / 18426 c
Kichwa
Mkufu
Vipimo
Urefu: 40cm
Fasihi
Merker, Moritz Masai, Ethnogr. Monographie e. ostafrikan. Semitenvolkes, 1910, GVK
Kiungo cha dondoo
https://www.amani-stade.gbv.de/item/sw_ms_8b5f6541-31bb-4dc2-90c4-800396196b97
nakala kwenye ubao wa kunakili
Kikundi cha kitu / kitu cha mtu binafsi
Kitu cha mtu binafsi
Uainishaji
Vito vya mwili na nguo (nguo za wanaume)  
Vito vya mwili na mavazi (Nguo za wanawake)  
Uzalishaji
Wakati
mpaka ca. 1906-05-30
Mtu
  • Person (Mtengenezaji)
Mahali
  • Tansania
Ethnolojia
  • Massai  
Kununua / Uuzaji
Wakati
1906-05-30
Maelezo
"Ijuma 30. Mwezi wa tano 1906 [kimepigwa mstari]jioni matembezi mafupi na Max. Ghafla tukakutana na mvua mkubwa. Kutoka kwa Wamasai wawili tukanunua: mapambo ya masikio yaliyotengenezwa na udongo mwekundu, yamepambwa na shanga chache ya kioo nyeupe na buluu. Angali shajara. 43 u. 104. Hadi sasa niliona vitu hivi [u.108] vya mbao tu (= hela 25.) Mkufu kama ulivyonunuliwa tayari u. 41 [...] (= 12 hela). Kutokana na kazi ya M. Merker. Die Masai (Berlin 1904) u. 346 mapambo haya yamepata jina kutokana na mtambaa unaotumika kuyatengenezahat ol mogou – gora „gome linalonukia vanila huunfanishwa lifanane na kamba halafu huvaliwe kama ukanda wa shingo (ol orowil) na wanaume & wanawake. Pia hutumika kama dawa ya siri ya ol oiboni na ol goiatiki.Jina la kisayansi halijulikani. Husemekana kupatikana kwenye misitu ya mito [?).“ [Utafsiri]

chanzo: Museum der Kulturen Basel, VI 56197, 46 (108)
mwandishi: Karl Braun
Mtu
  • Mtu, haijulikani (Mchuuzi)
  • Braun, Karl (* 1870 † 1935) (Mnunuzi)
    GND Explorer
  • unknown actor (Mshiriki)
Mahali
  • Amani
Malipo
Wakati
kutoka 1906-05-30
Maelezo
"38. Mkufu wa Massai, kutokana na mbao unaonukia vanila umepakwa udongo mwekundu/ Amani 30. mwezi wa kuminamoja. 1905 = hela 50 / TB. 46,41, 108, 52, 69. (20 mwezi wa isa. 1908) / M. Merker D. Masai (1904) u. 346 = ol mogou - gora [?] / mkufu = ol orowil [?]" [Utafsiri]

chanzo: Museen Stade, r 2018 / 18566
mwandishi: Karl Braun
Mtu
Nambari za hesabu za zamani
  • 38
Urithi
Wakati
1934-07-17
Maelezo
Mnamo mwaka 1934, aliyekuwa mkurugenzi wa Taasisi ya Biolojia ya Kilimo na Misitu (Biologische Reichsanstalt für Land- und Forstwirtschaft) Karl Braun (1870–1935) alitoa kile kinachoitwa “Kolonialsammlung Braun” (Makusanyo ya Mkoloni Braun) kwa Jiji la Hanseatic la Stade, au tuseme aliyekuwa mwakilishi wake, meya wa wakati huo Hans Arthur Meyer (1884–1961). Tazama faili „Uhamisho wa makusanyo ya kikoloni kutoka kwa diwani mkuu wa serikali Profesa Dk. Karl Braun huko katika Jiji la Stade” („Überlassung einer Kolonialsammlung vom Oberregierungsrat Professor Dr. Karl Braun in Stade an die Stadt Stade") katika Jimbo la Saxony ya Chini Hifadhi ya Nyalaka ya Stade (Niedersächsischen Landesarchiv Standort Stade).

chanzo: Niedersächsisches Landesarchiv Standort Stade, Dep. 10 Nr. 03025
Mtu
  • Braun, Karl (* 1870 † 1935) (Mfadhili)
    GND Explorer
  • Hansestadt Stade (Mpokeaji)
  • Hans Arthur Meyer (1884 - 1961) (Mpokeaji)
Mahali
  • Stade
Mkopo
Wakati
1997-02-17
Maelezo
Mnamo mwaka 1997, aliyekuwa mtunza kumbukumbu wa jiji kwa wakati huo Jürgen Bohmbach anahitimisha makubaliano ya makabidhiano kwa mkopo wa kudumu katika Jumba la Makumbusho (Museumsverein Stade e.V.) chini ya aliyekuwa mkurugenzi wa wakati huo Gerd Mettjes kwa kutia saini. Baadaye, makusanyiko kutoka kwa Karl Braun yalihamishiwa kwenye Jumba la Makumbusho (Museumsverein Stade e.V.) kwa ajili ya utunzaji.

chanzo: Museen Stade, Vereinbarung Leihgabe "Brauns'sche Kolonialsammlung"
Mtu
Mahali
  • Stade
Scientific use:
Wakati
2023-06-14
Maelezo
I: Sawasawa haya tunaendelea na picha nyingine hapa nina picha imesajiliwa kwa namba 2018_18426_C hebu angalia picha hii unaweza kutuambia hicho ni kitu gani? R: Haya ni makoja I: Makoja? R: Eeeeh yanaitwa makoja I: Makojaa ni kilugha gani hicho? R: Kisambaa I: Mnaita makoja? R: Eeeeeh I: Makoja? R: Eeeh yanavalishwa shingoni haya unavalishwa linazungushwa unavalishwa linazungushwa kama mara tatu hivi utakuwa unapendeza I: Wanavalishwa watu gani? R: Mara nyingi wanaotaka kuolewa I: Wa kike? R: Eeeeh wanawake makoja ya wanawake I: Wanawake? R: Eeeeeh I: Kuanzia umri gani? R: Kuanzia miaka 18 akipata mchumba akiozeshwa anatafutiwa makoja kwa ajili ya ndoa eeh na anavalishwa I: Kwahiyo inavaliwa wakati anataka kuolewa? R: Anataka kuolewa eeh I: Kipindi ambacho anawekwa ndani au wakati anatoka? R: Anawekwa ndani akitoka sasa kwenda kwa mume wake anavalishwa anapambwa anaenda kwake I: Ni wasambaa tu peke yake wanatumia makoja au na makabila mengine pia walikuwa wanatumia? R: Kwa ninavyoona makabila mengine pia yanatumia kwasababu wamasai wana shanga nyingi sana lakini msambaa hana nyingi sana yeye ana makoja eeh I: Kwahiyo msambaa ni makoja? R: Eeeeeh I: Lakini hiyo inaonekana ni kabla ya kupatikana kwa shanga au kipindi hiko shanga zilikuwepo hebu tuambie? R: Kipindi hiko shanga kulikuwa hakuna ni makoja tu I: Makoja tu? R: Eeeeeh I: Kwahiyo ni wasambaa na wamasai? R: Wasambaa, wazigua, wabondei walikuwa wanaendana mambo yao karibu yanafanana fanana mengi sana I: Wote walikuwa wanavaa? R: Eeeeh I: Na makabila haya yanapatikana sana mikoa gani? R: Mkoa wa Tanga I: Mkoa wa Tanga? R: Eeeeh I: Sawa unaweza ukafahamu mkoa wa tanga sehemu gani hasa yalikuwa yakivaliwa makoja tuelezee? R: Zamani kulikuwa kuna miviga huko mtu anaingizwa kwenye miviga akiwa anatoka kwenye miviga makoja yake anaozeshwa anaenda kwake yuko vizuri I: Sawa na ukilinganisha na sasa makoja yanaendelea kutumika au unadhani ikafika kipindi makoja? R: Wala hayajulikani kwanza I: Ndiyo R: Vitu vya zamani havipo kwanza saivi humkuti mtu ana mtoto anawekwa ndani sijui achezewe mviga hamna iliisha hiyo I: Iliisha? R: Eeeh saivi ni utandawazi I: Hahahahahha sasa hivi ni utandawazi? R: Eeeeh ni utandawazi I: Makoja yalikuwa yanavaliwa na watoto wa kike tu? R: Eeeeh wanawake has pale anapotaka kuolewa I: Kuolewa? R: Eeeeeh I: Kashawekwa ndani? R: Eeeeeh I: Na walikuwa wanawekwa muda gani ndani? R: Alikuwa anawekwa mwezi mmoja kadri ya uwezo wa wazazi maana kule kutengenezwa mtajiandaa wengine miezi miwili kadri ya uwezo wa wewe utakavo hudumia wale watu kwahiyo kila mtu itategemea uwezo wake I: Sawasawa kwahiyo sasa hivi makoja hayapo? R: Sasa hivi baba hayapo kwanza muda wa kuwekwa huko ndani uko wapi mtu akitokala kwanza la saba, form four, form six yuko wapi atakaye vikwa koja akaendani angoje koja hayupo I: Hakuna? R: Hapana I: Sawasawa kwahiyo sasa hivi wasambaa hawatumii tena makoja? R: Tena huo mviga unaweza ukae hata miaka 20 hujasikia mviga hakuna I: Mviga ni nini? R: Ndiyo hizo ngoma za mtoto wa kike I: Ambazo ndiyo zakuweka watu ndani? R: Eeeeh wanawake watoto wakike I: Mviga? R: Eeeeh mviga I: Kwahiyo hata saivi mviga hakuna? R: Hakuna I: Kwanini miviga hakuna tena hivi sasa? R: Watu wameendelea I: Wameendelea nini? Hahha R: Hahahhaha ya kale hayapo I: Hayapo ya kale? R: Hayapo I: Hhahahaha sawasawa na waliokuwa wanatengeneza makoja ni watu gani hasa wakati huo wa zamani? R: Ni wale akina mama eh I: Wakina mama kuanzia umri gani? R: Watu wazima wale ambao watawaweka ndani ndiyo wanachukua hizo shanga maana hayako duara yamekaa mabapa bapa ndiyo hayo wanayashona wanayafunga wanawavisha kipindi wanaolewa I: Walikuwa wanaotengeneza ni kuanzia miaka mingapi? R: Wakina mama watu wazima wale I: Kwasasa unaweza ukakadiria walikuwa wanaanza kutengeneza kuanzia miaka mingapi kama unakumbuka? R: Ilikuwa ni kuanzia miaka 45 na 50 I: Kwanini walikuwa watu wazima? R: Kwasababu watu wazima ndiyo wana hekima kwenye mtu mzima hapa haribiki neno hapana ngumi hapo I: Ndiyo hahaha R: Hhahahah I: Sawa sawa na unaweza kutuambia vitu vilivokuwa vinatumika kutengenezea makoja yanatengenezwa kwa kutumia kitu gani? R: Makoja I: Angalia vizuri unaweza ukatambua kwa kuangaliam picha yalikuwa yanatengenezwa kwa kutumia nini makoja? R: Haya mara nyingine yalikuwa ni vigongo hivi vizuri ambavyo vinarembwa vinakatwa katwa vinatobolewa vizuri vinapendeza I: Kwa maana ya miti? R: Eeeeh I: Vinatobolewa? R: Vinatobolewa vinashonwa, vinatungwa na unavaa I: Vilikuwa vinatungwa na nini? R: Yani vikikatwa katwa vizuri na kutobolewa njia basi unachukua kamba na kama yenyewe niya mti I: Kamba niya mti? R: Eeeh unachubua mti inakuwa vizuri unachomeka kwenye matundu anavishwa akitolewa hapo anakuwa kapendeza sana I: Ni mti gani hasa ulikuwa ukitumika kupata vitu vya kukatia mti kupata hivi vipande vidogo vidogo na kamba yake? R: Ni vya kamba kuna mti unaitwaje sosokole, sosokole una kamba I: Sosokole? R: Sosokole eeh unakamba ngumu hata kwa kujengea unajengea haukatiki kwasababu una Kamba mgumu sana I: Ndiyo R: Kwahiyo hiyo inachukuliwa inatungiwa wasichana wanavishwa kwenye shingo I: Na hadi kipindi ambacho zimepotea zilikua zinatengenezwa kwa kutumia hivyo hivyo miti pamoja na kamba za sosokole au ilifika wakati ikabadilishwa vitu ambavyo vya kutengenezea vikabadilika? R: Ndiyo sasa hivi vimebadilika ndiyo zipo hizo shanga sasa I: Shanga? R: Eeeeh sasa hivi hivyo havipo hizi ni shanga sasa vinaenda kimtandao hahahah I: Eeeeeh R: Viko kisayansi zaidi vimeboreshwa zaidi I: Ndiyo sawasawa kwahiyo saivi shanga? R: Ni shanga I: Labda umesema inaitwaje? R: Makoja I: Mkoja ukiletwa kwenye masoko ya sasa hivi unafikiri inaweza ikauzwa shilingi ngapi? R: Sasa nani atanunua mkoja wakati kuna shanga hahahahhaha I: Hhahahhahaha R: Labda uganga hahahhah I: Hahahahahah labda za uganga R: Eeeh uganga kama umeambiwa ukatafute koja ndiyo ukalitafute sasa lakini sasa ukute dukani linauzwa alafu unakuta vya ndani vimetengenezwa mishanga yafanya kumeremeta huwezi ukalichukua I: Huwezi ukalichukua

chanzo: Amani-Stade Project / Amani Field Research 2023, Interview No. 18
mwandishi: I: Mohamed Seif, R: Anonymous
Mtu
  • National Institute for Medical Research (NIMR) (Mteja)
  • unknown actor (wissenschaftlicheR BearbeiterIn)
Mahali
  • Amani
Scientific use:
Wakati
2023-09-15
Maelezo
I: Sawasawa asante sana sawa kuna picha nyingine hapa imesajiliwa kwa namba 2018_18426_C hebu iangalie? R1: Hii ni olimokongora I: Olimokongora maana yake ni nini? R1: Hii ni mzizi fulani unachimbwa unanukia vizuri hataunniitafuna na kama sasa hao wasichana wanaenda nyofoa wanaishonea kamba wanaiweka kwenye shingo anakuwa na harufu nzuri ina harufu nzuri kama hizi za hivi akipita unasikia harufu na hata wavulana sasa wanaitwa morani alafu njia nyingine ni dawa pia ukiwa na ngiri unatafuna inakwisha kabisa ngiri kwahiyo inatumika kama dawa pia I: Olimokongora kwahiyo hii ni kwa ajili ya wanawake tu? R1: Ni wote wavulana na wasichana I: Kuanzia umri gani? R1: Hawa vijana vijana kuanzia miaka 15, 20, 22 mwisho miaka 30 kutumia mtu anaachana nayo haitumii tena I: Kwahiyo kazi yake ni kwa ajili ya? R2: Harufu nzuri sana I: Na niiliigusa pia inanukia vizuri kweli hahahha R2: Eeeh hahaah kama inanukia vizuri ukija tutakuletea I: Sawasawa nani dawa kwa ajili ya ngiri pia? R2: Eeeeh dawa I: Kwa wanaume na wanawake? R2: Eeeeh ukitafuna hiyo ina saidia sana I: Kwahiyo wanavaa kuanzia miaka mingapi? R2: Wasichana kuanzia miaka 15 mpaka 20 wanakuwa washajua vitu vizuri wavulana kuanzia miaka 18 washajua vitu vizuri anavaa miaka 20 ikifika miaka 30 basi kwa wazee hapana hawataki na wakina mama wakubwa hawataki ni kama ile perfume ukipuliza puliza ukitoka siunanukia sasa na hii inakuwa na harufu nzuri inayovutia inayopendwa na vijana wengi kwahiyo wanaitumia sana vijana I: Kwahiyo inavaliwa shingoni? R1: Eeeh inavaliwa shingoni kama kawaida unatumbukiza shingoni huoni imeshonwa na kamba unavaa shingoni inaingia kabisa inakaa I: Kwahiyo huu ni mti? R1: Ni mti tena ipo mingi kwenye mlima huu ni mingi sana ukienda tu kuutafuta unaipata mingi sana I: Sawasawa na umuhimu wake ni huo kwa ajili ya kuvutia, kutoa harufu nzuri na wanaozitengeneza hizi ni akina nani sasa? R1: Wanaotengeneza yani hiyo inaletwa alafu inatengenezwa vijana siwanakwenda kuchukua wanatengenza wale wanaotumia I: Kwahiyo nikitaka kutumia mimi naenda porini? R1: Eeeh unaenda porini kama hizi mito zinazoshusha maji ni nyingi sana unanyofoa tu inachomoka hivi mzizi kama huu unaenda unakata I: Huo mti unaitwaje? R1: Ndiyo unaitwa olimokongora I: Olimokongora? R1: Eeeh unaikata hivi unaitoa unaiweka unaikata hivi I: Ina njia katikati? R1: Eeeh I: Olimokomgora lakini hii mnafahamu nyie tu wengine hawajui? R2: Hata wasambaa wanajua I: Wanavaa wasambaa? R2: Hawavai lakini ni dawa wanajua kama dawa I: Kwa wasambaa wanajua inatibu ngiri au wanajua kwa namna nyingine? R1: Wanaita ubombo I: Ubombo wanautumia kufanyia nini? R2: Yani ni dawa ya change inaaminika alafu asilimia kubwa walikuwa wanasema kama inaongeza nguvu R2: Nimekwambia ni dawa I: Aaaah ubombo Arusha, moshi wanaita nkongora R1: Eeeeeh I: Ndiyo hiyo? R1: Ndiyo hiyo I: Khaa basi naujua tena nimetoka juzi Mlalo kuna mama mmoja nilienda kununua dawa za asili akanipa R1: Nakwambia hivi hawa watu waliokuwa wanatoka juu huko kuja sokoni mbona wanaleta sana I: Sawasawa na mpaka sasa hivi jamii yenu wanatumia vijana kuvaa hii? R1: Mpaka sasa hivi lakini siyo wengi lakini wanavaa I: Sawasawa na huwa zinauzwa hizi au hata sokoni unaweza kuta kama hii imetengenezwa ikauzwa? R1: Hawatengenezi sokoni ni wewe mwenywe maana ikikauka siinapasuka wewe unachukua unaenda kutengeneza mwenyewe wiki moja unayo basi imeisha I: Kwahiyo inatumiwa kwa kipindi maalumu? R1: Ndiyo I: Baada ya wiki moja ikiisha unatengeneza nyingine? R1: Baada ya wiki kuisha inapasuka wale wa sokoni wanauza kwa ajili ya kutafuna mtu unamkuta anatafuna I: Cha ajabu unajua hii niliiona bado kiko hivihivi R2: Hii ipo hivohivo? I: Eeeeh R2: Ni dawa ya ngiri inasaidia sana I: Olimokongora aah mkongora hhahhaha sawasawa kwahiyo ni mti au ni kamba ya aina gani sasa hebu iangalie vizuri mzee [anonymous]? R1: Hii ni kamba tu ya kawaida ni kamba tu za porini wanasokota na kuzitumia katika kutengenezea

chanzo: Amani-Stade Project / Massai Field Research 2023 / Interview No. 01
mwandishi: I: Mohamed Seif, R1, R2: Anonymous
Mtu
  • National Institute for Medical Research (NIMR) (Mteja)
  • unknown actor (wissenschaftlicheR BearbeiterIn)
Mahali
  • Mnazi
Scientific use:
Wakati
2023-09-28
Maelezo
I: Nina picha nyingine hapa ambayo imesajiliwa kwa namba 2018_18426_C hebu mama [anonymous] shika hii hiyo inaitwaje ni nini hiyo? R1: Hii inaitwa Erureshi I: Maana yake ni nini orureshi? R1: Watu wanavaa kama urembo I: Wanavaa wapi? R1: Shingoni I: Erureshi? R1: Ina maana hii ni kama ushanga za sasa hivi lakini hii ni kama ushanga ambao niwa zamani sana I: Ilikuwa inatengenezwa kwa kutumia nini hii Erureshi mama [anonymous]? R1: Hii inaitwa engeene niyakutungia Erureshi I: Engeene ni kamba si ndiyo? R1: Eeeh ni kamba I: Alafu hivo vilivyotungwa ni vitu gani sasa? R1: Hii ni Erureshi I: Erureshi ni mti au ni nini? R1: Ina maana hii Erureshi lakini ya zamani kama miti gani I: Nataka kujua kama ni mti ni mti gani walikuwa wanatengenezea mama [anonymous] tuambiem kama unajua? R1: Hii ni ushanga lakini ushanga wake ni mti uliokuwa kwenye maji yani kama vile majani lakini siyo majani ni mizizi yake yani ndiyo yanaenda kutolewa yanakatwa katwa na yanatumika kutengenezea hiyo I: Unaitwaje huo mti? R1: Mkongoraa I: Mkongoraa naujua wanauza hata huko mjini haha! R1: Eeeeh I: Kwahiyo ndiyo unachukuliwa ule unakatwa katwa? R1: Eeeeh alafu unatobolewa ni ushanga wa zamani huoni ushanga wa sahivi siyo mweupe kama hiyo ya zamani I: Huu ndiyo ushanga wa zamani? R1: Eeeeh I: Walikuwa wanavaa watu gani wa kike au wakiume? R1: Yoyote anavaa kwasababu ni ushanga wa shingoni

chanzo: Amani-Stade Project / Massai Field Research 2023 / Interview No. 03
mwandishi: I: Mohamed Seif, R1, R2: Anonymous
Mtu
  • National Institute for Medical Research (NIMR) (Mteja)
  • unknown actor (wissenschaftlicheR BearbeiterIn)
Mahali
  • Mnazi
Scientific use:
Wakati
2023-09-29
Maelezo
I: Nina picha nyingine hapa ambayo imesajiliwa kwa namba 2018_18426_C hebu iangalieni na hiyo R2: Hii ni olimokongora hii zamani anashona na kamba ya ngozi ya mbuzi siunaona hii eeh hata hii ni olimokongora I: Olimokongora? R2: Eeeh I: Ulisema niya vijana? R2: Eeeh I: Vijana wakuanzia miaka mingapi? R2: Hata miaka 20, 30 na kuendelea I: Kwanini imeshona na ngozi ya mbuzi? R2: Sasa si kale hiyo sasa hii hawa ambao wanashona hivyo hata sisi hatujazaliwa niya kale hiyo wote hapa tulikuwa hatujazaliwa I: Ndiyo uzi ulikuwa unapatikana kirahisi huo wa ngozi ya mbuzi? R2: Alafu muda mwingine anakwenda kutafuta kamba ya miti anakuja kusuka na mguu mpaka anamaliza I: Olimokongoraa? R2: Eeeh!

chanzo: Amani-Stade Project / Massai Field Research 2023 / Interview No. 05
mwandishi: I: Mohamed Seif, R1-3: Anonymous
Mtu
  • National Institute for Medical Research (NIMR) (Mteja)
  • unknown actor (wissenschaftlicheR BearbeiterIn)
Mahali
  • Mnazi
Scientific use:
Wakati
2023-10-04
Maelezo
I: Nina picha nyingine hapa imesajiliwa kwa namba 2018_18426_C na hii ni hiyo hiyo olikeria au hii ni nyingine hiyo inaitwa? R3: Engonongoi I: Maana yake ni nini engonongoi? R3: Engonongoi ni ushanga ambao mzee, mtoto akipelekwa jando baba yake yule binti ana mtoto wa kiume anavaa kichwani kuonyesha kwamba huyu mzee amemtahiri kijana wake alafu anakaa kwa muda akishafikia siku chache iliyopita anakuja anatoa kichwani mzee anaenda anamvalisha yule kijana wake na kijana anavaa shingoni anakaa akishamaliza kwamba anatolewa kwenye stage ya esipolio anapelekwa kwa morani sasa mzee anachukua anavaa yeye kwahiyo hakuna sheria yoyote ya jando kwa mzee ambayo haitumii hiyo engonongoi na kilichotumiwa ni emboronoti ya kondoo I: Ngozi ya kondoo? R3: Eeeeh I: Kwahiyo engonongoi ndiyo hivi vidude vidogo vidogo? R3: Eeeeh I: Ni mti? R1: Siyo mti ni ushanga mweusi ambao umetobolewa katikati unakuja kushona ndiyo hizi nyeusi nyeusi ambazo zimeshonwa I: Nataka kujua hivi maana ni tofauti na ushanga ninaoujua ni vitu gani hivyo namba moja hebu tuambie? R1: Ndiyo hiyo tunasema ni ushanga lakini ushanga ambao umetobolewa katikati mfano anaweza toa ushanga kama hivi unapasuliwa katikati lakini hii inaitwa engonongoi ukienda kufafuta dukani hakuna engonongoi nyekundu ni nyeusi ambayo haitafanya kazi yoyote bila engonongoi kwasababu siku ambayo wanaenda kutahiriwa watoto wako baba anavaa shingoni lazima aandae maji ya kufua yule kijana ambaye amekuja kutahiriwa baadae anatafuta hii engonongoi hata kama hamna anaenda sehemu ambayo ipo mbali kuomba baba wengine naomba engonongoi itakayonifaa maana naenda kutahiri watoto wangu sina engonongoi ya kuvaa kichwani siku ambayo anarudisha kama siyo ya yule baba unaweza kununua sukari unanunua majani atamrudishia huyo baba engonongoi kwasababu ya heshima kwa yule ambaye alimpatia engonongoi R4: Ni kitu cha maana sana I: Napenda kufahamu tumeona kwenye hii iliyoisha ya olikeiani ni mti? R1: Ni mti ambao hata huyu nakaa nae sasa hivi yeye mwenyewe anajua sehemu unaota anatoka hapa namanga kwenda sinya kwenda kukata olikeria anaikata olikeria anaifunga anakuja na gari ila je kushonea na kutengeneza esoso kuelezea hizi ambazo anaona kila kitu wamasai wanafanya safari ya kwenda sehemu kama sinya lakini yeye mwenyewe au huyu yeye anajua sehemu ambayo inaota olikeria inaota kama majani kwahiyo anaenda kuchukua huko ambapo inaota anakuja nayo I: Na engonongoi pia imetoka kwenye mti? R1: Hapana engonongoi inatokana na ushanga ndani ya ushanga mtu ambaye anatengeneza engonongoi anatengeneza ushanga kwasababu ni ushanga pia kwenda kuangalia ukishika hivi kama mawe ushanga lakini anakuja kutoboa katikati maana siyo ndogo kama ushanga ni nyembamba hivi lakini anapasua katikati lakini hakuna engonongoi nyekundu hakuna engonongoi nyeupe hakuna engonongoi nyeusi I: Na wanaotengeneza engonongoi ni kina mama pia? R1: Mshonaji au mtemngenezaji mpaka aende kununua anaenda kununua duka la ushanga anaweza akawa ni baba ananunua alafu anakuja kumletea mama na mama ndiyo mwenye jukumu hilo la kushona mpaka ikamilike wa baba wao hawashoni kazi yao kubwa ni kununua tu na kumpa mama ashone

chanzo: Amani-Stade Project / Massai Field Research 2023 / Interview No. 10
mwandishi: I: Mohamed Seif, R1-3: Anonymous
Mtu
  • National Institute for Medical Research (NIMR) (Mteja)
  • unknown actor (wissenschaftlicheR BearbeiterIn)
Mahali
  • Kimokouwa
Mwandishi: Karl Braun, Tarehe ya kutengenezwa: 1906-05-30, Nukuu/Angalizo: Museum der Kulturen Basel, VI 56197, 46 (108)jifunze zaidi
Mwandishi: Karl Braun, Nukuu/Angalizo: Museen Stade, r 2018 / 18566jifunze zaidi

Rejeo la ndani la kitu

Bangili

Bangili

r 2018 / 18407
Rejeo la ndani la kitu
Kuhusiana na
Mkufu wa vipande vitatu

Mkufu wa vipande vitatu

r 2018 / 18426 b
Rejeo la ndani la kitu
Kitu kinacholingana
Shanga ya mkufu wa mbao na kishaufu

Shanga ya mkufu wa mbao na kishaufu

r 2018 / 18426 a
Rejeo la ndani la kitu
Kitu kinacholingana
Mkufu

Mkufu

r 2018 / 18426 d
Rejeo la ndani la kitu
Kitu kinacholingana
Asili ya data ya kitu
Museen Stade
Leseni
Creative Commons Namensnennung, nicht kommerziell, keine Bearbeitung 4.0jifunze zaidi
Imepitishwa katika lango imewashwa
2025-12-04T14:59:15+01:00

Rekodi zetu za takwimu zinafanyiwa maboresho kila mara. Tafadhali wasiliana nasi ikiwa una maswali au maoni au ikiwa unahitaji taarifa zaidi au nyingine zinazohusu mali hii. Taarifa juu ya ulinzi wa takwimu.
Rudi kwenye utafutaji