Hinweis: Um die korrekte Darstellung der Seite zu erhalten, müssen Sie beim Drucken die Hintergrundgrafiken erlauben.
Slider Bild - CC BY-NC-ND 4.0
Slider Bild - CC BY-NC-ND 4.0
1/2

Bangili

Sammlung Braun
r 2018 / 18443
Taasisi inayotoa
Museen Stade
Eneo la Mkusanyiko
Sammlung Braun
Nambari ya uvumbuzi
r 2018 / 18443
Kichwa
Bangili
Vipimo
Kipenyo: 6,5cm
Nyenzo
Chuma
Fasihi
Baumann, Oscar Usambara und seine Nachbargebiete, allgemeine Darstellung des nordöstlichen Deutsch-Ostafrika und seiner Bewohner ; auf Grund einer im Auftrage der Deutsch-Ostafrikanischen Gesellschaft im Jahre 1890 ausgeführten Reise, 1891, GVK
Kiungo cha dondoo
https://www.amani-stade.gbv.de/item/sw_ms_fcc60c24-22cf-44a7-a156-3081ec314474
nakala kwenye ubao wa kunakili
Kikundi cha kitu / kitu cha mtu binafsi
Kitu cha mtu binafsi
Uainishaji
vito vya kikabila  
Uzalishaji
Wakati
mpaka 1904-11-13
Mtu
  • Person (Mtengenezaji)
Ethnolojia
  • Swahili  
Kununua / Uuzaji
Wakati
1904-11-13
Maelezo
„Jumapili 13. Mwezi wa kumi na moja 1904 [imepigwa mstari] [...] hivi karibuni nimepata mapambo ya mikono: 1. Bangili ya Schenzi [Schenzi = Suaheli], nimeikuta kijijini ni kuukuu na mg‘ao, [mchoro] 2. Bangili ya kuvaliwa mkononi kwa juu [masahihishao: bangili, bangili ya paja] waya wa shaba (kamba ya utumbo iliyozungushwa waya zimeletwa kutoka Bondei na huitwa "dodi" [masahihisho Madodi ] kwa Wa Schenzi na "Talli" kwa Kiswahili). Zawadi kutoka kwa Bwana Krockenberger pale Derema [mchoro] 3. bangili,kibanda kinene cha shaba kilichozungushwa kimenunuliwa kwa Rupie 1 kutoka kwa Mswahili inaitwa „Talli“ . Kwa ufahamu wangu mimi Waswahili wanaita utepe wa waya Madodi au Dodi na bangili ya shaba nzito huitwa Talli (Baumann, O. Usambara. Berlin 1891. u. 31) [mchoro] [...]" [Utafsiri]

chanzo: Museum der Kulturen Basel, VI 56197, 43 (95)
mwandishi: Karl Braun
Mtu
  • Mtu, haijulikani (Mchuuzi)
  • Braun, Karl (* 1870 † 1935) (Mnunuzi)
    GND Explorer
Mahali
  • Amani
Malipo
Wakati
kutoka 1904-11-13
Maelezo
"3. Bangili "talli" iliyonunuliwa: Amani 13.11.1904 = 1 Rp. (Baumann, O. Usambara. Berlin 1891) [mchoro]" [Utafsiri]

chanzo: Museen Stade, r 2018 / 18566
mwandishi: Karl Braun
Mtu
Nambari za hesabu za zamani
  • 3
Urithi
Wakati
1934-07-17
Maelezo
Mnamo mwaka 1934, aliyekuwa mkurugenzi wa Taasisi ya Biolojia ya Kilimo na Misitu (Biologische Reichsanstalt für Land- und Forstwirtschaft) Karl Braun (1870–1935) alitoa kile kinachoitwa “Kolonialsammlung Braun” (Makusanyo ya Mkoloni Braun) kwa Jiji la Hanseatic la Stade, au tuseme aliyekuwa mwakilishi wake, meya wa wakati huo Hans Arthur Meyer (1884–1961). Tazama faili „Uhamisho wa makusanyo ya kikoloni kutoka kwa diwani mkuu wa serikali Profesa Dk. Karl Braun huko katika Jiji la Stade” („Überlassung einer Kolonialsammlung vom Oberregierungsrat Professor Dr. Karl Braun in Stade an die Stadt Stade") katika Jimbo la Saxony ya Chini Hifadhi ya Nyalaka ya Stade (Niedersächsischen Landesarchiv Standort Stade).

chanzo: Niedersächsisches Landesarchiv Standort Stade, Dep. 10 Nr. 03025
Mtu
  • Braun, Karl (* 1870 † 1935) (Mfadhili)
    GND Explorer
  • Hansestadt Stade (Mpokeaji)
  • Hans Arthur Meyer (1884 - 1961) (Mpokeaji)
Mahali
  • Stade
Mkopo
Wakati
1997-02-17
Maelezo
Mnamo mwaka 1997, aliyekuwa mtunza kumbukumbu wa jiji kwa wakati huo Jürgen Bohmbach anahitimisha makubaliano ya makabidhiano kwa mkopo wa kudumu katika Jumba la Makumbusho (Museumsverein Stade e.V.) chini ya aliyekuwa mkurugenzi wa wakati huo Gerd Mettjes kwa kutia saini. Baadaye, makusanyiko kutoka kwa Karl Braun yalihamishiwa kwenye Jumba la Makumbusho (Museumsverein Stade e.V.) kwa ajili ya utunzaji.

chanzo: Museen Stade, Vereinbarung Leihgabe "Brauns'sche Kolonialsammlung"
Mtu
  • Hansestadt Stade (Mkopeshaji)
  • Museum Schwedenspeicher (Mkopaji)
    GND Explorer
  • Bohmbach, Jürgen (* 1944) (Mkopeshaji)
    GND Explorer
  • Gerd Mettjes (Mkopaji)
Mahali
  • Stade
Scientific use:
Wakati
2023-06-19
Maelezo
I: hata ukiwa unaenda kwa mzee [anonymous] unaziona nyingi sana upande huu wa kushoto...sawa sasa tumemaliza picha zetu za postcard na sasa tunaenda kwenye picha za vifaa, na mkononi mwangu hapa nina picha ya kifaa ambayo imsajiliwa kwa namba 2018_18443_1, hebu angalia unweza ukafahamu ni kitu gani hiki R: hiki kifaa kinaonekana ni ring ya shaba ambayo tamaduni za ujana wa zamani watu walikuw wanavaa ring mkononi, kwa hiyo hii ni ring ya shaba ambayo ilikuwa inavaliwa I: unaweza ukatuambia kama ilikuwa na jina maalum kulingana na makabila ambao uliona wakitumia ring hiyo R: ndio, wenyewe walikuwa wanaita 'nanga' I: hicho ni kiliugha gani R: hiyo ni lugha ya kiswhili, kwamba hii walikuwa wanaona vijana kwamba akivaa hii akikorofishana na mtu akimpiga roba ya kabari, kw hiyo hii inachukua kama sehemu ya silaha inamsaidia kumbana vizuri huyo mtu I: na kwa makabila ambyo unayafahamu yalikuwa yakitumia hiyo unaweza ukatutajia makabila matatu hivi R: hii ilikuwa ni kama culture fulani inaenea kwa makabila yote kwa hiyo wasambaa wa huku walikuwa wanatumia, wanyamwezi walikuwa wanatumia na makabila na wasukuma, mpaka leo hii ukiwaangalia wasukuma bado wanavaa, wajaluo bado wanavaa, ukieda sehemu za huko bara utaona watu wengi bado wanava hizo ring mikononi I: labda kw wasambaa ilikuwa inajulikana kwa hilo la 'nanga' R: ee walikuwa wanajua, hilo jina nililokutajia ni la wasambaa wanaita 'nangaa' I: maana yake R: maana yake hii shaba ndio jina lake kisambaa I: na ikishatengenezwa bangili sasa nanga inaitwaje R: bado wanaita vile vile I: hivyo hivyo nanga R: ee I: na kitu hiki kilikuwa kinapatikana mikoa gani hasa R: hizi shaba hakuna mtu anaitafuta hii shaba isipokuwa vifaa kama vile nyaya za zamani zilizokuwa zikitengenezwa zlikuwa zinatengenezwa kwa shaba, hata nyaya za umeme mabakuli, sufuria zilitengenezwa kwa shaba, kwa hiyo kulikuwa na mafundi mchungo ambao wanagonga na kutengeneza kubadilisha uelekeo wa kifaa kilichokuja na kutengeneza kitu kingine R: kwa hiyo nanga ilikuwa inatumika mikoa gani hasa R: tusemem ni tanzania nzima, kwa sababu zamani kulikuwa na masufuria ya shaba, mabirika ya shaba na vitu vingi vya shaba, kwa hiyo kikishachakaa jamaa wanavigongwa wanatengeneza kitu kingine kama kile cha kuvaa I: na kipndi cha ukoloni sufuria ya shaba ilikuwepo R: ndio yalikuwepo, na ndio hao walieneza sana kwa sababu nadhani aluminium ilikuwa haifahamiki zaidi ndio maana walikuwa wanatumia shaba, kwa kuwa wenyeji wlikuwa wanatumia sana vyungu vya kienyeji, na hii shaba uaniona jinsi ilivyokuwa imepungua, zamani haya masufuria ya shaba haya ukipika mboga huwezi kuweka limau, ukiweka limau inakuwa chungu, shaba huwezi ukaweka limau, ukiweka limaua inakuwa chungu kabisa kama shubili I: kwa nini R: nafikiria kuna asidi fulani ambayo haielewani na ile shaba, na ndio maana hii inachakaa hivi, inamaana labda katika kijipaka mafuta au nini ndio maana ikabadilika badilika hivi I: na waliokuwa wakivaa nanga kwa kipindi hicho walikuwa ni watu jinsia gani R: ni wanaume I: kuanzia umri gani R: ni vijana tu, anavaa bangili moja tu I: nadhani nanga kwa sasa bado inaendele kutumika au itafika wakati itakuwa haina thamani tena kwa vijana R: kutokana na miaka jinsi ilivyokwenda watu wamebadilisha kwa sababu siku hizi kuna tamaduni za aina nyingi, ukifika sehemu za bara utakuta bado kuna watu wanavaa, hata humu bado kuna wachache ambao wanavaajapokwa sio nene kama hili, maana hili ni zito sio nene kama hili lakini wanavaa, kwa mfano mifano ya hiyo nanga bado upo ukifika kwa wamasai utakuta wao bado wnavaa bangili za shaba japokuwa zimebadilishwa dizaini sio kama hivi bado wanavaa, wasukuma bado wanavaa na wasukuma wameboresha zaidi sasa hivi wanazaa hata mipira fulani mieupe wanakatakata waniunga wanavaa, kwa maana hiyo hii bado inatumika I: na ili mtu atumie nanga kuna kitu kingine ambacho walikuwa wanapaswa kuwa nacho sambamba, yani anakivaa pamoja na nanga R: hapana, ile ni kwa ajili ya ujana ujana tu, mtu anaona kwamba nikivaa hiki nitakuwa smart zaidi nitapendwa basi... wote: wanacheka I: kupendwa na akina nani R: yani badala ya kuvaa saa anapata kitu ambacho kinamshughulisha mkononi I: na ilikuwa ina umuhimu gani katika tamaduni za watu uliowataja R: ni mapambo tu, hakuna kitu kingine zaidi ya mapambo I: ni watu wa jinsia gani waliokuwa wakitengeneza nanga kipindi hicho R: watu waliokuwa waktengeneza ni mafundi mchundo, nikisema mafundi mchundo sijui kiswahili kimeelekea maana mimi ni mswahili zaidi, ni hawa mafundi ambao wanatengeneza hata masufuria, ndoo na nini, ndio hao zamani walikuwa wataalam wakutengeneza vitu kama hivyo, ukikiangalia vizuri kwa mtu akikiangalia ambye hakuona hivyo vitu vya zamani hawezi kugundua kwamba hiki ni nini, lakini kwa mimi kwa sababu niliona napata idea hiyo I: walikuwa ni wakike au wa kiume waliokuwa wakitengeneza R: wakiume, nafikiria hata mimi ndani nikitafuta vizuri nitakuta ya babu yangu ninayo I: sasa babu kama utaweza kuiona itakuwa ni vizuri zaidi R: ngoja nitaitafuta I: ni wa umri gani hasa walikuwa wakitengeneza R: hii haina umri, zamani vijana walisifika kwa uhodari wa kutengeneza zana mbalimbali kwa maana hiyo kila aliyejifunza aliweza kutengeneza I: na kwa sasa katika maeneo tunayoishi hapa amani kuna mtu anayetengeneza vitu kama hivyo R: hapana, kwa sababu sasa ukikuta watu wamevaa ring kama hizi sio ring tena ni vitu vimedariziwa kwa ushanga aidha chata ya simba au ya yanga ndio watu wanavaa I: sawa, hapo ndio tumeweza kutambua kwamba ni shaba ndio ilikuwa inatumika kutengeneza hiyo, kwa ya kadiri miaka inavyozidi kwenda na kubadilika, nyenzo zilizokuwa znatumika kutengenezea nanga zilikuwa zikibadilika pia au ziliendelea kuwa shaba mpaka leo R: nyenzo zimebadilika baada ya kutokea vitu kama vile almunium, lakini hii ya babu yang ninayoizungumzia bado ni ya shaba hivi hivi, ina uhalisia huu huu lakini itabidi niitafute maana ina miaka mingi sana I: na ukingalia nanga hiyo na uhodari ilivyonakshiwa, ikiletwa katika sokola leo inaweza ikauzwa shilingi ngapi R: sidhani kwa sababu anayenunua lazima ajue kwamba hiki kitu ninakinunua kwa faida fulani na thamani fulani, ila sasa hivi ukimpelekea mtu anaweza akatengeneza heleni badala ya kutengeneza nanga tena kwa sababu nanga tena hazivaliwi, inaonekana shaba iliyokuwa inatumika hapo zamani ni ile shaba nzuri I: kwa mantiki hiyo shaba hiyo tuchukulie tunauza material, kwa shaba hiyo inaweza ikauzwa shilingi ngapi R: itaweza ikawa na thamani kama ya shilingi hela za kitanzania kama labda kwenye elfu 50 I: kwa sababu gani umetoa thamani hiyo R: hii ni nzito, ni shaba nzito nene, kwa maana hiyo kama ukikata vipande na kudizaini vitu vingine vidogo vidogo inatoa vitu vingi sana kama vile heleni, mikufu inaweza ikatoa vitu vingi sana

chanzo: Amani-Stade Project / Amani Field Research 2023, Interview No. 25
mwandishi: I: Mohamed Seif, R: Anonymous
Mtu
  • National Institute for Medical Research (NIMR) (Mteja)
  • unknown actor (wissenschaftlicheR BearbeiterIn)
Mahali
  • Amani
Mwandishi: Karl Braun, Tarehe ya kutengenezwa: 1904-11-13, Nukuu/Angalizo: Museum der Kulturen Basel, VI 56197, 43 (95)jifunze zaidi
Mwandishi: Karl Braun, Nukuu/Angalizo: Museen Stade, r 2018 / 18566 (3)jifunze zaidi

Rejeo la ndani la kitu

Bangili

Bangili

r 2018 / 18230
Rejeo la ndani la kitu
Mazingira/Muktadha wa upataji/Upatikanaji
Bangili

Bangili

r 2018 / 18479
Rejeo la ndani la kitu
Mazingira/Muktadha wa upataji/Upatikanaji
Asili ya data ya kitu
Museen Stade
Leseni
Creative Commons Namensnennung, nicht kommerziell, keine Bearbeitung 4.0jifunze zaidi
Imepitishwa katika lango imewashwa
2025-12-04T15:33:22+01:00

Rekodi zetu za takwimu zinafanyiwa maboresho kila mara. Tafadhali wasiliana nasi ikiwa una maswali au maoni au ikiwa unahitaji taarifa zaidi au nyingine zinazohusu mali hii. Taarifa juu ya ulinzi wa takwimu.
Rudi kwenye utafutaji