Hinweis: Um die korrekte Darstellung der Seite zu erhalten, müssen Sie beim Drucken die Hintergrundgrafiken erlauben.
Slider Bild - CC BY-NC-ND 4.0
Slider Bild - CC BY-NC-ND 4.0
1/2

Kizibao cha Violett kilichotariziwa

Sammlung Braun
r 2018 / 18384
Taasisi inayotoa
Museen Stade
Eneo la Mkusanyiko
Sammlung Braun
Nambari ya uvumbuzi
r 2018 / 18384
Kichwa
Kizibao cha Violett kilichotariziwa
Nyenzo
Nguo
Fasihi
Stuhlmann, Franz , Stern, R. Handwerk und Industrie in Ostafrika, Kulturgeschichtl. Betracht. ; Nebst e. Anh. Die Gewinnung des Eisens bei den -Nymwezi, Abhandlungen des Hamburgischen Kolonialinstituts, 1910, GVK
Stuhlmann, Franz , Stern, R. Handwerk und Industrie in Ostafrika, Kulturgeschichtl. Betracht. ; Nebst e. Anh. Die Gewinnung des Eisens bei den -Nymwezi, Abhandlungen des Hamburgischen Kolonialinstituts, 1910, GVK
Kiungo cha dondoo
https://www.amani-stade.gbv.de/item/sw_ms_0724b2ea-aef4-4662-9810-74c7ddb336c9
nakala kwenye ubao wa kunakili
Kikundi cha kitu / kitu cha mtu binafsi
Kitu cha mtu binafsi
Uainishaji
Nguo/Vitambaa  
Uzalishaji
Wakati
mpaka ca. 1908-08-30
Mtu
  • Mtu, haijulikani (Mtengenezaji)
Kununua / Uuzaji
Wakati
1908-08-30
Maelezo
„Jumapili 30. 1908 [imepigwa mstari] asubuhi nimemaliza kutengeneza kibweta cha Whisky kutoka Lehradous kwa ajili ya Ary. – nimeandika barua. – nimepokea "Kikoi" kimoja yaani kitambaa cha kiunoni cha Suaheli kitambaa nyeupe cha pamba chenye upinde wenye rangi mbalimbali Rangi za upinde: manjano, mwekundu, mweusi. Pia kuna nyekundu iliyokolea, kijani nk. angalia. Stuhlmann, Plandei [?] kuhusu ostafrikanische Baumwolle [u.60] "Der Pflanzer" III, S. 225. Nimekinunua kwenye duka la Muhindi [duka]. Mara zote vikoi viwili vimeunganishwa, kimoja ni 1 ½ rupie. Pia nimepata kwa Almeida & Minezas sketi kama zilizokuwa zinavaliwa na wajumbe na Akida zamani ila sasa imepitwa na wakati na inafanana na sare ya kihungaria Inatoka Uarabuni na haikushonwa vizuri hata kidogo 1 rp. 50 kwa kila moja. Hutengenezwa na washonaji wa Waswahili & kwa kutumia vitambaa kutoka ulaya [mchoro na mwaandiko] Kisibao = kisibao vyenye rangi tofauti tofauti. / – Leo msafara mkubwa umewasili Dr Junghaus na mke wake na Paul Rohrbach, mkufunzi wa maswala ya ukoloni." [Utafsiri]

1,5 Rupien

chanzo: Museum der Kulturen Basel, VI 56197, 52 (60)
mwandishi: Karl Braun
Mtu
  • Braun, Karl (* 1870 † 1935) (Mnunuzi)
    GND Explorer
  • Mtu, haijulikani (Mchuuzi)
Mahali
  • Amani
Malipo
Wakati
ca. 1908-08-30 - 1908-08-30
Maelezo
"98. Kisibao [?], kisibao cha Boy-bila, kina asilia ya kiarabu rangi mbalimbali / Amani 30 Augusmwezi wa nane 1908 = 1.50 / T.B. 52,60 / kimenunuliwa kwenye duka la wahindi. / Stuhlmann, F. Handwerk & Industrie in Ostafrika. 1910. u.116. / [mchoro]" [Utafsiri]

chanzo: Museen Satde, r 2018 / 18566
mwandishi: Karl Braun
Mtu
Nambari za hesabu za zamani
  • 098
Urithi
Wakati
1934-07-17
Maelezo
Mnamo mwaka 1934, aliyekuwa mkurugenzi wa Taasisi ya Biolojia ya Kilimo na Misitu (Biologische Reichsanstalt für Land- und Forstwirtschaft) Karl Braun (1870–1935) alitoa kile kinachoitwa “Kolonialsammlung Braun” (Makusanyo ya Mkoloni Braun) kwa Jiji la Hanseatic la Stade, au tuseme aliyekuwa mwakilishi wake, meya wa wakati huo Hans Arthur Meyer (1884–1961). Tazama faili „Uhamisho wa makusanyo ya kikoloni kutoka kwa diwani mkuu wa serikali Profesa Dk. Karl Braun huko katika Jiji la Stade” („Überlassung einer Kolonialsammlung vom Oberregierungsrat Professor Dr. Karl Braun in Stade an die Stadt Stade") katika Jimbo la Saxony ya Chini Hifadhi ya Nyalaka ya Stade (Niedersächsischen Landesarchiv Standort Stade).

chanzo: Niedersächsisches Landesarchiv Standort Stade, Dep. 10 Nr. 03025
Mtu
  • Braun, Karl (* 1870 † 1935) (Mfadhili)
    GND Explorer
  • Hansestadt Stade (Mpokeaji)
  • Hans Arthur Meyer (1884 - 1961) (Mpokeaji)
Mahali
  • Stade
Mkopo
Wakati
1997-02-17
Maelezo
Mnamo mwaka 1997, aliyekuwa mtunza kumbukumbu wa jiji kwa wakati huo Jürgen Bohmbach anahitimisha makubaliano ya makabidhiano kwa mkopo wa kudumu katika Jumba la Makumbusho (Museumsverein Stade e.V.) chini ya aliyekuwa mkurugenzi wa wakati huo Gerd Mettjes kwa kutia saini. Baadaye, makusanyiko kutoka kwa Karl Braun yalihamishiwa kwenye Jumba la Makumbusho (Museumsverein Stade e.V.) kwa ajili ya utunzaji.

chanzo: Museen Stade, Vereinbarung Leihgabe "Brauns'sche Kolonialsammlung"
Mtu
Mahali
  • Stade
Scientific use:
Wakati
2023-06-09
Maelezo
I: Sawa nina picha nyingine hapa imesajiliwa kwa namba 2018_18384 hebu angalia unaweza ukatambua kitu gani hicho? R: Huu kama ni mmea Fulani hivi I: Angalia vizuri R: Hii ni nguo ambayo imeshonwa mtindo wa choniline lakini ina maua yakufuma I: Inaitwaje nguo hiyo tuambie inaitwaje labda? R: Hii nguo ni nguo za kifalme hizi lakini sasa nilikua niseme kizibao jamii ya kizibao I: Jamii ya kizibao? R: Eeeeh I: Saa hiyo ni jamii ya kizibao kweli ambayo imenakishiwa na unaweza ukajua ni watu wa tamaduni gani walikuwa wakivaa visibao vya namna hiyo R: Hizi ni nguo za machief bwana I: Eeeh R: Hizi ni nguo za mtu mkubwa Chief I: Machief? R: Eeeeh I: Ndiyo walikuwa wakivaa R: Eeeh I: Machief wa makabila gani? R: Wazumbe wale wakilindi, na wafalme wakizungu kwenye hii miaka ya karibuni walipata nguo kama hizi ni watu wakubwa siyo mtu mdogo kwenye familia I: Kuvaa nguo kama hizo ? R: Eeeh I: Ukizungumzia wakilindi unazungumzia akina nani? R: Lakini bahati kama ungekuwa upo huo mimi nigekuwa ni zumbe sasa hivi kwasababu nina asili nayo hahhahhahha I: Haahhhahhaha mtawala? R: Eeeeh I: Kwahiyo ni nguo walizokuwa wanavaa watu wenye nafasi za juu? R: Eeeeh watu wenye nafasi za juu I: Nafasi ya juu R: Kwenye jamii eeh I: Na labda nguo hizo zilikuwa zinatoka wapi hasa? R: Hizi nguo zinatoka nchi za ulaya I: Kama nchi gani unaweza ukataja nchi? R: Sisi walikuwa wanaleta wajerumani, waingereza eeh hao waholanzi na wajerumani na waingereza ndiyo walibana hizo nafasi sana kwa Africa I: Na kilikuwa kinatumikaje unaweza ukatuambia? R: Hiki alikuwa anavaa siku maalum anapokutana na watu wake kuonyesha tofauti ya yeye na wao eeh hata ukitokea unajua kwamba yupo hapa ee I: Na kulikua na tofauti na anayevaa kulingana na umri na jinsia labda ni watu gani hasa wa kike au wa kiume wa umri gani walikuwa wakivaa nguo kama hizo? R: Bahati nzuri kwa waafrika kwa kipindi hicho walikuwa machief wengi ni wanaume kwahyo hizo walikuwa wanavaa wanaume wenye umri wa juu kidogo ili kuonyesha nafasi katika utawala wao I: Kuanzia miaka mingapi hivi? R: Kuanzia miaka sitini tuseme hamsini kwenda juu I: Sawasawa unadhani ukiangalia kizibao hicho bado kinaendelea kutumika katika mazingira yetu ya sasa au kimeshapoteza nafasi yake katika jamii zetu? R: Kwa muundo huu hakipo kwasababu bado ni vazi la heshima bado eeh saivi hakipo kuna nguo zinafanana fanana lakini havipo rasimi I: Sawasawa na unadhani kwasababu gani imepelekea isiwepo kwa wakati kama huu? R: Ni wakati tu sijui nisemeje nimpito au tuseme ni nini hazipo kwasababu kwanza tunaasili ya kuuza mambo ya kale kwahiyo hakuna anayeweza kuvaa nguo kma hii sasa hivi akaonekana kwenye jamii kwamba amevaa nguo nzuri I: Mhhh R: Eeeeh kwahiyo usasa umesababisha sana kupoteza vitu kama hivi I: Na aliyekuwa anavaa kizibao cha namna hiyo kuna mavazi mengine anatakiwa kuvaa au kilikuwa kinavaliwa tu chenyewe? R: Hii lazima avae na kanzu na joho moja kali sana alafu na kilemba kimoja kinakaa hapa inakuwa nzuri sana I: Kwenye bega ee? R: Kwenye bega I: Labda kulikuwa na kofia yakuendana na mavazi hayo au? R: Zipo kofia lakini sanasana kofia hizi kofia moja hata huyu jamaa anayo nyekundu alafu alafu inavikamba Fulani hivi eeh ya round ilikua tunaita kitunga I: Kitunga? R: Eeeeeh hahahahah I: Hahahahha sawasawa kwahiyo vazi hilo lilikuwa linaendana na kitunga? R: Kitunga, kanzu moja safi sana na kikoi I: Na kikoi? R: Eeeeh kinakaaa hapa yeah I: Sawasawa na unadhani kitu hiki umesema kimepitwa na wakati watu hawataki kurudi zamani kitu gani kinapelekea wasivipe thamani vitu vya zamani? R: Ni utandawazi I: Mhhh R: Eeeeeh utandawazi na hii mnaita new generation kizazi kipya hiki kinabadilisha mifumo na kuiacha kwamba haifai eeh I: Kwa sasa vizibao kama hivi vinatengenezwa? R: Hapana vinatengenezwa kwa mfumo mwingine lakini sio mfumo wa kifalme kama huu I: Huu ni mtindo wa kifalme? R: Yeah maana wanaita choniline umekatwa choniline kwanza alafu hii unaivaa na kitu kingine kuna mashati mengine ya rangi tofauti kwahiyo huyu bwana anapenda penda eeh anajua huyu bwana hahahahaha I: Kwahiyo vingi vilikuwa vina letwa kutoka nje? R: Ndiyo I: Havikuwa vinazalishwa mikoani? R: Hapana kwasababu hata viwanda vya nguo wakati huo vilikuwa bado vichanga sana vilikua havijaanza kuzalisha I: Vilikuwa hamna viwanda? R: Japokuwa material yote yalikuwa yanatoka huku yanaenda alafu tunarudishiwa tena I: Unaweza ukatuambia nyenzo zilizotumika kutengeneza kizibao hiki? R: Hiki hapa I: Ehee R: Nafikiri ni nyuzi, ila siwezi jua nyuzi za nini lakini nikiangalia kwa mbali kama vile ni mgono eeh either mgono lakini ni nguo moja ngumu kidogo iliyetengenezwa kwa nyuzi ngumu eeh I: Sawasawa R: Sina uhakika za mti gani au za zao gani lakini ni kitu kigumu kama gome gome la mti hivi I: Mhhh R: Yeah I: Unadhani kuna mabadiliko ya nyenzo zilizotumika kutengeneza kizibao hicho na kizibao na vizibao vinavyotengenezwa sasa hivi? R: Eeeeeh tofauti I: Totauti na vizibao vya sahivi ni nini? R: Vya sasa hivi havina nakishi kama hichi ninachokiona hapa kuanzia huku, hapa na hizi pamba ambazo zipo inapendeza huoni kwanza ni nilisema ni mnyama nilifikiria ni mdudu dudu hivi siunaona? I: Eeeeh R: Naona kama ni mdudu ni kitu gani iko vizuri yeah I: Labda kizibao hicho kwa muonekano wake kikiletwa katika mazingira ya sasa kinaweza kikauzwa shilingi ngapi? R: Hiki hapa kwa sasa ah kwa sasa kinaweza kuwa na thamani ndogo sana kwasababu hakina jina kwasababu hakina jina kinaweza kuwa na thamani ndogo I: Ndogo kama shilingi ngapi hivi? R: Sana sana labda utauziwa elfu thelathini eeh elfu thelathini, ishirini na tano kwasasa kwasababu hakina jina I: Hakina jina R: Lakini kwa hapo nyuma kilikuwa kina bei I: Hapo nyuma unafikiri kilikua kinauzwa shilingi ngapi? R: Hapo nyuma kwa hiyo hela ya zamani sikumbuki kwa kweili huu mwaka kimetengenezwa sijui hela walikua wanatumia senti tano tano hizi, senti mbili ni hela kubwa wakati huo ilikuwa hivo

chanzo: Amani-Stade Project / Amani Field Research 2023, Interview No. 5
mwandishi: I: Mohamed Seif, R: Anonymous
Mtu
  • National Institute for Medical Research (NIMR) (Mteja)
  • unknown actor (wissenschaftlicheR BearbeiterIn)
Mahali
  • Amani
Scientific use:
Wakati
2023-06-15
Maelezo
I: sawa, tunaenda kwenye picha nyingine, hapa nina picha ambayo imesajiliwa kwa namba 2018_18384, hebu angalia, unatambua hicho ni kitu gani R: haya ni mavavi ya wajumbe, yaani ni kama hivi jumbe joho ambapo sasa hivi wanasema ni madiwani sijui waheshimiwa wabunge, lakini sasa hivi haya mavazi ukiyaona ni ya watu wakubwa sana... I: yalikuwa yanaitwaje kwa kipindi hicho mavazi kama haya R: kwa kipindi hicho walikuwa wanaita ‘vikoi’, yani baada ya kuvaa kanzu unavaa na kikoi, lakini kikoi sio mtu wa hovyo hovyo ambaye alikuwa anavaa, waliokuwa wanavaa ni watu ambao ni maarufu kama 'jumbe salimu, jumbe kika, jumbe joho. I: hao majumbe walikuwa ni wakabila gani R: sana sana ni wa kilindi, hao wengine ni wadoe tu, lakini ni wakilindi ambao wanamaliza kesi, akikuambia unakwenda kufungwa unaenda kufungwa ndio walikuwa wanavaa mavazi hayo, na mkimuona kama jumbe joho, tena akiingia kwenye mji wenu mnatafuta hata mbuzi ili mchinjie kwamba kuna mambo ambayo mnayaweka sawa I: na walikuwa wanayapata wapi mavazi haya R: mavazi haya kwa kweli kuna DC au PC, yani kuna watu ambao wako kwenye serikali ndio wanajua kwamba tukija hapa tumkute joho ndio wanatoa hili vazi, ambapo hili vazi nalo sijui wanaliotoela wapi, aitha wamelinunua huko wanaleta, na hao wanaleta kwa mtu maarufu kwenye kile kijiji, unaona mpaka sasa hivi kuna jumbe kama akina jumbe salimu hapa na wengineo akina jumbe mdoe, wazungu wametusogeza ndio maana sasa hivi hatuna maeneo, sasa kwa vile ameshavalishwa hili anasema tunapanda chai na sisi tunakubali tunalipwa hela na tunaachia mashamba yetu... I: na wao ndio walikuwa wanamamlaka kwa wananchi wao? R: ndio akisema hasa kwa kilindi, na akivaa vazi hili sio kwamba ni siri, akikuambia huyu mke ni mamurugu anamchukua, muulize hata mzee chei, anakuambia ni mamurugu kwamba yule mke wako sio wa kwako tena anamchukua akivaa vazi hilo, I: anacheka... R: sio kwamba ni siri, akishavaa vazi lile jua ni bwana mkubwa hata akiingia nyumbani mwako wewe uko radhi uangalie kando lakini akikuambia mke wako ni mamurugu kweli anamchukua, na ndio maana utakuta makabila wengi sasa hivi.tume... sijui ni nini, hata mzee chei hili analijua hili vazi na anajua baba zao walivyofanya, maana utakuta mzee chai kwenye nyumba yao sio ajabu walikuwa wanawake wengine walikuwa ni wanawake wa watu wameletwa mle, ndio unakuta kuna makabile mengi, wengine ni weupe, wengine ni weusi, lakini ni majumbe ndio wanaovaa mavazi haya I: walikuwa wanavaa kipindi gani mavazi hayo R: haswa kipindi cha siku za kesi au siku za sherehe, au siku kama kuna ngoma hizi ambazo wenyewe wanakwenda kutambikia au kuna mkutano fulani sio wa kijiji, ni mkutano ambao labda labda watoto wanataka waende wakathiriwe au wakafanyiwejando, basi wanavaa hili na hao wenyewe ndio wanakaa kwenye vile viti vya kifalme wanaamua kitu kama hicho, lakini haya mavazi mimi nayakumbuka kabisa mzee jumbe joho au kama kuna mwenzake amefariki anataka arithi basi anavaa hili na kanzu yake na fimbo yake, anakua na fimbo na kanzu na hii scarf, basi akija pale akishachukua bunduki yake... sio hizi bunduki za sasa hivi , kuna zile bunduki za kuchochea hivi, magobole yale, akipiga hapo basi unajua huyo atarithi huyo mke, yuko radhi ajaze hata wanawke sita wenzao kama wamefariki ambapo sasa hivi watu hawataki kurithiana kwa ajili ya maradhi, kweli sio kwamba ni siri haya mavazi yananikmbusha mbali kwamba ni ya majumbe I: majumbe walikuwa wanaanzi umri gani na ni wa kike au wa kiume R: ni wa kiume haswa I: kuanzia umri gani R: mtu akishafikisha kama miaka 40 au 30, akishaozeshwa basi, 40, 50 na kuendelea, akiozeshwa basi na huwezi ukaoa kama sasa hivi, ukitaka kuoa wanakuambia uende nyumba ya mohamedi ukaoe mtoto wake, sio kama sasa hivi tu mnakutana mitaani, ni ile nyumba babayake ni mzuri na mama yake ni mzuri na huo ukoo utakuwa ni mzuri I: sawa, sawa, vikoi kama hivyo vinatumika hivi sasa? R: ah, sasa hivi si watakucheka wote: wanacheka I: unadhani kwa nini watakucheka sasa hivi ukiva kikoi kama hicho R: mambo ya kale hayo, unaona hata suruali zetu sasa hivi, hata sisi wazee pia tunajitahidi tuvae suruali za kisasa, sijui ni kwa nini na watu tunaenda na wakati, kisha mavazi kama haya yalikuwa yanasinga na ni mavazi yenye heshima lakini watu hawayapendi wanakuambia umepitwa na wakati, zamani ukivaa lile lo, hata akina mama huko wenyewe wanajua anapita jumbe sio ajabu atanipenda mimi, na watu wa zamani walipenda sana wanawake weupe, sijui kwanini, kwamba ukioa mke mweupe ujue atakwenda na majumbe tu wote: wanacheka... R: sio siri, ndio maana wakilindi wengi... usioe mke mweupe kilindi atamchukua atamchukua tu, wajumbe wanaovaa haya watambeba tu, sijui kwa nini wenyewe. I: na wao vazi hilo lilikuwa lina umuhimu gani kwao R: halina umuhimu bali tu ni kitu ambacho unajua kwamba huyu ni fulani, kama hivi wachezaji wa mpira kuwatambulisha ni timu gani, hata akiingia kijiji hiki hata humfahamu lazima tutaamka tukampokee jumbe na wote hata kofia tunaona wote, tena kwa kumuongoza vizuri, na awe anaenda kwa jumbe salimu, au anaenda kwa jumbe kika au kwa jumbe nani, anauliza jumbe fulani yuko wapi, mnamwambia yuko hapo basi mnampeleka, tena kwa mwend wa pole pole, si ana lile vazi... wote: wanacheka... I: na labda niulize, jumbe yule anaweza akaja ameoa labda ana miaka 40 lakini ndani ya ile jamii kuna watu wa miaka 60,70 ,80, akiwa amevaa hilo vazi hata hao wazee pia wanamheshimu? R: wanaamka, lazima wataamka, wewe labda huna asili ya ukilindi au huna asili ya kuvaa haya, sijui unatafuta kwenda kupigwa kigongo uende ukafie huko halafu watu kaburi yako watu wasiione, lazimu wamuheshimu hata kama unamiaka 50, 60, 70, lazima umuhesimu jumbe, yani kama mambo ya kifalme, haya mavazi mimi ninayakumbuka sana, na labda wengine walilirithi lakini baadaye sijui mavazi yalikwenda wapi, ninakumbuka hapa nyumbani kulikuwa na mzee mmoja baba yake huyu mkande atakuambia hili vazi, ilikuwa siku za iddi wakishamaliza sijui siku 30, akilivaa hili halafu na fimbo yake na scarf yake basi wanacheza, yani kama umwinyi mwinyi... I: umesema kulikuwa na kanzu, fimbo, scarf na kikoi, ni kitu gani kingine walikuwa wanavaa pamoja na vazi hili R: kilemba I: cha rangi gani R: rangi aina yoyote lakini sana sana kuna vilemba vile vya rangi nyekundu, au nyekundu, vinafanana na hivi hivi, kulikuwa kuna mavazi wajerumani sijui waliwaletea kutoka ujerumani, utafikiri ni kama wale maaskofu, ni mavazi kwa kweli kwanza huwezi ukaligusa na wala halifuliwi na mtu yoyote... I: anacheka... R: labda mke wake wa kwanza ndio anaruhusiwa kuligusa, na hapo lipo kwenye sanduku za mbao likitolewa hilo kuna manukato fulani ya dawa za sanduku, akitoka jumbe hapo anaangaliwa maana tunamgojea jumbe, hayo maelezo ninayoeleza ni vitu ambavyo nimeviona kwa macho yangu nikiwa sijui niko darasa la 5 la 6, nawaona nikasema hawa watu... baba alikuwa ni muislamu lakini baada ya kusoma misheni ikabidi aingie ukristo, na mimi nilikuwa naona nauliza haya mavazi wanayatoa wapi, mimi mwenyewe tu nina kaptula huko ndani sina chochote, lakin ile kaptula na shuka ile... I: labda unaweza ukatuambia kwa sababu mavazi hayo umeyaona, ukiangalia yalikuwa yanatengenezwa kwa kutumia kitu gani R: mh, hapo sijui labda huko ujerumani kwao, lakini sana sana ni pamba ambalo tulikuwa tunalilima sisi wenyewe, pamba ambalo tunapeleka nje, pamba katani, ni vitu vingi na vitu vingi sisi tulikuwa hatujui thamani yake, tunalima tu lakini wenzetu wakija wanachukua, sasa hivi hata huyo jumbe aje avae hivi utasikia 'huyu mzee ana nini, anaenda wapi sasa hivi', lakini mzee utampata nani sasa hivi, lakini mzee utampata nani sasa hivi, labda kama mzee chei tu ndio kama amebakia sasa hivi, lakini wazee wengi jumbe salimu amefariki,na kuna wazee wengi sana ambao walikuwa wanavaa hayo mavazi ambao ndio wajumbe, sisi wengine tulikuwa tunaitwa wadoe, yani wdoe ni watu wanaosikiliza kesi tu, lakini mwenye vazi hili ndio amekaa kwenye kile kiti kama pale Chemka , mzee jumbe joho au jumbe mkande pale Chemka, yani wana ngazi zao, ukitoka huku Kazita kuna jumbe, lakini kuna jumbe wao mkubwa kama yule mzee wa hapa Derema hapa Kwekuyu, jumbe joho yule naye alikuwa ni mtu mmoja maarufu sana, hata amani kule akiingia wazungu pia walikuwa wanamjua kwamba ni jumbe joho, hata akitembea mwendo wake anatembea pole pole, haya mavazi kwa kweli yana sifa zake zamani kwa kweli, sasa hivi hamna I: labda tulilete vazi hili kwa hali yetu ya sasa, likikutwa sokoni kwa anayejua thamani yake anaweza akalinunua shilingi ngapi ukikadiria kwa sasa R: ah, watakuambia labda elfu 10 au elfu 20 au hata 50 mtu anachukua lakini... ni mavazi yenye thamani kubwa sana lakini sasa hivi mtu tena hata anaweza hata bei asiliulize asilione umuhimu wake maana hajui umuhimu, inatakiwa ukinunua kitu labda una umuhimu nacho lakini kitu ambacho huna umuhimu anaweza akakuambia nikupe shilingi elfu 5 nimpelekee babu yangu, ambapo kwamba zamani thamani yake ilikuwa ni kubwa sana. I: na kwa maelezo uliyotuambia kwa sasa ingeuzwa ghali sana kutokana na hadhi ya hilo vazi jinsi lilivyokuwa likitumika R: ingekuwa hata laki tatu nne mtu anannua kwa sasa hivi , halafu kuna haya mashada ambayo yako humu kwenye kola, hivi vitu ambavyo ni vya thamani sana; kwanza hata kumsogela huyo jumbe akiwa kavaa hivyo sio rahisi kwa kweli, kwa kweli sio siri wenzetu wa zamani wamefaidi sana na heshima zao wamezipata, na sijui kama vitarudia tena hivi, sasa hivi tu mtu ni mwenyekiti lakini anaambiwa wazee benchi lote limeoza hilo, zamani useme hivyo si una... Wote: wanacheka R: sio siri, sasa hivi umekaa pale wewe ni mwenyekiti halafu ah, benchi lote limeoza hili... I: unataka kupigwa rungu... R: kwanza utathubutu hata kunyosha kidole... wewe unaangalia chini tu hivi, sivyo huendi kuzikwa, ndio maana utakuta kuna sehemu nyingine zenye mapango kule, utakuta mafuvu; utasikia huyo nenda ukamgone rungu, hata ukizaa mapacha wanaua mmoja abaki mmoja au wote wanauwawa I: kwa nini R: walikuwa wanasema sio vizuri watoto wawili, yaani wanasema sijui ni mbegu mbaya yaani hawatasikia, lakini sasa hivi kumbe mapacha ndio ambao wana akili, lakini zamani ukizaa mapacha au zeruzeru wanawaua

chanzo: Amani-Stade Project / Amani Field Research 2023, Interview No. 21
mwandishi: I: Mohamed Seif, R: Anonymous
Mtu
  • National Institute for Medical Research (NIMR) (Mteja)
  • unknown actor (wissenschaftlicheR BearbeiterIn)
Mahali
  • Amani
Mwandishi: Karl Braun, Tarehe ya kutengenezwa: 1909-04-10, Nukuu/Angalizo: Museum der Kulturen Basel, VI 56197, 53 (43-50)jifunze zaidi
Mwandishi: Karl Braun, Tarehe ya kutengenezwa: 1908-08-30, Nukuu/Angalizo: Museum der Kulturen Basel, VI 56197, 52 (59-60)jifunze zaidi

Rejeo la ndani la kitu

Vest nyeusi na embroidery

Vest nyeusi na embroidery

r 2018 / 18374
Rejeo la ndani la kitu
Kuhusiana na
Asili ya data ya kitu
Museen Stade
Leseni
Creative Commons Namensnennung, nicht kommerziell, keine Bearbeitung 4.0jifunze zaidi
Imepitishwa katika lango imewashwa
2025-12-04T15:51:11+01:00

Rekodi zetu za takwimu zinafanyiwa maboresho kila mara. Tafadhali wasiliana nasi ikiwa una maswali au maoni au ikiwa unahitaji taarifa zaidi au nyingine zinazohusu mali hii. Taarifa juu ya ulinzi wa takwimu.
Rudi kwenye utafutaji