Hinweis: Um die korrekte Darstellung der Seite zu erhalten, müssen Sie beim Drucken die Hintergrundgrafiken erlauben.
Slider Bild - CC BY-NC-ND 4.0
1/1

Zumbe fimbo

Sammlung Braun
r 2018 / 18320
Taasisi inayotoa
Museen Stade
Eneo la Mkusanyiko
Sammlung Braun
Nambari ya uvumbuzi
r 2018 / 18320
Kichwa
Zumbe fimbo
Vipimo
Urefu: 83cm
Nyenzo
Wood
Kiungo cha dondoo
https://www.amani-stade.gbv.de/item/sw_ms_720b38cc-9221-49d4-9e0c-48a5f1b2aaa7
nakala kwenye ubao wa kunakili
Kikundi cha kitu / kitu cha mtu binafsi
Kitu cha mtu binafsi
Uzalishaji
Wakati
mpaka ca. 1908-10-31
Mtu
  • Person (Mtengenezaji)
Mahali
  • Muheza
Kununua / Uuzaji
Wakati
1908-10-31
Maelezo
„Jumamosi 31. X [mwezi wa kumi] 1908 [imepigwa mstari] Nimefanyia kazi mimea yenye utembo wa karatasi. – chakula cha jioni kwa Prof Zimmermann, kwa sababu walipika "utumbo " chakula kizuri & nadra sana. Baadaye mchezo wa kuviringisha tufe Lakini jioni imevurugika kwa sababu Dr Mücke amegombana na Raab kwa sababu ya "mambo ambayo hayajapangwa" nimepata kitu kizuri sana fimbo iliyochongwa toka shina la mti lenye mzizi imechongwa na mwanamume kutoka Bondei fimbo inaonesha sungura –, kichwa cha "Sungura". Nimeilipia hela 40. [mchoro makini wa mwisho wa fimbo]" [Utafsiri]

chanzo: Museum der Kulturen Basel, VI 56197, 52 (85)
mwandishi: Karl Braun
Mtu
  • Mtu, haijulikani (Mchuuzi)
  • Braun, Karl (* 1870 † 1935) (Mnunuzi)
    GND Explorer
Mahali
  • Amani
Malipo
Wakati
kutoka 1908-10-31
Maelezo
"104. Mpini umeota hivyo ukaboreshwa / kazi ya Bondei. Mwenyewe amesema unaonesha kichwa cha sungura / Amani 31. mwezi wa tano. 1908 = hela 40 Heller / TB 52,85. / [mchoro]" [Utafsiri]

chanzo: Museen Stade, r 2018 / 18566
mwandishi: Karl Braun
Mtu
Nambari za hesabu za zamani
  • 104
Urithi
Wakati
1934-07-17
Maelezo
Mnamo mwaka 1934, aliyekuwa mkurugenzi wa Taasisi ya Biolojia ya Kilimo na Misitu (Biologische Reichsanstalt für Land- und Forstwirtschaft) Karl Braun (1870–1935) alitoa kile kinachoitwa “Kolonialsammlung Braun” (Makusanyo ya Mkoloni Braun) kwa Jiji la Hanseatic la Stade, au tuseme aliyekuwa mwakilishi wake, meya wa wakati huo Hans Arthur Meyer (1884–1961). Tazama faili „Uhamisho wa makusanyo ya kikoloni kutoka kwa diwani mkuu wa serikali Profesa Dk. Karl Braun huko katika Jiji la Stade” („Überlassung einer Kolonialsammlung vom Oberregierungsrat Professor Dr. Karl Braun in Stade an die Stadt Stade") katika Jimbo la Saxony ya Chini Hifadhi ya Nyalaka ya Stade (Niedersächsischen Landesarchiv Standort Stade).

chanzo: Niedersächsisches Landesarchiv Standort Stade, Dep. 10 Nr. 03025
Mtu
  • Braun, Karl (* 1870 † 1935) (Mfadhili)
    GND Explorer
  • Hansestadt Stade (Mpokeaji)
  • Hans Arthur Meyer (1884 - 1961) (Mpokeaji)
Mahali
  • Stade
Mkopo
Wakati
1997-02-17
Maelezo
Mnamo mwaka 1997, aliyekuwa mtunza kumbukumbu wa jiji kwa wakati huo Jürgen Bohmbach anahitimisha makubaliano ya makabidhiano kwa mkopo wa kudumu katika Jumba la Makumbusho (Museumsverein Stade e.V.) chini ya aliyekuwa mkurugenzi wa wakati huo Gerd Mettjes kwa kutia saini. Baadaye, makusanyiko kutoka kwa Karl Braun yalihamishiwa kwenye Jumba la Makumbusho (Museumsverein Stade e.V.) kwa ajili ya utunzaji.

chanzo: Museen Stade, Vereinbarung Leihgabe "Brauns'sche Kolonialsammlung"
Mtu
Mahali
  • Stade
Scientific use:
Wakati
2023-06-08
Maelezo
[...] R: huyu namuona kama ni kiumbe hai I: kiumbe gani huyo R: hawa nyoka zamani walikuwepo, sasa hivi naona kama wametoweka I: kwa hiyo ni nini, ninyoka au nini, hebu angalia vizuri R: huu mimi naona kama ni mti, na huu mti ulikuwa dhamira ni kama fimbo lakini ukarembeshwa na kichwa cha nyoka, mimi ndio nimefikia hapo sijui nitakuwa nimekosea au

chanzo: Amani-Stade Project / Amani Field Research 2023, Interview No. 01
mwandishi: I: Mohamed Seif, R: Anonymous
Mtu
  • National Institute for Medical Research (NIMR) (Mteja)
  • unknown actor (wissenschaftlicheR BearbeiterIn)
Mahali
  • Amani
Scientific use:
Wakati
2023-06-09
Maelezo
I: Sawa nina picha nyingine hapa ambayo imesajiliwa kwa namba 2018_18320_001 hebu angalia unaweza ukafahamu hicho ni kitu gani? R: Huu ni mkongojo huu I: Huo ni? R: Mkongojo I: Mkongojo? R: Eeeh ni fimbo ya kutembelea wazee I: Fimbo ya kutembelea wazee? R: Eeeeeh I: Ndiyo ilikuwa inajulikana kwa jina la mkongojo? R: Wasambaa wanaita kome I: Kome? R: Wasambaa wanaita kome lakini kwa lugha ninayoitambua mimi ni mkongojo naifahamu kwa jina hilo I: Mkongojo ni fimbo ya kutembelea? R: Wazee ambao wanahitaji msaada mwingine tuseme anayetegemea nguvu ya mkono ili aweze kutembea maana wanatembea lakini mkono lazima uwe unakita mahali fimbo kama hivi eeh huu ni mkongojo huu I: Kwahiyo ni watu tu ambao hawajiwezi kutembea au hata watu wengine ambao wanajiweza wanaweza kutumia mkongojo? I: Kwahiyo wengine wanatembelea kama fashion na wengine wanatumia kuwasaidia kutembelea? R: Eeeeh I: Kwahiyo umesema kisambaa ni mkongojo? R: Kome I: Kome R: Eeeeh I: Mkongojo ni kilugha gani sasa? R: Ni lugha mchanganyiko kwa waswahili na wasambaa eeh I: Na watu wa utamaduni gani walikuwa wakitumia sana hiyo mkongojo? R: Utakuta kuna baadhi ya watu wa ngoma nyingine utakuta pale kashika baadhi ya ngoma Fulani wanashika mkongojo I: Kama ngoma gani labda, kwa makabila ambayo yapo mkoa Tanga yalikuwa yakitembelea mkongojo? R: Hii kanda ya milimani sanasana ndiyo wanatumia mikongojo I: Kwa maana ya kabila gani? R: Wasambaa I: Ni wasambaa? R: Eeeeeeh hata hii kanda ya bonde hii kanda hii ya tambarare ya bonde unakuta kuna baadhi ya wazee wengine wana mikongojo yao I: Kwahiyo mkoa wa Tanga? R: Mkoa wa Tanga eeh I: Kwahiyo ilikuwa inatumika kwa ajili ya kutembelea? R: Eeeeh kutembelea mwingine anatembea nayo kama vile silaha yake kitakachomtokea inamsaidia kukipiga I: Kwahiyo ilikuwa inatumika kama nyenzo ya kutembelea? R: Eeeeh I: Kama silaha? R: Ndiyo I: Na nyingine matumizi mengine ilikuwa ikitumikaje? R: Kama vile ni fashion I: Fashion? R: Eeeeeh I: Hahahha watu wa hadhi gani walikuwa wakitembelea mkongojo? R: Umri tuseme uliopanda juu kidogo I: Kuanzia miaka mingapi? R: Kuanzia miaka 50 kwenda mbele huko 60 utakuta mkongojo haumuendei mbali lazima atumie kutembelea I: Wa kike au wakiume? R: Wote huuu bwana hauchagui mume wala muke I: Ndiyo R: Eeeeh I: Kwasasa unadhani bado mkongojo unatumika? R: Unatumika eeh I: Unadhani itafika kipindi mkongojo utakuwa hauna thamani tena kwa watu wanaoutumia? R: Haushuki thamani I: Kwanini haushuki thamnai? R: Ni kitu ambacho hakipingwi I: Ukisema hakipingwi unakuwa unamaanisha nini? R: Kwamba hutafokewa kwamba bwana we usitembee na mkongojo leta mkongojo nyumbani ni kitu ambacho kina supportiwa kwasababu hospitali kama umekwenda kule umetenguka mguu unapewa eeh ya kutembelea I: Sawasawa R: Ili ikusaidie I: Na ili utumie mkongojo ulikuwa unahitaji kitu kingine pia uwe nacho ili uweze kutumia mkongojo? R: Hauna kitu kingine cha kutegemea I: Sawasawa unadhani kilikuwa na umuhimu gani kwa tamaduni za watu waliokuwa wakitumia mkongojo? R: Kama nilivoongea hii bwana ni lazima kama unamapungufu kidogo kwenye mwili wako au miguu yako lazima utembee na mkongojo eeeh kusaidia mapungufu uliyonayo kwenye mambo ya miguu au katika balance yako ya mwili pia lazima atumie mkongojo ili ile balance ibaki pale pale I: Na bado wanaendelea kutengenezwa mkongojo? R: Inatengenezwa ndiyo I: Ni maeneo gani vinatengenezwa? R: Hii haichagui mahali popote pale unatengenezwa tu hata mtu unaenda porini kaniletee mti nataka nitengeneze mkongojo wangu anaenda kule anakukatia mti unafaa ana uchonga vizuri ukikauka basi mwenyewe anatembelea I: Aaaa kwahiyo ilikuwa inachongwa na mti? R: Ni mti I: Mti wa aina gani? R: Mti ambao unavumilia mti ambao ni mgumu I: Mti mgumu? R: Eeeh usio katika katika hovyo I: Mhhh sawasawa na waliokuwa wanatengeneza mkongojo ni akina nani wa kike au wakiume? R: Wakiume lakini kuna baadhi ya wakike hata kama either ana tofauti zake za kimwili hana mtu atakaye mtengenezea akikuta hapo mti ulionyooka vizuri anachukua panga lake anakata, anakata vizur size yake basi anatembelea lakini wanaotengeneza sanasana walikuwa wakiume ninavojua mimi I: Wa umri gani? R: Wanaotumia hii au wanaotengeneza? I: Eeeeh R: Ni hawa watu wazima I: Watu wazima? R: Eeeeh I: Lakini huo unaona umechongwa vizuri unanakishi nakishi? R: Ni hivi alivoukuta huko basi alivoupata akaja nao kama ulivo kaweka sehemu hapa huku kwa kushikia na huko kwa kushikia umechongwa vizuri eeh japo anachukua chupa anakwangua na chupa inakuwa laini I: Na kuna nyenzo nyingine zinaweza zikatumika kutengenezea mkongojo tofauti na mti uliosema mti mgumu? R: Eeeh unaweza ukawapata hawa wahunzi wa vyuma hawa I: Wahunzi wa chuma? R: Eeeh lakini upate chuma ambacho siyo kizito eeh kuna mabomba fulani hivi mepesi lakini ni imara yanavumilia anaweza akakutengenezea lile akalinakishi vizuri ukapata mkongojo wako mzuri sana I: Sawasawa na mkongojo kama huu ulio designiwa vizuri kiasi hiki kwa hali ya sasa unaweza ukauzwa shilingi ngapi? R: Huu? I: Eeeeeh R: Jinsi ulivo unajua saivi hela kuitamka shilingi elfu 10 au elfu 5 ni kitu laini sana siyo kama zamani unamtajia mtu shilingi 100 ilikuwa ikitumika lakini sasa anashituka unaniambia shilingi ngapi lakini kwa saivi unamtajia yoyote tu I: Anashituka? R: Eeeh lakini siku hizi kutamka 100 anakwambia hivi unaakili kweli wewe nikuuzie kwa shilingi 100 hii I: Hahhahha R: Anaweza akakwambia shilingi elfu 5 au elfu 6 jinsi gani alivokuona na huo mti kautoa wapi I: Kwa jinsi ilivo hebu iangalie ilivonakishiwa R: Ndiyo nimeuona hapa ndiyo maana anakwambia nipe shilingi elfu 10 kwasababu ameipenda anatoa anachukua I: Kwahiyo inaweza ikauzwa shilingi elfu 10 R: Ndiyo maana ukiangalia kama mbuzi huku kawekwa jicho hapa na mdomo huu hapa na haya huku ni masikio haya

chanzo: Amani-Stade Project / Amani Field Research 2023, Interview No. 04
mwandishi: I: Mohamed Seif, R: Anonymous
Mtu
  • National Institute for Medical Research (NIMR) (Mteja)
  • unknown actor (wissenschaftlicheR BearbeiterIn)
Mahali
  • Amani
Scientific use:
Wakati
2023-06-15
Maelezo
I: sawa, tuna picha nyingine hapa imesajiliwa kwa namba 2018_18320_001 hebu angalia, unaweza ukatmbua ni kitu gani hiki R: hii ni fimbo tu ambayo wale wanaovaa majoho ndio wanashika hizi fimbo I: hizo fimbo zilikuwa zinaitwaje kisambaa R: hapa mbele wanaweza wakachonga kama wanavyofanya wamasai, wanachonga kama sura ya mtu au mnyama wa aina yoyote, lakini sana sana kuna miti ile wanaita mpingo ambao ni mgumu sana ambao wanachonga, ni fimbo ambayo wale wanaovaa majoho wanapenda sana kisha hizi wale wa kilindi, huoni kama hii hapa sio ndege huyu ambaye amechorwa... I: ni kama sungura hivi R: ni kama sungura na masikio, sasa hata wewe unayempokea... I: ilikuwa ina jina maalum fimbo hiyo ikitumiwa na hao watawala R: wanasema fimbo ya mfalme au ya jumbe, na hazishikwi na watu, zinashikwa na watu maarufu I: kama hao wa kilindi... R: wa kilindi haswa, wa kilindi wenzetu walichukua nafasi kubwa sana ambao hata sasa hivi kweli sio siri hawako ...sio wale wa kilindi, walikuwa ni a kipindi hicho, sasa hivi ukiitwa mkilindi unasikia 'ah achana na mkilindi wamekuwa hapo zamani', manake zamani anaweza akakuambia huyu mke ninamchukua mimi, tena sio kwamba anamchukua, akishamuangalia anawaambia 'nendeni kwa bwana hiza, mwambieni yule awe wamurugu' akishaitwa jina la 'wamurugu', kweli akija anachukuliwa anakuja kwenye nyumba, au kama sivyo anawambia kama hamuamini nendeni na hii fimbo, akija anaambiwa hii fimbo ni ya jumbe... I: fimbo kama hii R: ee, kama hii, hii fimbo ni ya jumbe, na hakuna mtu mwingine ambaye anaweza akashika hii fimbo, anayeshika hii ni jumbe, sasa anayetakiwa ni mtoto wako eti aende kwa jumbe I: kwa hiyo fimbo ilikuwa inatumika kama sehemu ya kukaba... R: sehemu kama ya kukomoa komoa watu ambao hawana nafasi nzuri, yani walikuwa na vitu vyao, kwa kweli ukoloni na sasa hivi... tuwashukuru wazungu wametulete... na pia tumshukuru na nyerere, lakini ingekuwa bado sasa hivi tuko kwenye mambo ya kutawaliwa, lakini sasa hivi huoni mpaka sasa hivi hata nyinyi pia mmepata elimu mnakumbuka mambo zamani hvi, kwa sababu hata mimi mwenyewe nisingekumbuka kabisa, yani sio rahisi, lakini serikali sasa hivi inatumia utafiti huu, ujue kwamba ni jambo la kukumbusha, mzee chei pale pia si unaona kuna sahani zile pale zina mtu anachota maji na sahani ni ya dongo. I; fimbo kama hizi zilikuwa zinapatikana zaidi katika mikoa gani hasa R: mkoa wa tanga, handeni, hasa hasa mkoa wa tangau masaini huko, singida huko, kama hivyo akina chifu mkwawa, iringa kule, iringa bado mpaka sasa hivi mambo ya mila wanayo, bado iringa wana mambo ya mila, yani iringa na huku kwa chifu mkwawa na huku tanga kwa wakilindi, wakilindi walitawala sana, wabondei walikuwa naona safi I: kwa hiyo sasa hivi haitumiki kabisa hii fimbo R: sasa hivi kwamba kuipata, utaipata wapi, na watu wanajtahidi wanatafuta tafuta fimbo kama hizi, sasa miti iko wapi ni mbuga tupu, ilikuwa zamani tembo na chui zinapita humu, mbuzi wanakimbizwa na chui, sasa hivi hata sehemu za kuchungia hamna, ni mashamba tu I: kwa hiyo hata kutengenezwa sasa hivi hazitengenezwi tena R: kwanza ukishika fimbo wanakuambia ‘huyu naye anajiingiza kwenye uzee’ wote: wanacheka R: fimbo tu nasema inisaidie kama ile ya mzee chei pale, anakuambia mbona umekuwa mzee mara hii, kwa kweli mimi nimeshukuru kwa kunikumbusha mambo ya zamani, yani nashukuru sana I: hebu niambie, fimbo hizo walikuwa wanatengeneza watu wa jinsia gani R: kuna watu wenye fani zao kama hizi, unaweza ukaambiwa tengeneza fimbo hii kama watumwa watumwa hivi, unaelekezwa, fanya hiki fanya hiki na wale machifu, tengeneza hivi na hivi, chonga hivi, kuna visu vile vilikuwa vinaitwa okapi, sasa vile vinachonga, vile visu yani ni vikali mno, basi ukija unaambiwa tengeneza hivi, chonga hivi , fanya hivi... I: na hii picha inaonekana inang'aa, inawaka vizuri, walikuwa wakipaka nini mpaka ionekane kiasi hiki R: saa nyingine wanaweza wakapaka mafuta ya ng'ombe, ni sawa sawa na mwanamke akizaa inachinjiwa mbuzi anapakwa yale mafuta, mwanamke akitoka hata kama ni siku mbili tatu unamkuta ameng'aa kwa ajili ya yale mafuta wanayompaka, halafu na mila mara siku ya kwanza siku ya pili mwanamke unamkuta sokoni... wote: wanacheka I: mzee hiza, fimbo hiyo kwa mazingira ya sasa hivi, kwa wewe unayeijua umuhimu wake unaweza ukainunua shilingi ngapi sokoni R: hii ninaweza nikainunua kwa shilingi 20, 30, nainunua ili niwekee watoto kumbukumbu, kama sasa hivi nimeona vitu vya mzee chei pale kamera ile, kuna sumaku, ile kamer ina sumaku, tena yule mzee kuna vitu vingi watoto wake wamebeba beba wale wanaojua, kwa hii fimbo nikiipata ingawa hata siku moja ninaweza nikapita nayo ingaw watanicheka

chanzo: Amani-Stade Project / Amani Field Research 2023, Interview No. 21
mwandishi: I: Mohamed Seif, R: Anonymous
Mtu
  • National Institute for Medical Research (NIMR) (Mteja)
  • unknown actor (wissenschaftlicheR BearbeiterIn)
Mahali
  • Amani
Mwandishi: Karl Braun, Nukuu/Angalizo: Museen Stade, r 2018 / 18566jifunze zaidi
Mwandishi: Karl Braun, Tarehe ya kutengenezwa: 1908-10-31, Nukuu/Angalizo: Museum der Kulturen Basel, VI 56197, 52 (85)jifunze zaidi
Asili ya data ya kitu
Museen Stade
Leseni
Creative Commons Namensnennung, nicht kommerziell, keine Bearbeitung 4.0jifunze zaidi
Imepitishwa katika lango imewashwa
2025-12-04T15:17:36+01:00

Rekodi zetu za takwimu zinafanyiwa maboresho kila mara. Tafadhali wasiliana nasi ikiwa una maswali au maoni au ikiwa unahitaji taarifa zaidi au nyingine zinazohusu mali hii. Taarifa juu ya ulinzi wa takwimu.
Rudi kwenye utafutaji